Thursday, 2 March 2017

Tetemeko Kubwa Laikumba Yanga, Timu Kwenda Zambia kwa Treni...!!!!.Fahamu zaidi hapa.

Katika ile hali isiyotarajiwa, team pendwa wenyewe wakiita timu ya wananchi wamekutwa na tetemeko kubwa la kiuchumi kwa kuwa na hali mbaya ya kifedha.
Kutokana na utata huo uongozi wa juu wa timu hyo umeamua kusafirisha timu hyo kwenda nchini Zambia kumenyana na zanaco fc ya nchini humo kwa njia ya treni kupitia reli ya tazara had ktk kampilimposhi,
Mmoja wa kiongozi wa juu alionekana maeneo ya station ya tazara kwa ajili ya shughuli za booking na kuhitaji kujua taratibu za usafiri hyo
Alipoulizwa na mnyetishaji wetu kuwa kwnn wameamua kutumia usafiri huo alijibu kuwa wameamua kutumia usafiri huo kama njia rahis ya kuwawezesha kufika Zambia kwan wakiondoka alhamis ijumaa watakuwa Zambia, akaendelea pia kudai kuwa kocha ndo kashauri hvyo.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Magufuli: Serikali haitatoa chakula cha bure kwa wenye njaa.Fahamu zaidi hapa.

Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameendelea kusisitiza kuwa kuwa Serikali haitatoa chakula cha msaada kwa watakaopatwa na njaa ilihali wanaweza kuzalisha chakula katika maeneo yao.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo katika ziara yake mkoani Pwani, wakati akizungumza na wananchi wa Somanga, Nangurukuru na Mchinga Moja, ikiwa ni ziara yake katika mikoa ya Pwani, Lindi na Mtwara.

Amepokea kero za wananchi katika maeneo hayo nakuwataka  kufanya kazi kwa bidii ikiwemo kuzalisha mazao ya chakula cha kutosha

"Najua mmezoea kusikia maneno mazuri mazuri kuwa hakuna atakayekufa kwa njaa, sasa mimi nasema usipofanya kazi, usipolima mazao na kupata chakula wakati mvua inanyesha Serikali haitatoa chakula cha bure kwa wenye njaa, ni lazima tufanye kazi, sasa hivi mvua zinanyesha limeni mazao ya chakula" amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.

Pia Rais Magufuli amezungumza na wananchi wa Ikwiriri na kupokea kero zao ambapo amewaagiza Mamlaka ya Maji katika Mji huo kuhakikisha mradi wa maji uliojengwa na kukamilika tangu mwaka 2015 kwa gharama ya Shilingi Bilioni 5, unaanza kutoka maji kabla ya mwisho wa Mwezi huu na pia amepiga marufuku utozaji wa ushuru kwa wafanyabiashara wadogowadogo wa mazao.

Aidha, Mhe. Dkt. Magufuli amewaagiza viongozi wa Mkoa wa Lindi kushughulikia migogoro ya wakulima na wafugaji iliyoanza kuibuka mkoani humo na ameahidi kutoa Shilingi Milioni 20 kusaidia ujenzi wa Zahanati ya Somanga.

Mbali na hayo Rais Magufuli amewaagiza Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa kujenga kituo cha mabasi cha Nangurukuru na pia amemuagiza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Lindi kwa kushirikiana na Mbunge wa Jimbo la Mchinga Mhe. Hamidu Bobali kuhakikisha anapeleka Daktari katika kijiji cha Mchinga Moja ili kutatua kero ya wananchi kukosa huduma ya matibabu.

Mhe. Rais Magufuli ataendelea na ziara yake kesho tarehe 03 Machi, 2017 hapa Mkoani Lindi


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Shilole azungumzia la kuvunja ndoa ya Nuh Mziwanda.Fahamu zaidi hapa.

Msanii wa muziki na filamu Shilole amekanusha kurudiana na aliyekuwa mpenzi wake wa zamani Nuh Mziwanda ambaye kwa sasa ameoa mwanamke mwingine aitwae Nawal.


Kupitia mitandao ya kijamii zilizagaa taarifa kwamba wawili hao wamerudia na wako karibu zaidi.


Shilole alidai kwa sasa yeye na Nuh ni washikaji na kuna baadhi ya show wanaandaa pamoja ndio maana kuna wakati wanaonekana wako pamoja.


“Mimi na Nuh sasa hivi ni washikaji, hatuwezi kugombana kama zamani, mimi na Nuh tumesaidiana vitu vingi sana kwa hiyo bado kunaushikaji fulani. Pia sisi ni wasanii, mkituona pamoja mjue kuna kazi zinaendelea, mnajua Nuh ana mke kwahiyo hayo mambo sio ya kweli, kwanza navunjaje ndoa yao?,” alisema Shilole.


Katika hatua nyingine muingaji huyo amewataka mashabiki wa muziki wake kukaa mkao wa kula kwajili ya kazi mpya.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

CCM Yatangaza Mkutano Mkuu Maalum..!!!!.Fahamu zaidi hapa.

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinatarajia kufanya mkutano wake Mkuu maalum wa Taifa Machi 12 mwaka huu lengo likiwa ni kufanya marekebisho ya kanuni na katiba ya chama hicho.
Akizungumza na waandishi wa habari mkoani Dodoma, Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara) Rodrick Mpogolo amesema kuwa pamoja na mambo mengine mkutano huo pia utafanya kazi ya kujadili na kupitisha marekebisho ya katiba ya CCM ya mwaka 1977 toleo la 2012 pamoja na kanuni za chama hicho na jumuiya zake.
Amesema pia mkutano huo utapokea taarifa ya ratiba ya uchaguzi Mkuu wa CCM na jumuiya zake utakaofanyika nchini kote mwaka huu wa 2017.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Rais Magufuli: Marufuku kusafirisha mchanga nje ya nchi.Fahamu zaidi hapa.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amepiga marufuku usafirishaji wa mchanga wa madini nje ya nchi na ametaka mchanga wote ufanyiwe uyeyushaji hapa hapa nchini.

Rais Magufuli ametoa katazo hilo leo wakati akiweka jiwe la msingi la kiwanda cha kutengeneza vigae (Tiles) cha Kampuni ya Goodwill Tanzania Ceramic Limited kilichopo katika Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani.

Akizungumza baada ya kutembelea kiwanda hicho, Mhe. Rais Magufuli ameishukuru Menejimenti ya kiwanda hicho kwa uwekezaji huo na ameelezea kufurahishwa kwake na kutumika kwa teknolojia ya kuyeyusha mchanga wa kutengenezea vigae.

"Nchi hii tumechezewa vya kutosha, sasa nyinyi hapa mnayeyusha mchanga kwa kuuchemsha hadi nyuzi joto 1,000 wakati wengine wanasafirisha mchanga nje ya nchi wakati uchemshaji wake hauhitaji kufika hata nyuzi joto 1,000, naiagiza Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji na Wizara ya Nishati na Madini kuwa kuanzia sasa ni marufuku kusafirisha mchanga nje ya nchi" amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.

Kiwanda hicho kikubwa Afrika Mashariki na Kati ambacho ujenzi wake umegharimu Dola za Marekani Milioni 50 kwa awamu ya kwanza kitakuwa na uwezo wa kuzalisha mita za mraba 80,000 za vigae kwa siku, kitazalisha ajira za moja kwa moja 1,000 na ajira zisizo za moja kwa moja 2,000.

Akizungumza kabla ya kuweka jiwe la msingi la kiwanda hicho Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na uwekezaji Dkt. Adelhelm Meru amesema pamoja na kiwanda hicho, tangu Serikali ya Awamu ya Tano iingie madarakani jumla ya viwanda 2,169 vinavyojumuisha viwanda vidogo, vya kati na vikubwa vimesajiliwa na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) na vipo katika hatua mbalimbali za kukamilika.

Naye Balozi wa China hapa nchini Mhe. Dkt. Lu Youqing amempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa kutilia mkazo juhudi za kukuza uchumi zilizowezesha Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zenye uchumi unaokuwa kwa kasi kubwa Barani Afrika na amebainisha kuwa China itaendelea kushirikiana na Tanzania kuendeleza uwekezaji nchini Tanzania ikiwemo kujenga viwanda.

"Mhe. Rais kwa mujibu wa takwimu za TIC mpaka mwisho wa Juni 2016 uwekezaji wa moja kwa moja kutoka China umefikia Dola za Marekani Bilioni 6.6 na umezalisha ajira za moja kwa moja kwa Watanzania 150,000 na zisizo za moja kwa moja 450,000 na kiwanda hiki cha Goodwill Tanzania Ceramic Limited kimejengwa na wawekezaji kutoka China, vipo viwanda vingine vingi vinajengwa, Mbunge wa Mkuranga ameniambia kuwa kuna viwanda zaidi ya 50 vya Wachina vinavyojengwa hapa Mkuranga, nimefurahi sana kuona karibu kila sekta Watanzania wanafurahia ushirikiano wa Tanzania na China" Amesema Balozi Dkt. Lu Youqing.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

#Breaking News>>>Makonda Afunguka Kuhusu Elimu Yake,Atoa Majibu Haya Kwa Wanaoshinda Mitandaoni Wakimsema..!!!.Fahamu zaidi hapa.

KUHUSU ELIMU YAKE
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amefunguka tuhuma zinazozushwa kupitia mitandao ya kijamii na watu mbalimbali kuhusu elimu yake na zinazoeleza kuwa amefoji cheti cha mtu mwingine.
Akizungumza kwenye kikao cha kamati ya ushauri wa Mkoa (RCC) RC Makonda ameeleza kuwa kinachogombaniwa siyo Makonda bali ni kiti alichokalia (UKUU WA MKOA), hivyo ameeleza kuwa nafasi yake ya ukuu wa Mkoa amepewa na Mungu.
Na kufafanua kuwa hatakama angepata sifuri au daraja la kwanza katika masomo yake, Mungu angetaka awe Mkuu wa Mkoa angekuwa tu, kwani Mungu ndiye anapanga kila kitu na kuongeza kuwa yupo imara kuliko alivyokuwa jana.
KUTISHWA KWA WAZAZI WAKE
Pia RC Makonda amefunguka kuhusu kutishwa kwa baba yake mzazi, pia kuna watu walikwenda eneo analoishi baba yake na mama yake mzazi na kupiga picha, ili wakaoneshe nyumba anayoishi mzazi wake.
KUHUSU KUITWA SHOGA NA MGUMBA
RC Makonda ameeleza kuwa watu wamekuwa wakimtolea lugha chafu kuhusu uzazi wake na kumuita mgumba kwa kuwa hana mtoto na wengine wamekuwa wakimuita shoga, amefunguka na kusema kuwa haoni tusi jipya.
RC Makonda amesema ipo siku watu wataulizwa kuhusu matendo wanayoyafanya duniani kilasiku, hawana budi kuwa makini na matendo yao.
KUHUSU DAWA ZA KULEVYA
RC Makonda ameeleza kuwa tangu aianze vita ya dawa za kulevya yameibuka mengi na kusisitiza kuwa hatoacha ataendelea kwani wapo wanaoshukuru kuanza kwa vita hiyo na kuhoji kwanini haikuanza mapema kwani imeokoa maisha ya wengi, kuhusu maendeleo ya vita hiyo RC Makonda amesema kuwa mashamba ya bangi yanateketezwa kila uchwao, siku mbili zilizopita wamekamatwa watu 100 na kete 400 za dawa hizo pia zimekamatwa.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

CCM yamjibu hivi Mjane wa Kapteni Komba kuhusu mafao ya mumewe.Fahamu zaidi hapa.

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemtaka Mjane wa Marehemu, Kapteni Komba, Bi. Salome Komba kufuatilia malipo ya mafao ya mumewe kwa uongozi wa kundi la Tanzania One Theatre (TOT) ambako ndiko alikokuwa akifanyia kazi.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara), Rodrick Mpogolo, ametoa maelekezo hayo ikiwa ni siku moja tu baada ya Salome kukaririwa  akimuomba Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli aingilie kati kumsaidia ili alipwe mafao ya marehemu mume wake yanayofikia Shilingi Milioni 75.

Mpogolo amesema ofisi yao haiwezi kulizungumzia suala hilo kwa sababu masuala yanayohusu fedha yanapaswa kufafanuliwa vyema na uongozi wa kundi lao la TOT ambako Komba alikuwa akifanya kazi.

“Ofisi yao haiwezi kulizungumzia kwa sababu masuala yanayohusu fedha yanapaswa kufafanuliwa vyema na uongozi wa kundi lao la TOT ambako Komba alikuwa akifanya kazi,” amesema.

Kwa mujibu wa Bi. Salome, hadi sasa wakati mumewe akitimiza miaka miwili tangu afariki dunia, CCM imemlipa Shilingi Milioni 4.5 tu ikiwa ni sehemu ya malipo hayo huku akifuatilia kwa muda mrefu bila mafanikio kupata kiasi kilichobaki cha Shilingi milioni 70.5 bila mafanikio.

Komba aliyezaliwa mwaka 1954, alifariki dunia Februari 28, 2015 na kuzikwa Mkoani Ruvuma ambako enzi za uhai wake alijizolea umaarufu mkubwa kutokana na umahiri wake katika kutunga na kuimba nyimbo mbalimbali za kwaya, hasa za kukipigia debe chama chake (CCM) wakati wa kampeni mbalimbali za uchaguzi.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Ukweli Juu ya Freemason na Illuminant Kuhusika na Kifo cha Michael Jackson(Sehemu ya Pili)..!!!.Fahamu zaidi hapa.

Rais w CBS Records Walter Yetnikoff aliwatishia MTV na kuwaambia “Sitawaletea tena video na ninakwenda hadharani na **** kuwambia watu kwamba hamtaki kuonesha video za watu weusi"
Nafasi ya Walter iliwafanya MTV waanze kurusha vidio ya ‘Billie Jean’ na ‘Beat it’.
Bahati mbaya ni kuwa Thriller ilikuwa ni kama barabara ya kumfanya Michael kuwa kikaragosi cha Illuminati, kuanza kumtumia Michael na kipawa chake kuingiza maono ya kishetani kwa umma. Safari hiyo ilikuwa ni muhimu kufanyika kabla hawajamfanya Michael kuwa ‘White Man’ yaani kabla hawajampatia ugonjwa wa vitiligo ulio badilisha ngozi yake.
Dada yake na Michael, Latoya Jackson alikuwa na haya ya kusema kuhusu kifo cha kaka yake.
"I believe Michael was murdered," she said. "I felt that from the start. Not just one person was involved, rather it was a conspiracy of people. He was surrounded by a bad circle. Michael was a very meek, quiet, loving person. People took advantage of that. People fought to be close to him, people who weren’t always on his side."
"He had needle marks on his neck and on his arms and more about those will emerge in the next few weeks," she said. " I cannot discuss that any further as I may jeopardize the investigation. I can, however, say that I have not changed my mind about my feeling that Michael was murdered."
"I am going to get down to the bottom of this," she said. "I am not going to stop until I find out who is responsible. Why did they keep the family away? It’s not about money. I want justice for Michael. I won’t rest until I find out what and who killed my brother." 
Yaani kwa kiswahili.....
"Namini Michael aliuwawa, nilihisi hilo tokea mwanzo, sio mtu mmoja tu alihusika pasi na shaka ni kikundi cha watu, alizungukwa na kundi baya, Michael alikua mkimya na mpole na mwenye upendo,kwaio walitumia nafas hio vibaya kwake,,watu walipigana kua karibu nae,sio kila mara watu walikua upande wake. Alikua na majeraha ya sindano kwenye shingo na kwenye mikono,japo siwezi kuzungumzia hilo kwa kina nitaharibu upelelezi, lakini siwezi kamwe kubadili msimamo wangu na ninachoamini kwamba Michael walimuua. Sitapumzika hadi nihakikishe nani alihusika, kwanini wameitenga familia, sina shida ya pesa,nataka haki itendeke kwa Michael, sitapumzika.hadi nijue nani alimuua kaka.yangu".
Michael Jackson alifahamu kuwa Illuminati wanataka kumuua. Mwili wake ulipatikana na majeraha kadha ikiwemo shingoni na magotini, pia inaonesha kuwa alidondoka sakafuni kabla ya kifo chake, yaani alikuwa akipambana dhidi ya muuaji kuokoa uhai wake.
Latoya alipoulizwa ni nani aliyemuuwa Michael alijibu ....
“Doctor unaye muona, anaye tajwa kama msababishi wa kifo, ni kinga, yupo nyuma yake watu waliotaka Michael Jackson afe.”
Wakati wa shitaka la mara ya pili la Michael lililomalizika Juni 13 2005, wazazi wa Michael walimuita rafiki yake na Michael Dick Gregory, ambaye alikuwa ni rafiki mzuri wa Michael, walimuomba amtembelee Michael maana hayupo vizuri hata kidogo.
Baada ya siku chache Gregory alirudi na Michael kwenye jumba lake la Neverland. Michael alimkumbatia na kumuambia tafadhali usiniache wanataka kuniuwa.
Gregory akamuuliza Michael lini ilikuwa mara yake ya mwisho kula maana anaonekana kudhoofu, Michael akamjibu, “ wanataka kuniuwa kwa sumu”, akamuuliza ni lini mara ya mwisho amekunywa maji, Michael akamjibu, “Wanataka kuniua”
Gregory akamchukua Michael na kwenda naye kwenye hospitali ya karibu lakini mbali na Neverland bila kumuarifu mtu yeyote kwamba anakuja hapo na Michael Jackson, na akatundikiwa dripi kutoka 11:30 jioni mpaka 11:30 asubuhi na siku iliyofuata kwa masaa 24 akawa kwenye drip bila kupumzika, Dr. Aliyekuwa akimuhudumia akasema lau asingefika kwa wakati basi masaa mengine 12 angelikufa.
Utaona hapo kuwa Juni 2005, illuminati walikuwa wakifanya jaribio la kumuuwa Michael tena, lakini lilishindikana, lakini Juni 2009 walifanikiwa kutekeleza azma yao baada ya kumtumia mtu ambaye Michael alimuamini zaidi, Daktari wake, Conrad Murray. 
Michael alikuwa na nguvu za kutosha, dokumentari kadhaa zimetolewa zikimuonesha wiki kabla ya kifo chake, alionekana yuko safi, na akifanya maandalizi ya ‘tour’ yake ya London aliyoipatia jina la ‘THIS IS IT’, Tetesi ni kuwa kwenye Tour hiyo Michael kati ya mengi aliyo kuwa nayo ilikuwa ni kuufumbua macho ulimwengu kuhusiana na madhila na ubaya wa Illuminati, lakini jamaa nao walishaiona hatari hiyo na hawakuwa na muda wa kupoteza, ndipo daktari ambaye pia ni Freemason alipochukua jukumu hilo zito la kumuangusha King of Pop.
MWISHO....!!!


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Mahakama Kuu Dar yatupilia mbali ombi la Freeman Mbowe.Fahamu zaidi hapa.

Mahakama Kuu ya Tanzania leo March 2, 2017, imetoa uamuzi wa pingamizi la Serikali dhidi ya maombi ya Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, CHADEMA, Freeman Mbowe aliyeiomba Mahakama ilizuie Jeshi la Polisi kumkamata akituhumiwa kujihusisha na dawa za kulevya.

Mbowe alifungua kesi ya kikatiba dhidi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Kamishna  wa Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam, Mkuu wa Upelelezi kanda maalum na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Jopo la majaji wakiongozwa na Jaji Sekieti Kihiyo wameutaka upande wa mleta ombi hilo kufanyia marekebisho ya kifungu kwenye maombi ya Freeman Mbowe kuzuia kukamatwa na Jeshi la Polisi na kumuweka  ndani wakati kesi ya msingi ikiendelea

Baada ya uamuzi huo, kiongoz wa jopo la mawakili wa upande wa Freeman Mbowe, Jeneral Ulimwengu alisema nje ya Mahakama baada ya maamuzi hayo kuwa,

“Ombi limekataliwa kwa sababu hatukuwa na kifungu  ambacho katika sheria zetu kinafanya kazi katika nchi na maelekezo hayo ni kwamba kwa sababu tuna ‘import’ sheria zetu kutoka Uingereza. Tutafute kifungu ambacho kinaweza kusaidia kuendesha mashtaka, hiyo kazi itafanyika kati ya leo au kesho kwa sababu kesi ya msingi bado ipo na itasikilizwa March 8.” alisema Jenerali Ulimwengu.

Naye Mweneyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe baada ya maaamuzi hayo ya Mahakama alisema jopo la mawakili litahamia mjini Arusha kwenye kesi inayomkabili Mbunge wa Arusha mjini (CHADEMA) Godbless Lema.



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

KALA JEREMIAH: JINA HARMORAPA NI KUBWA KULIKO MAJINA YA WASANII WENYE ALBAMU SOKONI.FAHAMU ZAIDI HAPA.

Msanii wa muziki wa Hip pop Kala Jemiah amedai kuwa amefanya tafiti ndogo juu ya muziki wa sasa na mashabiki wake  na kugundua kuwa kiki ni kitu muhimu sana katika muziki wa sasa ili kukuza jina na muziki unaofanya, bila kutafuta kiki au kufanya kitu ambacho mashabiki wako watakuongelea muda wote inapelekea kusahaulika kimuziki.

Kala Jeremiah alizungumza kwa upande wake hawezi kutafuta kiki kwani anaamini ameshazeeka, majukumu ya kifamilia yameongezeka na kuna baadhi ya vitu ambavyo amezungumza kuaachana navyo kwani tayari ana mtoto.

Hali hii ni tofauti na muziki wa zamani, miaka ile msanii alikuwa anajulikana kupitia muziki wake au albamu yake aliyoifanya.

”Muziki wa sasa umebadilika kutokana na mashabiki kutaka vitu fulani ambavyo sio vya kawaida,” amesema Kala Jeremiah.

Katika tafiti ndogo aliyoifanya amegundua jina la rapa, Harmorapa ni kubwa kuliko hata majina ya baadhi ya wasanii wa muziki huo ambao tayari wana albamu mbili sokoni.

”Mimi hivi karibuni nilikuwa na msichana mmoja nikataka kujua nguvu za baadhi ya wasanii wa hip pop, nikawa namuuliza kuhusu wasanii watano ambao wengine wana albamu zaidi ya mbili sokoni alisema hawajui, lakini nilipomuuliza kuhusu kumjua Harmorapa alijibu kuwa huyo namjua sana, tena ana wimbo mmoja,” amesema Kala Jeremiah.

Ameongeza kwa kusema, ”kwaiyo nikagundua huu mziki sasa hivi msanii anatakiwa kuzungumziwa kila mara, sio ukitoa tu ngoma basi, kuna namna ambavyo unaweza kufanya ili uendelee kuwa midomoni kwa mashabiki”.

Ukifanya tafakari ndogo juu ya tafiti na mtazamo wa mwana Hip pop Kala Jeremiah, utagundua kuna ukweli ndani yake siku hizi watu wanatafuta njia ya kutokea kimuziki kwa kutafuta visa ili wajadiliwe mitandaoni na katika vyombo vya habari.

Ni jambo zuri na jema kutengeneza jina mtaani kwanza kisha  kuzama katika mziki maana tayari utakuwa unajulikana kwa kitu fulani ambapo ukiingia kwenye muziki ni rahisi watu kutaka kuujua muziki wako zaidi kama ilivyo kwa Harmorapa, Luludiva na Mimi Mars, ambao ni chipukizi lakini muziki wao unafanya vizuri sokoni.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

MBOWE NA MKEWE WABANWA TENA, TRA YAWABURUZA MAHAKAMANI.FAHAMU ZAIDI HAPA.

Mitihani inazidi kumkabili mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambaye pia ni kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe baada ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kumfungulia kesi yeye na mkewe, Dkt. Lilian Mtei.

Mbowe, mkewe Dkt. Mtui pamoja na Meneja wa Klabu ya Bilicanas, Steven Mlingo wameitwa mahakamani kupitia barua ya wito iliyotolewa na Mahakama ya Wilaya ya Ilala.

Mahakama imefanya uamuzi huo baada ya TRA kueleza kuwa imeshindwa kuwapata ili kuwapa hati ya wito mahakamani huku kesi hiyo iliyofunguliwa mwaka jana ikiwa imeshatajwa mara nne mahakamani hapo.

Washtakiwa hao waliofunguliwa kesi namba 402 ya mwaka 2016, wanakabiliwa na mashtaka matatu ikiwa ni pamoja na kutotumia mashine ya kielektroniki ya EFD kutoa risiti, kinyume cha Sheria ya Usimamizi wa Kodi ya Mwaka 2015, kutoa nyaraka za uongo na kushindwa kutekeleza masharti ya sheria tajwa.

Washtakiwa hao kwa pamoja wanadaiwa kutenda makosa hayo mwezi Mei mwaka jana jijini Dar es Salaam.

Mke wa Mbowe, Dkt. Mtei ni daktari anayefanya kazi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, lakini mwanasheria wa TRA, Marcel Busegano aliieleza mahakama hiyo kuwa walifika hospitalini hapo kumpa barua ya wito bila mafanikio.

Awali, Mbowe aliburuzana mahakamani na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) iliyokuwa ikieleza kuwa inamdai zaidi ya shilingi bilioni 1 ya kodi ya pango iliyokuwepo club ya Billicanas, sakata lililopelekea club hiyo ya usiku kubomolewa.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Download wimbo mpya wa TID Ft. Fid Q unaoitwa "Maisha ya Jela".

Download wimbo wa TID Ft. Fid Q - Maisha ya Jela.



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Download wimbo mpya wa Harmo Rapo ft Juma Nature unaoitwa "Kiboko ya Mabishoo".

Download wimbo wa Harmo Rapo ft Juma Nature - Kiboko ya Mabishoo.



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Download wimbo mpya wa Mwasiti unaoitwa "Kaa Nao".

Download wimbo wa Mwasiti - Kaa Nao.




Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

DAKTARI ALIYEMTIBU NGOMA ASEMA ALIDANGANYA, ATAKA AWAAMBIE UKWELI WANA YANGA.FAHAMU ZAIDI HAPA.

Na Dr Haroun Haroun

Yanga  ina  daktari wa  timu  anaitwa  Dr Edward bavu nafikiria  ana  taaluma  ya  kutibia  wachezaj  vizuri, lakini  wakati  mwingine kwa sisi madaktari ikitokea ukishindwa kumtibu mgonjwa unaweza kuomba  daktari  mwenzio akusaidie.

Nilipigiwa  simu  na  Mjumbe  mmoja  wa  yanga ili  nimsaidie  kumtibu Donald Ngoma baada ya kutoka Zanzibar , Nilifanya  hivyo  nafikiria  hii inatokana  na weledi wangu mzuri  wa  uelewa  katika  taaluma  ya  matibabu  ya  michezo, nilimpokea nikamfanyia vipimo pamoja na matibabu (angalia picha na maelezo ya tiba hapo chini).

Nimewasaidia  wachezaji  wa  yanga  waliokuwa  na  shida  mbalimbali za kimatibabu hasa  yale  yaliyokuwa  sugu  katika  michezo (Hissan) wewe ni shahidi, nina  reference  ya Mwashiuya, Juma  Abdul  na Canavaro pamoja na  wachezaj  wengine  mbalimbali  sijawahi  lalamikiwa  hata  siku  moja.

Nilimtibu  Kwa  muda  wa  wiki  mbili  kwa  jeraha la goti  na  kupona  kabisa ,nakumbuka  tarehe  3 Februari,  Yanga  walicheza dhidi ya Stand United  nikiwa nyumbani naangalia mchezo huo ambao Ngoma aliumia na kushindwa kuendelea na mchezo, baadaye nikamwandikia sms kwa  Whatsap  kujiridhisha  kama  bado  jereha  linamsumbua,? akasema, hapana  anachoumwa  Sasa  ni  groin  ikiwa  na maana  kiuno  au  wengine  hupenda  kusema  nyonga na alinijibu Kwa  whatsap  SMS (screen shot nimekutumia), nikamuahidi  kumsaidia  tena  kwa  tatizo  hilo,baada ya matibabu akasema  anajisikia  amepona  na  hata  majibu  ya  vipimo  hayakuonyesha tatizo (picha za vipimo na matibabu hizo nimetuma). 

Kitaalamu  Kuna  aina  nne  ya  matibabu  katika  mpira, kuna  sports medicine doctor, physiotherapy, sport nutrition advisor na  chiropractor  ambayo  tunaita  matibabu  mkandamizo  utaalam  huu  nchi  yetu  Hakuna, Ngoma  aliwaongopea  viongozi  wa  Yanga SC  kwa  kuja  na  report  ya  kutengenezwa  kutoka  London  Health  ambayo  imeandikwa  na  physiotherapy  na  siyo  daktari  wa  Michezo.

Fomu  ya  FIFA  ina  sehemu ya daktari  wa  timu na  daktari wa viungo, daktari  wa  viungo  hawez  kuandika  report  Ya  Mchezaji  itakuwa  mara  ya  kwanza  Tanzania.

Ukitazama  report  ya  London  Health  haiko  kwenye maandishi  ya  kidaktari  kabisa inaonekana ilikuwa  mahitaji  ya  Mgonjwa, report  ya  Medical  ina  sehemu  tatu, historia  ya  mgonjwa  ,vipimo  na  ugonjwa  ulioonekana  na  matibabu  yaliyofanyika ambapo daktari  wa  mazoezi  atachukua  report  kutoka  Kwa  daktari.

Niliwaambia ukweli viongozi wa Yanga SC na wewe ukiwemo uliponiuliza (Februari 18) juu ya tatizo lake, nikawajibu kuwa amepona na hana tatizo lolote kiafya hicho ndicho kilichomkasirisha Ngoma na kuamua kunichafua, ukweli ndio umenifanya mimi kuchafuliwa.

Sio kitu  kizuri  kuonyesha  report  ya  Mgonjwa  lakini  hamna  namna, nataka uma wa wana Yanga na wapenzi wa mpira waujue ukweli kuhusu Ngoma, Yanga SC wamekuwa wanaleta  wagonjwa  kwangu  wakati  wana  daktari  wa  timu hii  inaonyesha  ubora  wangu  wa  kazi na imani waliyonayo kwangu, sio jambo jema kwangu kulikalia kimya jambo ambalo linahatarisha mustakabali wa taaluma yangu.


Niwaombe radhi wote niliowakwaza kwa namna moja ama nyingine, nawaomba mliokuwa na imani muendelee kuniamini na sitowaangusha, imani yenu kwangu isipotee kwa jambo hili.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

MADRID NUSURA "WAKANYAGE MIWAYA", YANUSURIKA MWISHONI NA KUPATA SARE YA 3-3 NA LA PALMAS.FAHAMU ZAIDI HAPA.

REAL MADRID (4-3-3): Keylor Navas; Carvajal, Ramos, Nacho, Marcelo; Kroos, Kovacic (James 71), Isco (Lucas 65); Bale, Morata (Benzema71), Ronaldo
Unused subs: Casilla, Pepe, Modric, Asensio
Goals: Isco 8, Ronaldo 86 pen, 89
Sent off: Bale
Booked: Bale, Ronaldo, Morata, Ramos
 LAS PALMAS (4-1-4-1): Varas, David Simón, Lemos, Bigas (Aythami 27), Dani, Roque Mesa, Vicente, Jonathan Viera (Halilovic 75), Tana, Jese, KP Boateng (Mateo 69)
Unused subs: Lizoain, Garcia, Momo, Hernan
Goals: Dominguez 10, Viera 56 pen, Boateng 59
Booked: Boateng, Simon, Halilovic
Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Wednesday, 1 March 2017

Nishawahi kutoa mimba ila sikumbuki ni ngapi! – Aunt Ezekiel.Fahamu zaidi hapa.

Msanii wa filamu Aunt Ezekiel amefunguka kwa kudai kuwa ameshawahi kutoa mimba kadhaa lakini hajui ni ngapi.
Muigizaji huyo ambaye ni mama wa mtoto mmoja aitwae Cookie, akijibu swali la shabiki wake kupitia Kikaango cha EATV aliyetaka kujua idadi ya mimba ambazo amewahi kutoa, Aunty alisema hawezi kusema uongo kuwa hajawahi kutoa mimba, lakini kitu ambacho hakumbuki ni idadi ya mimba alizowahi kutoa.

“Kutoa nishawahi, nikisema sijawahi nitakuwa muongo, ila kukumbuka ni mimba ngapi ndiyo tatizo,”alisema staa huyo wa filamu.

Muigizaji huyo ambaye kwa sasa yupo kwenye mahusiano na dansa wa Diamond Platnumz, Mose Iyobo, amesema kwa sasa anatamani zaidi kupata mtoto wa kiume atakamuita jina la Greyson ambalo ni jina la babu yake.



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Imefichuka... Unene Kupita Kiasi Chanzo cha Ugonjwa wa Kansa..!!!.Fahamu zaidi hapa.

WANASAYANSI wa Uingereza wanasema wamethibitisha kuwepo kwa uhusiano mkubwa kati ya kunenepa na aina 11 za saratani.
Watafiti wamebaini unene unasababisha saratani kadhaa ikiwemo saratani ya tumbo, ini, matiti, utumbo na mfuko wa kizazi.
Watafiti hao kutoka Chuo Kikuu cha Imperial jijini London, wanasema, mbali ya kuepuka uvutaji sigara, kutunza uzani unaozingatia afya bora, ni njia muhimu inayopunguza uwezekano wa kuugua saratani.
Shirika la afya duniani linasema asilimia 40 ya watu wazima kote duniani ni wanene

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Polisi Watinga Nyumbani kwa Gwajima....Mwenyewe Agoma Kufungua Mlango.Fahamu zaidi hapa.

Jeshi  la Polisi kwa mara nyingine jana lilizingira nyumba ya Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, kwa kile lilichodai kuwa lilifika kufanya uangalizi.

Taarifa ambazo zimethibitishwa na Askofu Gwajima mwenyewe, zinaeleza kuwa polisi walifika nyumbani kwake wakiwa katika gari lao.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, polisi hao walipojaribu kutaka kuingia nyumbani kwa askofu huyo, walizuiwa mlangoni kwa sababu hawakuwa na kibali chochote wala maelezo yanayojitosheleza ya kutaka kukutana na kiongozi huyo wa kiroho.

Askofu Gwajima  jana alikiri polisi hao kumfuata nyumbani kwake na hivyo kulazimika kumtafuta wakili wake mara moja.

“Ni kweli walikuja wakiwa na gari la polisi, lakini walipofika nami nilimpigia mwanasheria wangu ambaye aliniambia tuwaulize wametumwa na nani na kama wana ‘search warrant’ (kibali cha kufanya upekuzi) au ‘arrest warrant’ (kibali cha kukamata),” alisema.

Askofu Gwajima alisema walipowauliza, walimtaja Afande Kingai kama ndiye mtu aliyewatuma, lakini hawakuwa na kibali chochote.

Kwa mujibu wa Askofu Gwajima, mwanasheria wake alifanya mawasiliano ya simu na Afande Kingai ambaye amepewa jukumu la kuwafuatilia wale wote waliotuhumiwa katika sakata la dawa za kulevya na kumuuliza sababu za kumfuata nyumbani.

“Afande Kingai amemweleza mwanasheria wangu kuwa walikuwa wamekuja kwa ajili ya ‘observation’ (uangalizi) tu, kwa hiyo mwanasheria wangu akasema kama ni ‘observation’ tu tusiwaruhusu kuingia ndani kwa sababu sheria ya hivyo hakuna, na sisi tumewazuia hawakuingia ndani,” alisema Askofu Gwajima.

Alipoulizwa kama kufuatwa kwake sasa na polisi kuna uhusiano wowote na kauli alizozitoa kanisani kwake hivi karibuni kuhusu elimu ya Paul Makonda ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Askofu Gwajima alisema huenda ikawa hivyo, lakini akasisitiza kuwa hana uhakika kwa sababu hajazungumza na askari waliomfuata.

Na alipoulizwa kama anadhani ujio huo pia unatokana na andiko ambalo linasambaa kwenye mitandao ya kijamii ambalo linasema Jumapili ijayo mwalimu aliyemfundisha mtu mmoja anayetajwa kwa jina la Bashite atakuwapo kanisani kutoa ushuhuda, Askofu Gwajima alikana akisema andiko hilo si lake.

Pamoja na hayo, Askofu Gwajima alikwenda mbali na kuhoji: “Hata kama ni kweli, sasa unaogopa mwalimu kuja… kanisani kwangu wapo watu wengi waliosoma naye Bashite kuanzia shule ya msingi na Sekondari ya Pamba… vyeti kama huna huna tu.”

Alipoulizwa haoni kauli yake kwamba Rais Magufuli ni tofauti kabisa na Makonda ilikuwa na nia ya kuwatenganisha viongozi hao, Askofu Gwajima alisema aliyemtaja kwa kumshambulia ni Makonda na si Rais.

“Aliyenitaja kwa kunishambulia katika sakata la dawa za kulevya ni Makonda na si Rais, mimi nimemuongelea Makonda, mimi ni mtumishi wa Mungu siwezi kuongozwa kwa ‘speculation’, si unajua hata Yesu alisema kama wewe huna dhambi basi uwe wa kwanza kushika jiwe,” alisema Askofu Gwajima.

Alipoelezwa kuwa katika mahubiri yake ni kama anaonekana kumshtaki Makonda, askofu huyo alisema: “Nilisema nitamshtaki kwa mahakama iliyo juu yake na nilisema Makonda aombe radhi, angekuwa mstaarabu baada ya sakata lile yeye mwenyewe angenipigia simu na kuniambia Gwajima nilikengeuka, lakini hajafanya hivyo.”
 
Pamoja na hayo, Askofu Gwajima alisema kwa aliyoyafanya Makonda tayari amekwishamsamehe na ndiyo maana hajampeleka mahakamani.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Rais Magufuli Amteua Mama Salma Kikwete Kuwa Mbunge wa Viti Maalum.Fahamu zaidi hapa.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 01 Machi, 2017 amemteua Mhe. Salma Kikwete kuwa Mbunge wa Viti Maalum wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mhe. Salma Kikwete ni Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete.

Mhe. Salma Kikwete ataapishwa kwa mujibu wa sheria na taratibu zitakazotangazwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

Waziri Nape: Nitajiuzulu Uwaziri Kama Itabainika Natoka Kimapenzi na Wema Sepetu.Fahamu zaidi hapa.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, amesema atajiuzulu uwaziri endapo mtu atampelekea ushahidi wa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na msanii yeyote.

Kauli hiyo ya Nape inakuja ikiwa ni takriban wiki tatu tangu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, aseme watu wanaotetea wale aliowataja hadharani kwa kuhusika na dawa za kulevya wengine ni wapenzi wao.

“Wengine wanaumia tunagusa wapenzi wao, wawasaidie waache si kupiga kelele tu, ujumbe umefika,” alisema Makonda katika moja ya mikutano yake.

Ingawa katika mkutano huo Makonda hakumtaja mtu kwa jina, lakini aliitoa kauli hiyo siku chache baada ya Nape kupinga mfumo wake wa kutaja majina ya watu hadharani, hususani wasanii na kuwatuhumu kuhusika na dawa za kulevya.

Nape alisema kuwataja watu bila ushahidi ni kuwachafulia majina yao waliyoyatengeza kwa muda mrefu.

Mbali na Nape, Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Msukuma (CCM), alizungumza mara kadhaa bungeni akimpinga Makonda kwa mfumo wake aliokuwa akitumia, kutaja majina ya watu wanaojihusisha na dawa za kulevya.

Akizungumza katika kipindi cha Dakika 45 kinachorushwa na kituo cha luninga cha ITV juzi, Nape alieleza kushangazwa na kitendo cha kuhusishwa kuwa na mahusiano na wasanii.

“Ila kama mtu ana ushahidi alete hapa mezani aseme Nape hili unalofanya, unafanya kwa sababu una uhusiano, na mtu akileta najiuzulu uwaziri.

“Hii ni katika watu ambao wanakosa hoja halafu wanasingizia hoja ambazo hazina msingi, ningefurahi mtu akisema Nape hana sababu ya kutumia busara, twende na hoja hii nyingine ni upuuzi,” alisema Nape.

Akizungumzia kuhusu kutajwa kuhusishwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na msanii nyota wa filamu, Wema Sepetu, Nape alisema wasanii wengi ni wadogo zake akiwamo Wema.

“‘Majority’ ya wasanii hawa ni wadogo zangu. Wamezungumza habari ya Wema, sasa nieleze ukweli kwamba baba yake, mzee Sepetu (Isack) na baba yangu (Moses Nnauye) ni mtu na kaka yake, kwa hiyo Wema ni mdogo wangu sana sana.

“Mama yake anatoka Singida, mama yangu naye anatoka Singida, ni mtoto mdogo lakini mtu akiamua apoteze ‘direction’ (mwelekeo) ya mjadala anaweza kuja na hoja nyingi sana.

“Mimi nimeanza kufanya kazi na wasanii, nimefanya nao kazi kwa miaka 16, hii ya uwaziri imekuja juzi tu. Pia msisahau hawa wasanii tuliwatumia kwenye kampemi ya CCM, mimi ndiyo nilikuwa Katibu wa Uenezi wa CCM.

“Ukizungumza burudani, hamasa na ‘publicity’ mimi ndio nashughulika nayo, hivyo kuwaingiza wasanii kwenye kampeni haikuwa kazi rahisi, sasa nikiwa nao karibu dhambi inatoka wapi, maana ndio nilipewa dhamana ya kuwasaidia. Hizi hoja zingine ni za kijinga kabisa,” alisema Nape.

Pamoja na mambo mengine, Nape alisema utaratibu uliokuwa ukitumiwa na Makonda kwa kutaja majina ya watu hadharani una madhara makubwa kwani unajenga chuki katika jamii.

Nape ambaye pia ni mbunge wa Mtama mkoani Lindi, alisema hakuna mahali popote duniani vita ya dawa za kulevya ilishinda kwa kupiganwa hadharani.

 “Tutajenga chuki kubwa sana kwenye jamii kama tukianzisha utaratibu wa kila mtu anasimama anamtaja mtu hadharani, ukishamtaja anaandikwa kwenye mitandao.

“Nchi itaingia kwenye vurugu kubwa bila sababu na wale wenye chuki zao watapitia hapo kuanza kutajana majina, tukitajana majina hadharani, hii vita hakuna mahali walipigana hadharani wakashinda popote duniani, haipo,” alisema.

Aidha alisema watu wasihukumiwe bila kosa bali haki itendeke na sheria na taratibu zifuatwe.

“Namshukuru Rais (Dk. Magufuli) ametumia busara namna ya kuli-handle (kulishughulikia) hili suala, amemteua kamishna na amemkumbusha waziri mkuu kwamba yeye ndie mwenyekiti wa hii kamati na mawaziri wako ndio wajumbe, sasa ameweka vita hii katika chombo salama.

“Pia namshukuru kamishna mwenyewe kasema tusitaje majina hadharani, lakini tufuate sheria na akasema hakuna jiwe litabaki juu ya jiwe, tutahakikisha tunasimamia sheria,” alisema Nape.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

#BREAKING NEWS>>WATU WANAO DHANIWA NI POLISI WAVAMIA NYUMBA YA GWAJIMA.FAHAMU ZAIDI HAPA.

 Watu wanaodhaniwa kuwa ni polisi wamezingira Nyumba ya Askofu Mkuu wa Makanisa ya Ufufuo na Uzima Josephat Gwajima huko Salasala muda huu.
Bado haijafahamika wanatafuta nini.
Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

NGOMA AANDIKA HAYA MADUDU YA VIONGOZI WA YANGA,AMTAJA KIONGOZI ALIYE SABABISHA YOTE HAYA.FAHAMU ZAIDI HAPA.




Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa