Wednesday, 24 January 2018

Gesi ya Helium ya futi za ujazo bilioni 98.9 yagunduliwa mkoani Rukwa.

Kampuni ya uchunguzi na utafiti wa madini, Helium One, ambayo kwa sasa inafanya utafiti wa gesi ya heliamu mkoa wa Rukwa imegundua kuwapo kwa futi za ujazo bilioni 98.9 za gesi hiyo katika maeneo iliyokwishafanyia uchunguzi.

Hayo yalielezwa katika warsha ya siku moja iliyofanyika Chuo Kikuu cha Dar es salaam, na kuratibiwa na Idara ya Jiolojia ya chuo hicho, Helium One na Chuo Kikuu cha Oxford.

Akizungumza katika warsha hiyo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Helium One, Thomas Abraham-James, alisema kwamba kampuni yao imetafuta leseni 23 za uchunguzi na kwamba nyingine tatu zimeombwa.

Alisema kwamba leseni hizo zote zinamilikiwa na kampuni hiyo kwa asilimia 100 na kwamba ina haki za kipekee za gesi hiyo ya heliamu .

Pamoja na kutoa taarifa hiyo,alisema lengo la kuwa na warsha ni kuwaita wataalamu na wadau mbalimbali wa hapa nchini na kimataifa kubadilishana uzoefu na taarifa zilizopo kuhusu gesi hiyo na kuangalia fursa zinazoambatana na uwapo wa gesi hiyo katika harakati za kitaifa za kuwa na taifa la viwanda.

“Helium One inaamini kwamba kuna fursa kupitia utafiti huu kuweza kutengeneza utaalamu wa kiwango cha juu na utaalamu wa hapa nchini juu ya uendelezaji wa gesi hiyo. Tutaendelea kujenga uhusiano na Chuo Kikuu cha Dar es salaam kuweza kubadilishana elimu, kutoa mafunzo kwa wanafunzi na maofisa wizara ya madini na kutengeneza mpango wa ufadhili wa masomo,” alisema.

Kwa mujibu wa Abraham-James, warsha hiyo ilihudhuriwa na wanasayansi waandamizi wa gesi kutoka Chuo Kikuu cha Oxford cha Uingereza na Idara ya Jiolojia ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam,UDSM, watu wenye mamlaka na maamuzi, wadau wa maendeleo, watengeneza sera kutoka serikalini, watafiti na sekta binafsi.

Aidha kampuni hiyo imetoa ufadhili wa masomo ngazi ya shahada ya uzamili kwa wanafunzi wawili wa UDSM kusoma katika Chuo Kikuu cha Oxford , ikiwa ni sehemu ya kuingiza utaalamu wa hali ya juu wa kisayansi kwa watanzania na pia kuendeleza uhusiano mzuri kati ya Helium One na UDSM.

Wakati wa warsha hiyo, Profesa John Machiwa, akimwakilisha Makamu Mkuu wa Chuo, Prof Cuthbert Kimambo, alisema kwamba jukwaa hilo ni jema kwa wanafunzi, wakufunzi na Chuo kizima kutafuta njia ya kuona namna ya kushirikiana na Helium One.

“Tunaweza kufanyakazi pamoja na kunoa taaluma na pia kupata utaalamu katika utafiti wa heliamu uzalishaji na usafirishaji wake,” alisema.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Msongo wa Mawazo Husababisha Unene?

Sote tunafahamu nini kinatufanya tunenepe: ulaji wa vyakula vyenye kalori kupita kiasi.

Japo jibu hili ni la kweli, halijibu swali la msingi zaidi - je, ni kwanini watu hula chakula kupita kiasi?

Ni kwa nini wakati mwengine najihisi kula keki ama chokleti licha ya kwamba nafahamu nitajutia baada ya dakika chache zijazo?

Kwa mara nyingi huwa ni tamaa - ama ni kitu chengine kinachoendelea?

Licha ya kwamba nidhamu ni muhimu, kuna ushaidi mwingi kwamba msongo wa mawazo huchangia pakubwa kwa mtu kuongeza kilo za mwili.

Msongo wa mawazo kupita kiasi, huathiri jinsi mtu anavyopata usingizi na viwango vya sukari mwilini. Hali hiyo huongeza njaa na kuzidisha zaidi ulaji wa chakula kwa utaratibu.

Na hali hiyo huathiri zaidi usingizi, hata viwango vikubwa vya msongo wa mawazo huathiri zaidi viwango vya sukari. Kwa muda, huo unaweza kusababisha viwango vikubwa vya mafuta na kisukari aina ya type -2.

Na kuona kile kinachoweza kutokea, Dkt Giles Yeo, mwanachama wa Trust Me ,yeye ndiye daktari wa timu ambayo pamoja na usaidizi wa wanasayansi kutoka chuo kikuu cha Leeds, aliamua kujiweka yeye mwenyewe kwenye katika hali ngumu ya msongo wa mawazo.

Wanasayansi wa Leeds walianza kwa kumuuliza Giles kufanya mambo tofauti ambayo yangemsababishia msongo wa kiakili.

Walimuweka mbele ya tarakilishi na wakamlazimisha kufanya hesabu ya kuondoa ,17 , kutoka kwa nambari kama 2,043. Na alipokuwa akikosea, waliona akipatwa na hali ya msongo wa mawazo jambo ambalo lilimpatia Giles shida.

Baada ya hapo wakamlazimu kuweka mikono yake kwenye beseni ya maji baridi kwa muda. Kabla na baada ya uchunguzi huo, kikosi hicho cha chuo kikuu cha Leeds wakampima kiwango cha sukari.

Kiwango cha sukari mwilini huongezeka wakati mtu anapokula, na kwa mwenye afya njema kama Giles, kiwango hicho cha sukari hushuka na kuwa kawaida kwa haraka.

Lakini kikosi hicho cha Leeds kilibaini kwamba siku ambayo Giles alikuwa amepitishwa kwenye shida hizo zote, bado kiwango cha sukari kilichukua muda wa saa tatu kurudi katika hali ya kawaida ambayo ni mara sita zaidi katika siku ambayo mtu ametulia bila wasiwasi wowote.

Sababu kuu ambayo husababisha hayo ni kwamba endapo mtu anapata msongo wa mawazo, mwili hujipata ''ukipigana.''

Mwili hudhani uko katika mashambulizi na hutoa glukosi kwenye damu ili kuongeza nguvu kwenye misuli.

Lakini endapo huhitaji nguvu za kukimbia kujiepusha na hatari yoyote ile, basi wengi hutoa insulini ili kuweza kurudisha kiwango cha sukari kwa kiwango cha kawaida.

Ongezeko la kiwango cha insulini na kushukwa kwa kiwango cha sukari humfanya binadamu kuhisi njaa na ndio sababu kuu kumfanya mtu kutamani kula vyakula vya sukari hasa iwapo mtu anakumbana na msongo wa mawazo.

Kitu kama hicho hutokea iwapo hujapata usingizi mzuri usiku. Utafiti wa hivi karibuni uliofanywa na watafiti wa chuo kikuu cha King, mjini London imebaini kwamba iwapo mtu akikosa usingizi anauwezo wa kula zaidi ya kalori 385 kwa siku , ambayo ni sawa na kalori iliyoko kwenye keki ndogo.

Watoto pia hupata tamaa ya vyakula vya sukari iwapo hawajalala vizuri, kwenye utafiti mwengine,wa hivi karibuni, watafiti walichukua kikundi kidogo cha watoto wenye umri wa miaka mitatu na minne ambao hulala kila siku mchana na kuwalazimu kutolala mchana mmoja na kuhakikisha wamekaa macho saa mbili zaidi wakati wao wa kwenda kulala kila siku.

Usingizi ni muhimu kwa binadamuHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image caption
Usingizi ni muhimu kwa binadamu
Siku ya pili ,watoto hao walibugia asilimia 20 ya kalori kuliko kawaida, hasa vyakula vyenye sukari nyingi na waliruhisiwa kulala kwa muda waliotaka.

Na siku ya tatu, bado watoto hao walikula kalori asilimia 14 kuliko kawaida.

Jinsi za kupunguza msongo wa mawazo kila siku?

Kitu cha kwanza, ningependa watu wanashauriwa kupata usingizi wa kutosha. Hili ni rahisi kwa kusema na si kwa vitendo, lakini mamlaka ya huduma ya afya-NHS inatupatia mbinu muhimu za kufuata.

Pia ungejaribu njia ambazo zinazofahamika zinazopunguza msongo wa mawazo kama vile mazoezi, ukulima ama kushiriki mazoezi ya yoga.

Lakini kitu muhimu tulichobaini kwenye utafiti wetu ni kwamba utafaidika iwapo ulifurahia.

Kwa hivyo jaribu kufanya vitu tofauti na uone kile kinachoweza kukufaa.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Serikali Imevunja Mkataba na Wakala wa Majengo TBA.

SERIKALI imevunja mkataba na Wakala wa Majengo TBA baada ya kutoa taarifa za uongo kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kuhusu ujenzi wa majengo ya Ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Butiama na halmashauri mpya Wilaya ya Butiama mkoani Mara.

Wiki iliyopita kuwa wakala huyo wa majengo alipewa onyo na Waziri wa Elimu, Prof. Joyce Ndalichako baada ya kusuasua kuanza mradi wa Ujenzi wa Madarasa, Ofisi za Chuo Kikuu cha Muhimbili Kampasi ya Mloganzila huku wakiwa wamepewa fedha na Serikali tayari.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Vanessa Mdee Asimulia Alichokerwa kwa Jux.

Malkia wa Bongo Fleva anayefanya vizuri ndani na nje ya nchi, Vanessa Mdee amefunguka na kuweka bayana kwamba alikuwa anakerwa na tabia ya mpenzi wake Jux ya ku-follow wanawake ambao hawaendani nae katika mitandao ya kijamii.

Vanessa ametoa siri hiyo ambayo ilikuwa inamtafuna katika moyo wake kwa kipindi kirefu kupitia kipindi cha 'Planet Bongo ya East Afrika Radio' wakati alipokuwa akifanya mapitio ya albamu yake 'Money Monday', na kusema wimbo wa unfollow ni jambo la kweli ambalo yeye mwenyewe amelipitia katika mahusiano yake na lilikuwa linamkera kupita kiasi.

"Wimbo huu ni stori ya ukweli kabisa ambapo mpenzi wangu alikuwa ananikera na tabia ya ku-follow wasichana wengine katika 'Instagram' ambao nilikuwa siwataki, siwapendi halafu hatuendani nao. Nikawa namuuliza unawa-follow wa kazi gani ? lakini sikuwa napata majibu sahihi", alisema Vanessa.

Pamoja na hayo, Vanessa amedai ameandika wimbo huo kutoka na shida wanazipitia jinsia ya kike (wasichana na wanawake) wanayoipata kwa wapenzi wao pindi wanapotumia mitandao ya kijamii.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Mbowe Atua Mbeya Kusikiliza Kesi ya Sugu.

Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Mhe Freeman Aikael Mbowe, leo amefika Mahakama ya Mkoa wa Mbeya kwa ajili ya kusikiliza kesi inayomkabili Mbunge wa Mbeya mjini, Mhe. Joseph Mbilinyi na Katibu wa CHADEMA Kanda ya Nyasa, Emmanuel Masonga.

Mhe. Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ anakabiliwa na kesi kutoa maneno ya uchochezi.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Idriss Sultan 'Kenya Wanatuzidi Kwa Kutengeneza Satellite yao na Tuzo za Oscar ila Kwa Umbea na Instagram Followers Hawatakaa Watukute'.

Muigizaji wa filamu ambaye siku  zijazo anatarajia kwenda kuigiza katika filamu ya ‘The Blue Maurtius’ Idris Sultan, ametoa neno kwa Watanzania kuhusiana na majirani zetu Kenya kupata nafasi katika tuzo za filamu za Oscar.



Idris ametoa maneno katika mtandao wa Twitter na huku akionyeshwa kukerwa na baadhi ya watu wanaopenda umbea kuliko kazi.


“Kenya imepata Oscar award moja ya Lupita, imekua nominated Oscar award nyingine movie ya WATU WOTE na sasa wamefanikiwa kutengeneza satellite yao ya kwanza. Kwa kifupi watafanya yote ila hawatakaa watukute kwa instagram followers, sisi ndio noma. Satellite ndo nini ? Ina umbea ?,” ameandika Idris.

Washiriki wa tuzo za Oscar mwaka 2018 walitajwa hapo jana huku upande wa Afrika Mashariki imetoa filamu moja iitwayo iiywayo ‘Watu Wote/All of Us’ kutoka Kenya ambayo inazungumzia shambulizi la kigaidi la Al-shabaab lililotokea nchini Kenya mwaka 2014 katika eneo la Mandera ambapo watu 28 waliuawa kwenye tukio hilo.
Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Tabia ya Mwanamke Asiyewajibika Kitandani.

Inasemekana wanawake wengi wenye ndoa wanakuwa na tabia zifuatazo zinazosababisha waume zao kwenda nje ya ndoa na wale wasio na tabia ya nyumba ndogo wanaishia kubakwa na waume zao

*Mwanamke asiyemtamkia kabisa mumewe kuwa anajisikia kuwa naye.
*Mwanamke ambaye baada ya mechi huwa haonyeshi dalili yoyote kama ameridhika na tendo au hakuridhika
*Mwanamke ambaye akiwahi kulala yeye mume akija hataki kuguswa
*Mwanamke ambaye mumewe akimgusa anakubali huku analalamika .. kama ulikuwa unataka kwa nini hukuwahi kulala unangoja nilale ndo unakuja kunisumbua..
*Mwanamke huyo hatingishiki kwenye mechi kata kidogo tena amenuna... anangalia kushoto au kulia anangoja goli liingie ... kama golikipa aliyekata tamaa ya kudaka penati......
*Mwanamke haweki kabisa maandalizi kama zana za kufanyia usafi baada ya mechi kama taulo, kitambaa nk

Ziko nyingine nyingi ambazo ni kero zinazowafanya wanaume kusononeka....na mara nyingine juamua kuzira na kuwa mwanzo wa mmoja kuhama chumba..... Wanawake wenye tabia hizi jirekebisheni

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Sijafulia na Wala Siongwi Elfu 20- Pretty Kind.

Baada ya kufungiwa Miezi 6 kutoa nyimbo mpya, kutumbuiza na kujihusisha na muziki kivyovyote, leo January 24 , 2018 Msanii Pretty Kind amesema sio kweli kwamba amefulia mpaka amekua akihongwa Elfu 20.

Pretty Kind amesema kwanza anataka akirudi aonesha kabadilika sio kwenye kuimba tu hata katika maisha yake ya kawaida huku akikiri kusumbuliwa na wanaume na wengine kuchukulia matatizo yake kutaka kufanya mambo wanayotaka wao.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Tuesday, 23 January 2018

Kenya Yatengeneza Setilaiti Yake ya Kwanza,

Kenya imetengeneza setilaiti yake ya kwanza kabisa ambayo imepangiwa kurushwa anga za juu Machi mwaka huu.

Wahandisi kutoka chuo kikuu cha Nairobi, wakisaidiwa na maafisa kutoka shirika la anga za juu la Japan walitenengeza chombo hicho katika mradi uliogharimu zaidi ya dola milioni moja.

Setlaiti hiyo itatumika kuchunguza mienendo ya kilimo, pamoja na kuchunguza maeneo ya pwani ya taifa hilo.

Mwandishi wa BBC Tomi Oladipo anasema setilaiti hiyo ni ya umbo la mchemraba na ina ukubwa wa sentimita 10 mraba - hujulikana kama nano-setilaiti.

Setlaiti hiyo itatumwa hadi Kituo cha Kimataifa cha Anga za Juu (ISS) mnamo mwezi Machi na kuzinduliwa rasmi kuizungukza dunia na roboti mwezi mmoja baadaye.

Hatua hiyo itaifanya Kenya kuwa miongoni mwa mataifa sita barani Afrika yaliyo na setilaiti zinazoizunguka dunia.

Kundi la wahandisi kutoka chuo kikuu cha Nairobi walioitengeza walikuwa kundi la kwanza kufaidika kutokana na mradi wa pamoja kati ya Umoja wa Mataifa na shirila la anga za juu la Japan unaolenga kuzisaidia taasisi za elimu kutoka mataifa yanayostawi kutengeneza setilaiti zao. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

RPC Aweka Wazi Sababu Kukamatwa Msigwa

Kamanda wa polisi mkoa wa Iringa, (RPC) Julius Mjengi amefunguka na kuweka wazi sababu zilizopelekea kumkamata Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa na kudai kuwa walimkamata wakimtuhumu kuratibu kuchoma na kubomoa nyumba.


Mjengi amesema hayo leo Januari 23, 2018 wakati akiongea na www.eatv.tvna kudai kuwa Mbunge huyo jana alipokamatwa alihojiwa na baadaye aliachiwa kwa dhamana hivyo yupo huru kwa dhamana toka jana majira ya saa tano usiku.

"Jana Msigwa alijisalimisha baada ya kusikia tunamtafuta hivyo tulimuhoji na usiku alipata dhamana, hivyo sisi tulikuwa tunamtafuta kwa tuhuma za kuratibu matukio mawili ya uhalifu hapa Iringa Mjini ambapo kuna nyumba ya diwani mmoja ambaye alijiuzulu na kuhama CHADEMA na kuhamia CCM nyumba yake pagale lilibomolewa"

Kamanda aliendelea kusema kuwa 

"Lakini pia usiku wa kuamia tarehe 17 kuna nyumba moja Kihesa ilichomwa moto ikateketea na ndani mle katika wapangaji mmoja alikuwa ni Katibu wa UVCCM Wilaya ya Iringa Mjini kwa hiyo Msigwa ana tuhuma za kuratibu matukio haya, kwa hiyo tulimuhoji na kudhamini ila tunaendela naye" alisisitiza Kamanda wa polisi mkoa wa Iringa, (RPC) Julius Mjengi  

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Matumizi ya Bangi Yahalalishwa na Gavana Bila Kupiga Kura Marekani.

Kwa mara ya kwanza, jimbo la Marekani limehalalisha bangi kwa kuweka saini na si kwa kupiga kura.

Gavana wa jimbo la Vermont, Phil Scott amesaini muswada wa sheria namba 511 (House Bill 511) ambao unahalalisha kumiliki bangi za uzito usiopungua wakia moja na kuondoa adhabu za makosa ya kumiliki mimea iliyokomaa isiyozidi miwil au miine ambayo haijakomaa.

Hata hivyo, sheria hiyo haizungumzii lolote kuhusu kuanzishwa kwa soko kwa ajili ya mmea huo. Sheria hiyo itaanza kufanya kazi Julai, imeandika yahoo.com ikikariri tovuti ya HuffPost.

“Leo, kwa hisia tofauti, nimesaini H. 511,” alisema Scott katika taarifa aliyoituma kwa Bunge la jimbo hilo.

"Binafsi naamini kwamba ambayo ambayo watu wazima wanafanya ndani na kwenye nyumba zao ni chaguo lao, ili mradi tu hayana athari hasi kwa afya na usalama kwa wengine, hasa watoto.”

Kwa saini hiyo ya Scott, Vermont itaungana na majimbo mengine nane yaliyohalalisha bangi, ikiwa ni pamoja na Washington, D.C., katika wimbi linaloendelea kukua kufanya maamuzi yanayopingana na serikali ya shirikisho.

Serikali ya Marekani bado inaiweka bangi  katika jedwali la kwanza la madawa, ikiwa pamoja na dawa ya kulevya aina ya heroin na LSD.

Vermont ilihalalisha matumizi ya bangi kwa matibabu mwaka 2004, na sasa ni miongoni mwa majimbo 30, pamoja na nchi za Guam na Puerto Rico, na Wilaya ya Columbia, zilizohalalisha bangi kwa ajili ya matibabu.

Ingawa majimbo mengine yamehalalisha bangi kwa kutumia kura ili wananchi waamue, Vermont hairuhusu mchakato kama huo, badala yake wabunge wa jimbo hilo wamekuwa wakishughulikia suala hilo kwa kutaka mabadiliko ya sheria.

Muswada kama huo uliwasilishwa mezani kwa Scott mwaka jana, lakini alikataa kuupitisha, akisema kulikuwa na matatizo katika lugha iliyotumika katika adhabu kwa watakaobainika kuuza bangi kwa watoto na uanzishwa wa kamisheni kwa ajili ya kutafiti jinsi sheria sheria za kusimamia soko la bangi zitakavyofanya kazi katika jimbo hilo. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Ester Bulaya na Halima Mdee Wamaliza Kifungo Chao.

Kifungo walichokuwa wakitumikia wabunge wa Chadema, Ester Bulaya (Bunda Mjini) na Halima Mdee (Kawe) cha kutokuhudhuria shughuli za Bunge kimemalizika na wamesema wamerejea na kasi ileile.

Wabunge hao waliadhibiwa kwa azimio la Bunge Juni 5 mwaka jana kutohudhuria mikutano mitatu ya Bunge ambayo ni jumla ya siku 47, waliyokosa ukiondoa shughuli zote za mikutano ya kamati za Bunge.

Adhabu hiyo ilikwenda sanjari na kulipwa nusu mshahara na posho kwa kipindi chote walichotumikia adhabu hiyo wakituhumiwa kudharau kiti cha spika.

Mikutano mitatu waliyoikosa ni wa bajeti uliokuwa ukiendelea, wa saba uliofanyika kati ya Septemba 5 hadi 15 na mkutano wa tisa wa Novemba 7 hadi 17.

Makato ya mshahara na posho yamebainishwa katika Kanuni 75 ya Bunge inayosema: “Mbunge aliyesimamishwa kazi atatoka katika Bunge na hataingia tena katika sehemu yoyote ya ukumbi wa Bunge na maeneo ya Bunge kwa muda wote atakapokuwa amesimamishwa na atalipwa nusu mshahara na nusu posho zinazoambatana na mshahara huo.”

Jana, kwa nyakati tofauti Bulaya na Mdee walizungumzia kurejea kwao, huku wakisema hawajutii kwa adhabu hiyo na hawatorudi nyuma au kutetereka katika kusimamia wanachokiamini.

“Nitaendelea kuwa Mdee yuleyule wa siku zote, kama walidhani wakinifungia mwaka nitabadilika. Hapana! Sitaraji kubadilika. Nimetumwa na wananchi wangu kusema ukweli na nitausema, sijaja kumpigia magoti mtu,” alisema.

Mdee ambaye pia ni mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha), alisema wakati akitumikia adhabu hiyo amepata fursa ya kufanya shughuli kwa karibu za jimboni kwake na zile za Bawacha.

Naye Bulaya alisema: “Nimerudi bungeni tayari na leo (jana) nilihudhuria kamati yangu ya uwekezaji na mitaji.”

Alipoulizwa amejifunza nini kutokana na adhabu hiyo, alisema: “Bulaya wa kukosoa, Bulaya anayesimamia kile anachokiamini pasi na kuvunja sheria na taratibu hajabadilika, nitaendelea kuwakosoa.”

“Hata nilipokuwa natoka CCM kuja Chadema nilijua mambo kama haya ya kukamatana, kufungiana yatakuwapo kwa hiyo nilijipanga na wala hawanitetereshi, nimerudi na sitarudi nyuma,” aliongeza.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Ajali ya Basi Yaua Wawili na Kujeruhi 8 Jijini Mwanza.

Watu  wawili wamefariki dunia papo hapo na wengine wanane kujeruhiwa vibaya katika ajali ya mabasi mawili yakugongana uso kwa uso katika kijiji cha Kamanga, Sengerema mkoani Mwanza saa nne asubuhi jana.

Akizungumzia ajali hiyo, shuhuda aliyekuwa katika pikipiki na kunusurika kugongwa na mabasi hayo, Philipo Budeba, alisema chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa mabasi yote mawili.

“Mimi nilikuwa naendesha pikipiki, mbele yangu kulikuwa na basi la Mkombozi Trans lenye namba T540 DLF na nyuma kulikuwa na Basi la Walawi Express lenye namba T167 CSN yote yalikuwa na mwendokasi," alisema Budeba.

"Dereva wa Mkombozi ndiye aliyetaka kupita gari lingine, lakini ilishindikana na kusababisha magari hayo kuvaana... mimi nilijirusha kwenye kilima cha pembeni mwa barabara."

Naye abiria wa Mkombozi Trans iliyokuwa ikitokea Kanyara Buchosa, Sengerema, Fransisco Kansola alisema tabia ya madereva kushindwa kuchukua tahadhari na kujali kuwahi abiria ndiyo chanzo cha ajali hiyo.

Walawi Express lilikuwa likitoka Mwanza kwenda Nemba wilayani Biharamulo.

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi alisema dereva wa basi la Walawi, Frank Kimboka ni miongoni mwa majeruhi wanane wa ajali hiyo baada ya kujeruhiwa miguu yote.

“Waliofariki ni dereva wa basi la Mkombozi Trans aliyefahamika kwa jina la Simon Mdalesalamu na mwanamke aliyekadiriwa kuwa na umri wa miaka 18 hadi 20," alisema Kamanda Msangi.

Majeruhi watatu wametajwa kuwa ni Frank Mushi aliyevunjika miguu yote miwili, Isaack Hamisi (22) mkazi wa Nyasaka wilayani Ilemela na Mwinyi Ismail (50) aliyevunjika miguu yote miwili, alisema Kamanda Msangi.

"Chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa mabasi hayo.”

Aidha, ajali hiyo ilitokea wakati mkoa wa Mwanza ukizindua maadhimisho ya wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani, yenye kaulimbiu inayosema ‘Zuia ajali, tii sheria, okoa maisha'.

Majeruhi walikimbizwa katika Hospitali ya Rufani ya Bugando jijini Mwanza kwa ajili ya matibabu.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

TFF Yasubiria Ripoti ya Kamishna wa Michezo Ili Kumuadhibu Nyoso.

Baada ya beki wa Kagera Sugar, Juma Nyoso kudaiwa kumpiga shabiki wa Simba hapo jana, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limesema linasubiri ripoti ya kamishina wa mchezo huo ili kumchukulia hatua za kinidhamu.

Nyoso alishikiliwa jana na polisi kwa kosa la kumpiga shabiki huyo wa Simba aliwahi kufungiwa kwa miaka miwili kwa makosa ya utovu wa nidhamu.

Afisa Habari wa TFF, Clifford Ndimbo alisema ripoti wa kamishina iteleza kama beki huyo alifanya kitendo hicho cha utovu wa nidhamu.

"Kanuni zipo wazi hivyo hiyo ripoti itafikishwa kwa kamati ya saa 72 ambayo na wenyewe watafanya kazi yao na baadaya hapo tamati itakuwa kwa kamati ya nidhamu," alisema Ndimbo. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

WhatsApp Waruhusu Video za Youtube Kucheza Kwenye Programu Yao.

Baada ya muda mrefu WhatsApp kutangaza kuwa itafanya maboresho makubwa matano kwa mwaka huu tayari, Program hiyo imeanza maboresho hayo kwa kuanza kuruhusu video za YouTube kucheza moja kwa moja kwenye Programu wezeshi yao.

Program hiyo ilianza kuruhusu kwanza kwa watumiaji wa iOS mwanzoni mwa mwezi Januari mwaka huu lakini kwa sasa imeruhusu kwa watumiaji wa Android ambapo mtumiaji kama bado hujaona maboresho hayo itakubidi u-update kifaa chako ili uweze kupata huduma hii mpya.

Awali WhatsApp ilikuwa inaruhusu link tu kwenye programu hiyo ambapo mtumiaji alikuwa analazimika kubofya Link na kupelekwa moja kwa moja kwenye App ya YouTube. 


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Jeshi la PolisiYadai Nabii Tito Ana Matatizo ya Akili Apelekwa Kupimwa Milembe.

JESHI la Polisi mkoani Dodoma,  baada ya kumkamata na kumfanyia mahojiano Onesmo Machija (44) anayejiita ‘nabii’ Tito, kutokana na mahubiri ya kidini anayoyafanya, limesema mtu huyo ana  matatizo ya akili.

 Akizungumza na wanahabari mjini Dodoma leo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma, Gillesi Muroto, amesema mnamo Juni 23, 2014, mtu huyo aliwahi kulazwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya matibabu ya akili chini ya daktari aliyejulikana kwa jina moja la William ambapo aliporuhusiwa alitakiwa kurejea hospitalini hapo Julai 9 mwaka huohuo lakini hakurejea.

Kamanda Muroto aliendelea kusema kwamba baada ya hapo, Machija ambaye kanisa lake halijasajiliwa popote,  aliibukia mkoani Dodoma katika kijiji cha Nong’ona kilicho karibu na Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) akifanya  mahubiri ya kidini yaliyodaiwa kuwa hayakuwa na maadili ya kidini.

Kwa msingi huo, alisema jeshi la polisi limempeleka Hospitali ya Rufaa ya Mirembe iliyoko mkoani Dodoma  kwa ajili ya kumpima tena matatizo hayo ya akili na baada ya majibu kutolewa,  Dkt. Dixon Philipo aliyemshughulikia alithibitisha kwamba bado ana matatizo hayo.

Pamoja na hayo, Muroto alisema jeshi la polisi mkoani humo  bado linaendelea kumshikilia kutokana na matendo yake aliyoyafanya ili kufanya uchunguzi zaidi.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

"Bob Junior Anaogopa Kusema Ukweli" - Amber Lulu

Msanii Amber Lulu hapo jana alikanwa kuwahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na msanii Bob Junior, amefunguka na kudai kuwa msanii huyo anaogopa kusema ukweli.


Akizungumza na mwandishi wa www.eatv.tv Amber Lulu amesema tukio hilo lilitokea siku nyingi akiwa mdogo, hivyo huenda Bob Junior anaogopa kukiri kwa kuwa lilikuwa kosa kisheria.

"Sasa kwa nini nimsingizie, labda anaogopa lakini ilikuwa siku nyingi na nilikuwa mdogo, sina sababu ya kumsingizia kweli nilikuwa naye, labda uoga wake, nimsingizie mimi na yeye nani ana kiki!", amesema AMber Lulu.

Hapo jana Bob Junoir alikana kuwahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na msanii AMber Lulu akiwa mwanafunzi wa kidato cha pili, baada ya Amber Lulu kutoa siri hito huku akisema ndiye aliyemleta Dar es salaam. 



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Msimamizi wa Uchaguzi Kinondoni Atupilia Mbali Mapingamizi ya Wagombea Katika Jimbo Hilo.

Msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Kinondoni ambaye pia mkurugenzi wa manispaa hiyo, Aron Kagurumjuli ameyatupilia mbali mapingamizi matatu yaliyowasilishwa na wagombea wa vyama vya Chadema, CCM na CUF.

Mapingamizi hayo ni kwa mgombea wa CUF, Rajab Juma kumwekea mgombea wa Chadema, Salumu Mwalimu, wakati Mwalimu yeye alimwekea Maulid Mtulia wa CCM na mgombea huyo wa chama tawala alimwekea mgombea wa SAU, Johnson Mwangosi.

Baada ya jana ofisi ya msimamizi wa uchaguzi kutoa barua ya utetezi kwa wagombea waliowekewa mapingamizi leo Jumanne imetoa majibu ya kuyatupilia mbali mapingamizi hayo.

Akizungumza na Mwananchi leo, Jumanne Januari 23, 2017, Kagurumjuli amesema “Tumeyatupilia mbali mapingamizi yao kwa sababu hayana mashiko, kilichobaki ni wagombea kwenda uwanjani wakapambane,” amesema msimamizi huyo. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Monday, 22 January 2018

Baada ya Kuvurugana na Heri Muziki Mrembo Diva Atangazia Dunia Kuwa Yupo Single

From Diva - "Im single ....baada ya mwaka sasa niko huru ..sina mahusiano na mtu yoyote n not looking .....life huh?
2018 wuddapppp..
JIMBO HURU..
DIVA WA WATANZANIA
P:s make up on fleek "

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Mchezaji Juma Nyosa Aingia Matatani Tena Baada ya Kumshushia Kipigo Shabiki Mpaka Kuzirai Leo.

KAITABA: Jeshi la Polisi linamshikilia Beki wa Kati wa Klabu ya Kagera Sugar, Juma Nyoso kwa tuhuma za kumpiga shabiki hadi kuzirai

Inadaiwa kuwa Mchezaji huyo alikerwa na maneno(matusi) ya Mashabiki ndipo alichukua uamuzi huo wa kumshambulia mmoja wao

Majeruhi huyo ameondolewa Uwanjani hapo(Kaitaba) kwa gari maalum la kubebea Wagonjwa(Ambulance)

Ikumbukwe kuwa Mchezaji huyo wakati akiichezea Mbeya City aliwahi kuadhibiwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini(TFF) kwa kosa la kumdhalilisha kwa kutumia kidole cha kati Mshambuliaji, John Bocco(aliyekuwa akiichezea Azam FC)

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa