Monday, 11 December 2017

Hili ndilo Kombora jipya la korea Kaskazini Linaloweza Kuitandika Marekani.

Korea Kaskazini imetoa picha za jaribio la kombora lake jipya ambalo inadai kuwa linaweza kushambulia popote pale nchini Marekani.

Picha hizo zinaonyesha kiongozi wa Korea Kaskazini Ki Jong un na maafisa wengine kadha ya ngazi za juu jeshini wakisherehekea kombora la Hwasong-15 wakati likipaa.

Wengi wameshangazwa na ukubwa wa kombora hilo. Picha hii ambayo haijulikanai ilichukuliwa lini na iliyotolewa na vyombo vya habari vya taifa inaonyesha Kim akilikagua kombora hilo.

Michael Duitsman, mtafiti katika kituo kimoja alisema kuwa kombora hilo ni kubwa kuliko kombora la kwanza la Hwasong-14 "ni nchi chache tu zinaweza kuunda kombora kama hilo na Korea Kaskazini imejiunga nazo."

Pia linaonekana kuwa na kichwa kikubwa ikimaanisha kuwa linaweza kubeba bomu zito la nyuklia kwenye kichwa chake.

Yote haya yanaashiria kuwa kombora hilo lina uwezo kwa kusafirisha bomu la nyuklia kwa muda mrefu.

Lilisherehekewa kwa sigara

Kim mwenye furaha anaonekana akicheka kwa furaha  wakati kombora hilo linapaa. Linaaminiwa kuwa kombora la kwanza la Korea Kaskazini lililopaa mbali zaidi katika kilomita 4,475.

Bw Kim na wenzake walionekana wakisherehekea  mafanikio ya jaribio hilo kwa sigara.

Credit: BBC

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

“Timu ya Taifa si Sehemu ya Kujifunzia Ukocha”-Mwambusi Arusha Dongo.

Kocha aliyetamba na kikosi cha Mbeya City Juma Mwambusi ametoa maoni yake kuhusiana na timu ya taifa ya Tanzania bara ‘Kilimanjaro Stars’ kufanya vibaya kwenye mashindano ya Chalenji 2017 ambapo amesema, timu ya taifa sio mahali pa kujifunzia ukocha.

Mwambusi ambaye amewahi kufanya kazi kama kocha msaidizi kwenye timu ya Yanga ameonesha kusikitishwa na matokeo mabovu ya Kili Stars kwenye mashindano ya mwaka huu na kuongeza huenda ugeni wa mwalimu ukawa moja ya tatizo kwa timu hiyo kushindwa kufanya vyema.

“Kinachosikitisha watanzania ni timu yetu kufanya vibaya sana katika mashindano ya Chalenji yanayoendelea kule Kenya. Kubwa kama mwalimu ni kuelezana ukweli, watanzania wanataka matokeo mazuri kitu ambacho kocha aliyeteuliwa na wachezaji lazima wajitume na kujitolea kwa ajili ya nchi yao.”

“Timu ya Taifa watu wanaitegemea ni kigezo gani TFF wanakitumia kuteua kocha ni swali ambalo nimekuwa nikiulizwa na wadau wengi wa soka kwa sababu wanaamini kutokana na taaluma yangu na uzoefu huenda nikawa najua, lakini hata mimi sifahamu TFF ndio wenye majibu na wanatakiwa kuwajibu watanzania wapenda michezo kwamba ni vigezo vipi wanavyovitumia.”

“Mwalimu huyu ni mgeni katika soka la Tanzania labda kama alicheza lakini hajafundisha kwa sababu lazima ufundishe vilabu vya ligi kuu ili uweze kuteuliwa mwalimu wa timu ya taifa, lakini sio kufundisha tu umefanya nini katika klabu au vilabu ulivyofundisha. Una wasifu mzuri unawajua watanzania unajua utamaduni wa wachezaji wetu, kwa sababu mwalimu anaweza kuwa mzuri lakini anafundisha katika mazingira yapi na yeye katoka mazingira gani?”

“Watanzania wataendelea kuumia hadi lini kutokana na matokeo ya timu yao ya taifa? Isiwe sehemu ya kujaribia makocha ni kutowapa thamani watanzania ambao mioyo yao inapenda sana matokeo mazuri kutoka kwa timu yetu.”

“Nakumbuka Rais mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassani Mwinyi aliwahi kusema “timu yetu imekuwa kichwa cha mwendawazimu” kwa hiyo kuifuta hii kauli ni lazima tufanye vizuri. Inatakiwa timu iwe na mwelekeo, naishauri TFF kwamba walimu wapo waliofundisha ligi kuu wamefanya vizuri wanatakiwa wapewe nafasi wafundishe timu ya taifa tumechoka kuumia, timu ya taifa sio sehemu ya kwenda kujifunzia au kujaribia.”

“Wachezaji tutawalaumu lakini labda waliletewa utamaduni ambao hawajauzoea na wao wanatakiwa kujituma katika timu yao kwa sababu sisi watanzania tunaumia.” 
Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Monday, 4 December 2017

Simba Kicheko Tu....Haya Ndo Mambo 10 Bilionea Mohammed Dewji Atakayoanza Nayo Baada ya Kukabidhiwea Timu Hiyo.

Bilionea Mohammed Dewji ameipokea kwa mikono miwili ishu yake ya ushindi kuwa mwekezaji mpya Simba na ametoa ahadi zake 10 kuhakikisha zinafanyika kuleta mabadiliko makubwa.

Mo Dewji ameshinda zabuni ya kuwa mwekezaji wa Simba kwa dau la Sh bilioni 20 alizoweka ‘mezani’ na hakukuwa na mtu yoyote aliyejitokeza kushindana naye kama ilivyokuwa ikielezwa awali.

MOJA:
Kambi ya Simba itajengwa upya kabisa na itakuwa ni hosteli ya kisasa yenye vyumba hadi 35. 30 vitakuwa kwa ajili ya wachezaji na vitano kwa ajili ya benchi la ufundi.
 
MBILI:
Simba sasa itafaidika kwa kuwa na gym yake ya kisasa, bwawa kubwa la kuogelea kwa ajili ya mazoezi na sehemu ya kupumzika kwa wachezaji.
 
TATU:
Wachezaji, makocha na viongozi watakuwa na mgahawa wao wa kisasa kabisa.
 
NNE:
Mo Dewji anaamini timu lazima iwe na viwanja vya mazoezi. Hivyo ataanza na viwanja viwili, kimoja nyasi asilia na kingine nyasi bandia.
 
TANO:
Mo Dewji ameahidi kuwekeza katika soka la vijana akianza na wale wenye umri wa chini ya miaka 14, 16 na 18 na lengo ni kuwakuza.
 
SITA:
Mo Dewji amesema atasimamia wachezaji kuitambua thamani ya Simba kwa kujituma hasa.

SABA:
Simba itaanza kufanya mambo kimataifa kwa kuitangaza na kuikuza brand ikiwa ni pamoja na kutengeneza vifaa mbalimbali kama fulana, kofia, vishika ufunguo na kadhalika.

NANE:
Ameahidi kutenga kitita cha  Sh milioni 500 ambazo zitatumiwa na benchi la ufundi katika mipango yao kama kambi na kadhalika pia Sh bilioni moja kwa ajili ya usajili.

TISA:
Kushindana na timu kubwa Afrika na sio Tanzania pekee.

KUMI:
Kurejesha Simba katika historia ya kimataifa

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

MENEJA WA ULIMWENGU AELEZA NAMNA ALIVYOVUNJA MKATABA NA TIMU YA NDEMLA SWEDEN.

Jamal Kisongo ambaye ni meneja wa straika, Thomas Ulimwengu, yupo kwenye mchakato wa kuvunja mkataba wa mteja wake huyo dhidi ya timu ya AFC Eskilstuna iliyokuwa ikishiriki Ligi Kuu ya Sweden kufuatia kushuka daraja.

Timu hiyo ndiyo inayojiandaa kumchukua Said Ndemla ambaye amefuzu majaribio akitokea klabu ya Simba ya nchini.

Ulimwengu alijiunga na timu hiyo msimu uliopita ambapo alisaini mkataba wa miaka mitatu na hadi anafikia uamuzi huu hakuwahi kucheza mechi yoyote ya ligi kutokana na kusumbuliwa na majeraha ya goti anayouguza mpaka sasa.

Kisongo alisema kuwa kwa sasa yupo kwenye mchakato wa kumtafutia timu nyingine Ulimwengu ambapo anaamini mpaka Januari, mwakani, atakuwa amepata timu kubwa inayoshiriki ligi kuu na hatarejea Sweden tena.

Meneja huyo aliongeza kuwa kwa sasa Ulimwengu yupo nchini hapa akifanya mazoezi binafsi ya kujiimarisha baada ya kutoka Ubelgiji alikokuwa kwa mapumziko binafsi.

“Nipo kwenye mchakato wa kumtafutia timu Ulimwengu na ninaamini hadi kufika Januari nitakuwa nimepata ile ambayo inashiriki ligi kuu na hatarudi tena Sweden. Tunataka kuvunja mkataba na wale AFC Eskilstuna kwa kuwa imeshuka daraja licha ya kuwa tumebakiza miaka mawili kwenye mkataba,” alisema Kisongo.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

KOCHA NINJE AELEZA KIKOSI CHAKE KILIVYOJITAHIDI CHALENJI..

Kocha Mkuu wa Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars’, Ammy Conrad Ninje amepanga kesho Jumanne Desemba 5, 2017 kuanza kufanyia kazi upungufu ulioonekana kwenye mchezo dhidi ya Libya  uliofanyika Jumapili Desemba 3, mwaka huu.

Katika mchezo huo uliofanyika Uwanja wa Kenyatta ulioko Machakos hapa nchini Kenya, Tanzania Bara ilipata sare katika safari ya kuwania Kombe la Cecafa – michuano inayofanyika hapa Kenya.

Ninje amesema katika mchezo huo wa kwanza waliecheza katika kiwango cha kuridhisha na kikubwa anataka kuangalia namna ya kufanyia kazi upungufu ikiwa ni pamoja na pale timu inapopoteza mpira.

Anasema kwenye mchezo dhidi ya Libya timu ilicheza kuanzia nyuma kupitia sehemu ya kiungo na kuunganisha sehemu ya ushambuliaji – jambo ambalo limemfurahisha kwa namna timu ilivyotengeneza nafasi.

Akizungumzia mchezo unaofuata dhidi ya Zanzibar Heroes, Ninje amesema ni mchezo mgumu kama ambavyo historia inaonesha wakati timu hizo mbili zinapokutana.

“Lakini kuanzia mazoezi ya kesho nitaiandaa timu kupata ushindi na nimepanga kwenda kuitazama Zanzibar itakapocheza mchezo wake wa kesho dhidi ya Rwanda,” amesema.

Amesema ataiangalia Zanzibar Heroes kiufundi ili kubaini upungufu wao ili naye ajue namna atakavyoweza kutumia nafasi hizo kwenye mchezo unaofuata.

“Ni fahari kwa timu zetu hizi mbili kila mmoja kupambana kupata pointi bahati nzuri wao wanacheza kesho kwa hiyo mchezo wao nitautumia kutazama mapungufu (upungufu wao) yao yatakayoweza kutusaidia," alisema Ninje.

Leo Desemba 4, mwaka huu asubuhi kikosi cha Kilimanjaro Stars kimefanya mazoezi ya kuondoa uchovu baada ya mechi ya jana kabla ya hapo kesho kuanza rasmi kujiandaa kwa mchezo huo unaofuata.

Mbarak Yusuph ndiye mchezaji pekee ambaye hakufanya mazoezi hayo baada ya kuumia misuli kwenye mchezo wa jana dhidi ya Libya.
Mbarak atapumzishwa kwenye mchezo unaofuata ili kuwa tayari kuikabili Rwanda.

Leo jioni Kocha Ninje atakutana na wachezaji kuutathmini mchezo wa Libya ambao ulimalizika kwa sare ya bila kwenye Uwanja wa Kenyatta, Machakos.

Kilimanjaro Stars ipo kundi A pamoja na timu za Zanzibar, Libya, Rwanda na wenyeji Kenya.


Kenya wana pointi tatu baada ya kuifunga Rwanda mabao 2-0 wakati Kilimanjaro Stars na Libya wana pointi 1 kila mmoja baada ya kutoka sare ya bila kufungana kwenye mchezo wao wa kwanza wakati Zanzibar na Rwanda wenyewe hawana pointi huku Zanzibar ikiwa haijashuka dimbani katika kundi hilo.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Bunduki ya Nassari Yachunguzwa na Polisi Mkoani Arusha.

Wakati mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari akilihusisha tukio la kuvamiwa nyumbani kwake na watu wasiojulikana na masuala ya kisiasa, polisi inashikilia bunduki ya mwanasiasa huyo kwa uchunguzi.

Polisi mkoani Arusha imesema imeanza uchunguzi wa kina wa kuwasaka washukiwa, huku ikichunguza silaha ya Nassari aina ya shotgun, ikisema tukio hilo lina utata kutokana na mazingira lilivyotokea.

Kamanda wa polisi wa mkoa, Charles Mkumbo aliliambia gazeti hili kuwa wameanza uchunguzi wa kina ili kubaini endapo kulikuwa na tukio au la.

“Tunaifanyia uchunguzi bunduki yake, tunataka kujiridhisha endapo kulikuwa na tukio au la,” alisema Mkumbo.

Hata hivyo, kamanda huyo alisema msako unaendelea ili kuwabaini washukiwa na kwamba hawajapata maganda ya risasi zinazodaiwa kutumika katika uvamizi huo.

Juzi Nassari aliwaambia waandishi wa habari kuwa nusu saa baada ya kuwasili nyumbani kwake alisikia hali isiyo ya kawaida ndani ya uzio wa nyumba na baadaye kulisikika milio ya risasi. Alisema mbwa wake aliyekuwa akibweka alinyamaza, hali iliyomfanya achukue silaha yake kujihami.

“Nilipiga risasi tano, kisha kukawa kimya nikaenda kuwaamsha vijana wanaonisaidia hapa nyumbani kuwaeleza tukio lililotokea kisha nikaondoka.”

Alisema waliofanya tukio hilo hawakujua kama ana silaha kwa sababu mwaka 2014 wakati wa uchaguzi wa Serikali za mitaa, bastola yake ilichukuliwa na polisi na hadi leo haijarudishwa, hivyo kuwa na silaha nyingine kulimsaidia kujibu mapigo.

Katika tukio hilo, Nassari alisema aliwajibu watu hao kwa kupiga risasi tano hewani huku wenyewe wakipiga 12 na moja ilimpata mbwa wake ambaye alimzika juzi katika maeneo ya nyumba anayoishi.

Hivi karibuni mbunge huyo aliwasilisha makao makuu ya Takukuru ushahidi wa CD aliodai kuwa unawahusisha madiwani wa Chadema mkoani Arusha kushawishiwa kuhamia chama taw 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Jumatatu.

26 Job Opportunities at Tanesco Tanzania

Job Opportunity at Tigo Tanzania, Regional Distribution Coordinator

Job Opportunity at EGPAF, Project Coordinator

Job Opportunity at EGPAF, Health Information System (HIS) Officer

Job Opportunity at EGPAF, Technical Officer TB services

Sales Jobs at METL (2 Vacancies)

Nafasi zingine Bonyeza www.ajirayako.co.tz

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Diamond, Tudd Thomas Washinda Tuzo Nigeria.

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz na Muandaaji wa muziki, Tudd Thomas wote kutoka Tanzania wameshinda tuzo za African Entertainment Legends Awards (AELA) jana Desemba 3, 2017 jijini Lagos, nchini Nigeria.

Diamond Platnumz ameshinda tuzo ya kolabo bora ya mwaka 2017 kupitia wimbo wake wa FIRE aliomshirikisha msanii kutoka Nigeria Tiwa Savage huku producer Tuddy Thomas akinyakua tuzo ya Muandaaji bora wa muziki kwa mwaka 2017 barani Afrika.

Wengine walioshinda tuzo hizo ni Davido kupitia wimbo wake wa Coolest Kid in Afrika kwenye kipengele cha ‘Best Music Video of the Year’, RunTown, Black Coffee na wengine wengi.

Tazama orodha kamili ya washindi wa Tuzo hizo za (African Entertainment Legends Awards 2017) . 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Shilole Harusi Yangu Ipo Pale Pale Mwezi Huu.

Zikiwa zimesalia siku kadhaa mwaka 2017 kumalizika, msanii Shilole amezidi kusisitiza azma yake ya kufunga ndoa kwa mwaka huu ipo pale pale.

Mwishoni mwa weendend iliyomalizika katika sherehe ya ndoa ya Dj wa Clouds Media, Dj Zero shilole katika kutoa nasaha zake alisema mwezi huu atafunga ndoa.

Pia hivi karibuni kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Instagram, Shilole alimweleza msanii wa filamu Bongo, Steven Nyerere kuwa harusi yake ipo pale pale.

Shilole ambaye yupo katika mahusiano na mpenzie, Uchebe hivi karibuni walioneka wakiwa wote Igonga, Tabora nyumbani kwa kina Shilole.  July Mwaka huu ndio Shilole alimuweka wazi mpenzi wake huyo na kueleza mwaka watafunga ndoa. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Wednesday, 29 November 2017

Uwoya Amnyima Penzi Dogo Janja Tangu Ndiku Afariki.

Kwa habari za kunyapia nyapia ni kwamba Irene Pancras Uwoya (Sheila Abdul) aanza kumchukia dogo janja kiasi cha kuyumbisha penzi lao na mbaya zaidi amekuwa akimnyima penzi dogo janja na mara nyingi hupenda kumkwepa kwepa janjaro na kiasi fulani anahisi kama janjaro ndo chanzo cha mumewe kipenzi Hamadi Kataut.

Dogo janja mara kwa mara akitafutwa kujibu suala hili la kunyimwa penzi na uwoya amekuwa akibabaika sana na muda mwengine hupenda kujibu nje ya mada ili asiendelee kuulizwa. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Alikiba na Abdukiba Kwenye Kolabo ya Pamoja Kuachia Nyimbo Mpya Kesho.

Baada ya kimya cha muda mrefu wakali kutokea Bongoflevani Alikiba na Abdukiba ambao ni ndugu wa damu wameamua kurudi tena kwenye headlines za bongofleva baada ya kujiandaa kuachia wimbo wao mpya.

Uthibitisho wa kuachia wimbo huo umepatikana baada ya Alikiba na Abdukiba kupost kupitia mitandao yao ya Instagram kwa kuahidi kuwa wataachia Audio na Video kwa pamoja siku ya Alhamisi hii, ambapo Abdukiba ameandika…>>>“The long wait is almost over!!!!King’s Music presents @officialabdukibaanew single featuring @officialalikiba – Audio & Video zinadondoka Alhamisi hii. Subscribe to AbduKiba youtube channel uwe wa kwanza kuiona video ya #Singledirected by @hanscana_#SupportedByKiba#KingKiba..” – Abdukiba


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

TANESCO Wataja Chanzo cha Kukatika kwa Umeme Dar, Pwani.

Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) limetoa taarifa kwa wateja katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani kuwa baadhi ya maeneo hayana umeme kutokana na hitilafu iliyojitokeza.

Taarifa ya Tanesco imesema baadhi ya maeneo ya mikoa hiyo hayana umeme kuanzia saa 3:20 asubuhi ya leo Jumatano Novemba 29,2017 kutokana na mashine namba tatu ya kuzalisha umeme kwa njia ya gesi asilia kituo cha Ubungo II kupata hitilafu.

“Mafundi wa shirika wanaendelea na jitihada za kutatua hitilafu hiyo kwa haraka ili kurejesha umeme katika hali yake ya kawaida,” imesema taarifa ya Tanesco.

Shirika hilo limesema litaendelea kutoa taarifa za maendeleo ya kazi hiyo.

Pia, Tanesco imetoa tahadhari kwa wananchi kutosogelea, kushika wala kukanyaga waya uliokatika au kuanguka.

Uongozi wa shirika hilo umewaomba radhi wateja kwa usumbufu uliojitokeza.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Inasikitisha Baba Amtoa Kafara Mwanaye Amkata Sehemu za Siri kwa Shoka.

MTU mmoja huko mwenye umri wa miaka 39 huko Chhattisgarh, India, amemtoa kafara mwanaye mdogo katika kitendo cha ushirikiana kwa kumkata uume na sehemu za kichwa kwa shoka hadi kusababisha kifo chake, kwa madai ya kufukuza mapepo mabaya ‘mashetani’.

Watuhumiwa wakiwa chini ya ulinzi.
Kitendo hicho kilifanyika huko Balodabazar wilayani Chhattisgarh, polisi walisema jana. Ramgopal Patel, na mganga wa kienyeji, Rajesh Yadav (19) walikamatwa leo, ikiwa ni siku mbili baada ya kufanya kitendo hicho kijijini Amera.
Polisi walisema mwili wa mtoto huyo mwenye umri wa miaka 13 ulikutwa ukiwa katika dimbwi la damu ambapo baada ya polisi kufanya uchunguzi, Patel alikiri kumwua mwanaye huyo ili kuondoa mapepo mabaya na hivyo wamemfungulia mashitaka. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Mabasi ya Mwendokasi Kupanua Wigo Sasa Hadi Sinza, Masaki.

WAKALA wa  Mabasi Yaendayo Haraka (DART) unatarajia kupanua wigo wa usafiri huo kwa kuongeza ruti za Sinza, masaki na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Sambamba na ruti hizo, DART pia inatrajia kuongeza mabasi katika mfumo wake kutoka 140 yaliyopo sasa hadi mabasi 305 pindi awamu ya kwanza ya mfumo huo itakapokamilika.

Mtendaji Mkuu wa DART, Mhandisi Ronald Lwakatare, alisema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari, baada ya kupokea wageni sita kutoka serikali ya Rwanda ambao wako nchini kwa ziara ya siku tano ya kujifunza mradi huo unavyofanya kazi nchini.

“Tunatarajia kuwa hatua ya kukamilika kwa awamu ya kwanza ya mradi huu, itaongeza idadi ya watumiaji wa mabasi ya mfumo huo kutoka 200,000 kwa siku   kufikia watumiaji 400,000 hadi 500,000 kwa siku,” alisema.

Mhandisi Lwakatare alisema mradi huo utaongeza njia  kutoka mbili zilizopo sasa hadi njia  tisa, hivyo kupanua huduma ya usafiri katika maeneo mbalimbali yaliyomo ndani ya mfumo wa DART katika awamu ya kwanza ya mradi.

“Awamu ikikamilika tutakuwa na njia tisa, kuna nyingine zitakuwa zinaenda Masaki, Sinza, Chuo Kikuu na maeneo mengine ambayo yako jirani,” alisema.

Kuhusu athari zilizotokana na mvua zilizonyesha Oktoba 26,  mwaka huu, Mhandisi Lwakatare alisema mfumo wa mabasi uliathiriwa na mvua hizo na mabasi 40  yaliharibika na kati ya hayo 20  yaliharibika zaidi.

Hata hivyo, alisema mabasi hayo  yameshatengenezwa na yameanza kutoa huduma na kwamba wamejipana kuhakikisha mitaro yote inayozunguka karakana ya Jangwani inasafishwa ili kuepuka eneo hilo kukumbwa tena na mafuriko.

“Tumefarijika kupokea ugeni kutoka serikali ya Rwanda kuja kutembelea mradi kwa lengo la kujifunza hatua tuliyofikia ukizingatia kuwa jiji la Kigali nalo lina mpango wa kuwa na mfumo kama huu,” alisema.

Timu hiyo inaongozwa na Rwagatore Etienne kutoka Mamlaka ya Jiji la Kigali akiwa na wataalamu washauri ambao ndio waliopewa kazi ya usanifu wa jiji la Kigali kuwa na mfumo wake wa mabasi yaendayo haraka.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Uchambuzi wa Wimbo Mpya wa Diamond Platnumz Unaitwa Sikomi.

UCHAMBUZI WA WIMBO
JINA LA WIMBO: SIKOMI
MSANII : DIAMOND PLATNUMZ

UTANGULIZI

Diamond Platnumz ni msanii wa muziki wa kizazi kipya (bongofleva) kutoka Tanzania. Anaiwakilisha nchi yake na fasihi ya kiswahili nje na ndani ya nchi kwa ufanisi. Wimbo wake mpya wa Sikomi ni mojawapo ya nyimbo zake nyingi ambazo amepata kuziimba tangu alipoanza mziki wake. Ufuatao ni uchambuzi wa wimbo wa Sikomi. Angalizo uchambuzi huu utajikita zaidi kwenye vipengele vya maudhui na wala mhakiki hajagusa vipengele vya fani.

DHAMIRA KUU
Dhamira kuu katika wimbo wa Sikomi ni mapenzi. Msanii anaeleza historia yake ya kimahusiano toka alipotoka kimuziki mpaka hapa alipofika. Amegusia visa na mikasa aliyopitia katika mahusiano yake ya kimapenzi. Msanii amepitia katika mengi katika mapenzi lakini bado haachi kujihusisha na mapenzi huu ndiyo msingi wa jina la wimbo "Sikomi". Msanii anasema kila anapoumizwa na mwanamke mmoja anatafuta mwanamke mwingine wa kumfuta machozi.

DHAMIRA NDOGO NDOGO

USALITI KATIKA MAPENZI

Msanii anaeleza jinsi alivyosalitiwa na wanawake aliowapitia msanii anasema " aliyonifanyia wa sentro siwezi Sema... ndiyo maana sikushangaa ile ghafla toka CCM kwenda CHADEMA"
Msanii anaeleza jinsi alivyoumizwa na usaliti katika mapenzi. Msanii anasema mara baada ya kutoka kimuziki alivamia tasnia ya bongo movie ambapo alisalitiwa sana.

Msanii anaeleza jinsi alivyosalitiwa na Penny aliyedai ana ujauzito wake hali iliyompelekea kumhonga gari mpenzi wake huyo ambaye mwisho wa siku alikuja kumsaliti. Msanii anasema ameshafumania na kufumaniwa pia katika mapenzi hii ni kielelezo cha usaliti katika mapenzi kwenye kazi ya msanii.

MIGOGORO
Msanii amesadifu yale yanayotokea katika jamii kwa kuonesha migogoro mbalimbali kwa kutumia wahusika katika wimbo wake baadhi ya migogoro ni hii ifuatayo;

Mgogoro wa msanii na mama yake

Mgogoro wa nafsi wa msanii kuhusu kuachana na mapenzi au kuendelea.

Mgogoro wa msanii na Esma kuhusu kuachana na mapenzi ni baada ya Esma kumwambia msanii mapenzi basi msanii hakutaka kusikia.

Mgogoro wa msanii na Zari. Msanii anasema richa ya Zari kumzalia watoto wawili wa kiume na wa kike lakini bado alimsaliti.

Mgogoro wa Msanii na wa Sentro na mgogoro wa msanii na wa sentro.

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA JAMII

Msanii amemchora mwanamke kama mzazi na mlezi mfano ni mama yake na msanii na Zari.

Msanii amemchora mwanamke kama mshauri mzuri mfano ni mama yake na msanii na Esma.

Mwanamke kama mtu mwenye mapenzi ya dhati mfano Zari aliyempenda msanii mpaka kumzalia watoto wawili, mama yake msanii na Esma.

Msanii amemchora mwanamke kama mtu aliyekosa msimamo na msaliti, mfano wa Sentro na Penny.

KUFANIKIWA KWA MSANII KIMAUDHUI

Msanii ameweza kusawiri ipasavyo mambo yanayotokea katika jamii ya kitanzania na hasa katika ulimwengu wa mapenzi.

UDHAIFU WA MSANII
Msanii amekuja na hitimisho jumuishi kuwa wasanii wa sinema (bongo movie) siyo wa kuaminiwa jambo ambalo siyo la kweli kwenye uhalisia kwani kuna wasanii wengi wa tasnia ya filamu wanajiheshimu na wengine ni watu wazima wenye kujiheshimu pia na kuaminika na jamii. 
Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa