Thursday, 2 June 2016
#BURUDANI>>> Huu ndo utambulishwa wa Rich Mavoko WCB hii leo.Fahamu zaidi hapa.
Rich Mavoko akitia saini kuingia WCB.
A video posted by TANGAZA BIASHARA ZAKO HAPA. (@hebronmalele.blogspot) on
#YALIYOJIRI>>>>Wabunge 7 wa Upinzani Waliosimamishwa Kuhudhuria Vikao vya Bunge Waongezewa Adhabu.Fahamu zaidi hapa.
Wabunge
saba wa upinzani waliosimamishwa bungeni, watakumbana na kibano kingine
cha kukatwa mshahara na posho kwa kipindi chote cha kutumikia adhabu.
Wabunge
hao ambao Jumatatu walisimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge kwa muda
tofauti kwa madai ya kukiuka kanuni ni Zitto Kabwe (Kigoma Mjini), Tundu
Lissu (Singida Mashariki), Halima Mdee (Kawe), Ester Bulaya (Bunda
Mjini), John Heche (Tarime Vijijini) na Godbless Lema (Arusha Mjini).
Adhabu
hiyo ilitolewa kama azimio la Bunge baada ya Kamati ya Haki, Maadili
na Madaraka ya Bunge kupendekeza wabunge hao waadhibiwe kutokana na
kuomba mwongozo wa kiti cha Spika kwa jambo ambalo tayari lilishatolewa
uamuzi.
Habari
zilizopatikana bungeni zilieleza kuwa wabunge hao watakumbana na Kanuni
ya Bunge ya 75, ambayo inahusika na masharti ya mbunge aliyesimamishwa
kazi.
Naibu
Katibu wa Bunge (Shughuli za Bunge), John Joel alithibitisha kuwa
utekelezwaji wa kanuni hiyo utafuatwa kwa wabunge wote ambao
wamefukuzwa.
Akizungumzia
hatua hiyo, Heche alisema hadi sasa hajapata barua ya kusimamishwa
Bunge, hivyo hata kama watakata posho au mshahara haimsumbui kwa kuwa
hawezi kusikitikia kitu hicho wakati haki inaminywa.
Zitto
alisema hajasikia taarifa hizo za kukatwa mshahara kwa kuwa hajapewa
barua inayoeleza mambo hayo wala ya kusimamishwa Bunge.
Nuh Mziwanda atoboa Siri ya ‘Jike Shupa’.Fahamu zaidi hapa.
Nuh Mziwanda amefunguka kile kilichojificha kwenye wimbo wake wa ‘Jike
shupa’ ambao kwa sasa unafanya poa, aliomshirikisha Alikiba, na jinsi
alivyoupokea kwa mara ya kwanza.
Akiongea kwenye kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio, Nuh
Mziwanda amesema Alikiba alimtaka Nuhu autoe wimbo huo bila yeye kutia
sauti yake, kwani aliuona umekamilika na mzuri pia.
“Kiukweli nilikuwa nishaurekodi ushaisha, na nilikuwa nina plan ya kuuachia mimi mwenyewe, baadae nikaona mbona nimekaa kimya muda mrefu alafu nahitaji kuja kitofauti, ndio nikamfuata Alikiba nikamsikilizisha, nashukuru Mungu mwenyewe aliupenda kwa muda mfupi, akaniambia Nuh mbona wimbo umekamilika? uachie tu hivi hivi, nikamwambia hapana nahitaji sauti yako, ndio maana Kiba kaimba kidogo sana lakini kafanya kitu kikubwa”, alisema Nuhu Mziwanda.
Pia Nuhu Mziwanda amesema anaamini wimbo huo utakuja kubadilisha status yake na kuwa kubwa zaidi kuliko alipo sasa , kwenye kazi zake za muziki.
eatv.tv
“Kiukweli nilikuwa nishaurekodi ushaisha, na nilikuwa nina plan ya kuuachia mimi mwenyewe, baadae nikaona mbona nimekaa kimya muda mrefu alafu nahitaji kuja kitofauti, ndio nikamfuata Alikiba nikamsikilizisha, nashukuru Mungu mwenyewe aliupenda kwa muda mfupi, akaniambia Nuh mbona wimbo umekamilika? uachie tu hivi hivi, nikamwambia hapana nahitaji sauti yako, ndio maana Kiba kaimba kidogo sana lakini kafanya kitu kikubwa”, alisema Nuhu Mziwanda.
Pia Nuhu Mziwanda amesema anaamini wimbo huo utakuja kubadilisha status yake na kuwa kubwa zaidi kuliko alipo sasa , kwenye kazi zake za muziki.
eatv.tv
Snura Amkabidhi Jipu Mama Samia.Fahamu zaidi hapa.
STAA wa muziki Bongo, Snura Mushi ameibuka na kumkabidhi Makamu wa
Rais, Samia Suluhu jipu la wanaume wanaowakataa watoto wao na kuwaachia
wanawake mzigo wa kulea peke yao.
Akizungumza na Risasi Mchanganyiko, Snura alisema
siku hizi wimbi la wanaume kuwakataa watoto wao ni kubwa sana hivyo
tatizo hilo ni sawa na majipu mengine, anamuomba mama Samia alitumbue.
“Namuomba mama Samia kwa sababu ni mwanamke mwenzetu atusaidie kulitumbua hili jipu maana ni kubwa sana yaani tena ni tambazi kabisa, kama rais anavyowatumbua watu naye atumbue hili maana wanawake tumechoka.
“Nina watoto wawili lakini baba zao wamenisusia, wa kwanza alimkataa tangu nikiwa na mimba ya wiki mbili mpaka sasa nalea mwenyewe, huyu mwingine hajawahi kutoa chochote tangu mwanaye huyu azaliwe kitu ambacho kinaumiza sana,” alisema Snura.
Aliendelea kusema kuwa baada ya mama Samia kutumbua hilo jipu anaomba serikali iweke sheria ya kwamba kila kituo cha polisi kiwe kinapokea malalamiko ya wanawake wanaosusiwa watoto au mimba ili shtaka linapokwenda waandikishane na baada ya mtoto kuzaliwa ikigundulika mtoto ni wa mwanaume husika alipishwe fidia.
“Pia kipimo cha DNA kiwepo katika hospitali mbalimbali ili iwe rahisi kupima kwa wale wanaume wanaokataa kwamba watoto siyo wao, sheria hizi zikiwekwa zitasaidia kutokomeza tatizo hilo la watoto kukataliwa na baba zao,” alisema Snura.
Jitihada za kuzungumza na Waziri wa Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu kujua ameipokeaje changamoto hiyo, hazikuzaa matunda kufuatia simu yake kutopatikana hewani.
Snura ni mama wa watoto wawili kila mmoja na baba yake ambapo anawalea mwenyewe huku akikiri kwamba huwa anawaeleza wanaye hao jinsi baba zao walivyowakataa ili baadaye kusije kutokea mvutano wa kimasilahi pindi watakapofanikiwa.
Chanzo:GPL
Snura Mushi
“Namuomba mama Samia kwa sababu ni mwanamke mwenzetu atusaidie kulitumbua hili jipu maana ni kubwa sana yaani tena ni tambazi kabisa, kama rais anavyowatumbua watu naye atumbue hili maana wanawake tumechoka.
“Nina watoto wawili lakini baba zao wamenisusia, wa kwanza alimkataa tangu nikiwa na mimba ya wiki mbili mpaka sasa nalea mwenyewe, huyu mwingine hajawahi kutoa chochote tangu mwanaye huyu azaliwe kitu ambacho kinaumiza sana,” alisema Snura.
Aliendelea kusema kuwa baada ya mama Samia kutumbua hilo jipu anaomba serikali iweke sheria ya kwamba kila kituo cha polisi kiwe kinapokea malalamiko ya wanawake wanaosusiwa watoto au mimba ili shtaka linapokwenda waandikishane na baada ya mtoto kuzaliwa ikigundulika mtoto ni wa mwanaume husika alipishwe fidia.
“Pia kipimo cha DNA kiwepo katika hospitali mbalimbali ili iwe rahisi kupima kwa wale wanaume wanaokataa kwamba watoto siyo wao, sheria hizi zikiwekwa zitasaidia kutokomeza tatizo hilo la watoto kukataliwa na baba zao,” alisema Snura.
Jitihada za kuzungumza na Waziri wa Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu kujua ameipokeaje changamoto hiyo, hazikuzaa matunda kufuatia simu yake kutopatikana hewani.
Snura ni mama wa watoto wawili kila mmoja na baba yake ambapo anawalea mwenyewe huku akikiri kwamba huwa anawaeleza wanaye hao jinsi baba zao walivyowakataa ili baadaye kusije kutokea mvutano wa kimasilahi pindi watakapofanikiwa.
Chanzo:GPL
#YALIYOJIRI>>>Update: Wabunge Wote Wa Upinzani Watoka Nje Asubuhi Hii Kupinga Naibu Spika Kuendesha Vikao vya Bunge.Fahamu zaidi hapa.
Wabunge
wote wa vyama vya upinzani leo tena wametoka nje kupinga Naibu Spika
wa Bunge Dk. Tulia Ackson kuendesha vikao vya Bunge na kumwachia Bunge
yeye na wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Taarifa
kutoka Bungeni zinaeleza kuwa, wabunge wote wa upinzani wametoka nje
kususia kikao cha Bunge ikiwa ni kutekeleza azimio lao la kutokuwa na
imani na Dk Tulia.
Baada
tu ya kusomwa dua ya kufungua Bunge, wabunge hao wametoka nje majira
ya saa 3:00 asubuhi na kumwacha Dk. Tulia akiwa na wabunge wa CCM pekee.
Kambi upinzani ilianza utaratibu huo juzi kwa kutoka ndani ya ukumbi wa Bunge baada ya Dk. Ackson kuingia ukumbini.
Kiongozi
wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, juzi alisema
wataendelea kutoshiriki vikao vinavyoongozwa na Naibu Spika hadi pale
"haki itakapopatikana."
#YALIYOJIRI>>>>JWTZ Yajitosa Mauaji Ya Watu 8 Tanga.Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange Atangaza Msako usiku na Mchana.Fahamu zaidi hapa.
Uamuzi huo umechukuliwa baada ya watu wanane kuuawa kinyama kwa kuchinjwa juzi usiku katika Kitongoji cha Kibatini, Kata ya Mzizima, Manispaa ya Tanga.
Habari
za uhakika ambazo tulizipata jana, zinasema tayari vikosi hivyo
vimeanza operesheni kali katika mapango ya Amboni ambayo yanadaiwa kuwa
maficho ya watu hao.
Akitoa
salamu za rambirambi wakati wa mazishi ya marehemu wanne kati ya wanane
waliozikwa Kibatini jana, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama,
Jenerali Davis Mwamunyange, alisema vyombo vya dola vitahakikisha watu
wote waliohusika katika mauaji hayo wanatiwa mbaroni.
“Ndugu
zangu nawapeni pole kutokana na kuondokewa na wapendwa wetu… naomba
kuwahakikisha sisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya dola
tutahakikisha tunawatia nguvuni watu wote waliohusika na mauaji haya,” alisema Jenerali Mwamunyange.
Alisema tukio la mauaji hayo ni la kusikitisha mno kutokana na Tanzania kusifika kuwa nchi ya amani duniani.
“Tanzania inasifika kuwa na amani duniani kote, lazima hatua za kiusalama zichukuliwe haraka ili kunusuru amani yetu isichezewe.
“Ni tukio la ajabu ambalo limegusa watu wengi wasio na hatia, tutasaidiana na wenzetu kuhakikisha wahalifu hawa wanapatikana,” alisema Jenerali Mwamunyange.
Naye
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Masauni Hamad Masauni, alisema
Serikali inaendelea na uchunguzi kuhusu tukio hilo ili kuwakamata
wahusika ndani ya kipindi kifupi.
Aliwahakikisha wananchi kuwa ulinzi unaimarishwa na kwamba matukio hayo hayatajirudia tena.
“Vyombo vya ulinzi vitafanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha tunawatia nguvuni haraka watu waliohusika na mauaji hayo,” alisema Masauni.
Aliwaomba ndugu na jamaa ambao wamefiwa na ndugu zao kuwa na subira wakati Serikali inaendelea kuchukua hatua.
Naye Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Ernest Mangu alisema wataendelea kuimarisha ulinzi na usalama maeneo yote.
Katika
hatua nyingine, wakazi wa mitaa mitatu ya Mleni Kati, Mleni Mashariki
na Kibatini katika Kata ya Mzizima, Manispaa ya Tanga, wameanza kukimbia
makazi yao kwa kuhofia usalama wao baada ya mauaji hayo.
Mauaji
hayo yalitokea juzi usiku ambapo watu wanaoaminika kuwa majambazi
walivamia nyumba tatu katika eneo hilo, wakiwa wamelala usiku, kisha
kuwateka na kuwapeleka msituni kabla ya kuwachinja.
Wakazi
hao wanaounda zaidi ya kaya 30, walisema wameamua kuyakimbia makazi yao
kwa kutokuwa na imani ya usalama wao katika eneo hilo, baada ya wale
wanaoitwa majamabzi kuvamia makazi yao kwa mara ya pili kwa staili ya
kutisha.
Kabla
ya tukio hilo la juzi, watu wasiofahamika walivamia makazi yao na
kuchinja kuku 40, mbuzi wanne na ng’ombe mmoja na kukimbilia mapango ya
Amboni na hawajawahi kukamatwa.
Mwandishi
wetu jana alishuhudia wanawake na watoto wakiwa na mizigo mithili ya
wakimbizi wakiondoka katika eneo hilo huku wanaume wakibaki kwa ajili ya
kuzika ndugu, jamaa na marafiki zao waliouawa katika tukio hilo.
Mmoja
wa wananchi hao, Juma Issa, alisema wamelazimika kuwahamisha wanawake
na watoto kwa kuhofia wanaweza kuvamiwa tena kwa mara ya pili.
Nae
Lucas Muhina alisema kuwa anashindwa kuhama katika eneo hilo kutokana
na kuwa na mifugo, hivyo anashindwa kujua mahali salama pa kuihifadhi.
Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kibatini, Shabani Mwamini, alithibitisha baadhi ya wananchi wa mitaa mitatu kuhama katika eneo hilo.
“Nyumba nyingi zimebaki na wanaume pekee yake kwani wanawake na watoto wote wamehama kwa sasa,” alisema.
Wakati huohuo, maiti nne kati ya nane zimezikwa jana huku nyingine nne zikisafirishwa nje ya mkoa huo.
Mwamini aliwataja waliozikwa kuwa ni Issa Husein, Mkola Husein, Issa Hamis na Salim Adam.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martin Shigella alisema kuwa vyombo vya dola vinaendelea na uchunguzi kuhusu tukio hilo.
Simulizi ya Mauaji
Mtoto
wa marehemu Mkola Hussein anayeitwa Salimu Mkola (16) alisababisha
vilio na simanzi kwa waombolezaji baada ya kusimulia namna watu hao
walivyomchukua baba yake na kwenda kumchinja mbele ya nyumba yake.
Akisimulia
tukio hilo huku akibubujikwa machozi, mtoto huyo alisema watu hao
walifika nyumbani kwao wakagonga mlango saa sita usiku na kumuamrisha
baba yao atoke na fedha.
“Nilipoona
hivyo nilijaribu kupiga kelele kuomba msaada kwa majirani, lakini mmoja
wa wauaji aliingia ndani na kunitoa nje ya nyumba yetu, huku akiniuliza
wakati wale vijana saba
wanachukuliwa na polisi mimi nilikuwa wapi.
“Waliendelea
kuniuliza kama nina habari ninayoijua, huku wakiwa wameshika mapanga na
bunduki, ndipo waliponiambia wapo kwa ajili ya kutetea dini yetu.
“Baadaye
waliniruhusu niingie ndani na kulala, lakini niliendelea kusikia
vishindo vya kipigo na watu wakikoroma ambayo ilikuwa ni ishara ya kuwa
baba yangu alikuwa anakata roho pamoja na watu wengine,” alisema.
Mtoto
mkubwa wa marehemu, Abuu Mkola, alisema vijana saba ambao sasa
wanashikiliwa na Jeshi la Polisi awali walionekana katika Kitongoji cha
Kibatini wakiwa wanakimbia kusikojulikana.
Alisema
baada ya hali hiyo baba yake ambaye ni marehemu, Mkola Hussein
akishirikiana na wananchi wa mtaa huo walitoa taarifa kwa Jeshi la
Polisi ambao walikuja na kuwakamata vijana hao lakini mmoja wao
alifanikiwa kukimbia.
Abuu
alisema kuwa katika tukio la juzi, wauaji hao wakati wanamchukua baba
yake walisema wanawahitaji vijana wao saba waliokamatwa na polisi,
lakini aliposema hajui ndipo walimuunganisha na watu wengine kwa ajili
ya kumchinja.
Bunge Lataka Taarifa
Ofisi
ya Bunge imeiagiza Serikali kutoa taarifa rasmi kuhusu mauaji
yanayoendelea nchini ili kuwatoa hofu wananchi waliopo katika maeneo
mbalimbali.
Akitoa
maagizo hayo, Naibu Spika, Dk. Tulia Ackson alisema Naibu Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Yusuph Masauni anapaswa kuzungumza na
Kamati za Ulinzi na Usalama katika maeneo yote ambayo yametokea mauaji
ili aweze kutoa taarifa ndani ya Bunge.
“Waziri
atuletee taarifa kwa sababu Waziri Mkuu (Kassim Majaliwa) yupo hapa na
waziri anayehusika na mambo ya Bunge yupo, naomba watuletee taarifa kwa
sababu mauaji yamekuwa yakitokea mara nyingi na tumekuwa tukiwasihi
Serikali ituletee taarifa na si mtakuwa mnazitafuta,” alisema Dk. Tulia.
Baada ya maelezo hayo Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugola (CCM) alisimama na kuomba mwongozo chini ya kanuni 68 (7).
“Mheshimiwa
Naibu Spika pamoja na haya uliyoyatolea maelezo juu ya mauaji
yanayotokea katika nchi yetu, nimelazimika kuomba mwongozo huu kwa
sababu matukio yaliyoanza kujitokeza katika maeneo mbalimbali na maeneo
mengine mambo haya tuliwahi kuyauliza Serikali na kuahidi watayatolea
ufafanuzi.
“Sasa
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani amekwenda kuangalia na atazungumzia
jambo hilo wakati mambo haya wabunge tulishaiomba Serikali itoe
ufafanuzi ni jinsi gani inajipanga kukabiliana nayo,” alisema Lugola.
#YALIYOJIRIBUNGENI: Kambi ya Upinzani imewasilisha hoja ya kumwondoa madarakani Naibu Spika, Dkt. Tulia Ackson kwa kutokuwa na imani naye hii Leo.Fahamu zaidi hapa.
Wabunge wa upinzani wamewasilisha kwa Spika wa Bunge hoja ya kumwondoa
madarakani Naibu Spika, Dk Tulia Ackson kwa kutokuwa na imani naye.
Hatua hiyo imefikiwa na wabunge hao kufuatia kutoridhishwa na mwenendo wa uongozi wa Dk Tulia anapokalia kiti cha Spika.
Tangu Jumanne wiki hii, wabunge hao wamekuwa wakisusa vikao vinavyoongozwa na kiongozi huyo kwa madai anaminya demokrasia.
Walifikia
uamuzi huo baada ya Dk Tulia kuzuia kujadiliwa hoja ya kufukuzwa kwa
wanafunzi zaidi ya 7,000 wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) iliyowasilishwa
na Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari na kukatisha mjadala wa
bajeti ya maji.
Kitendo hicho kiliwafanya wabunge wote wa upinzani kupingana na maamuzi ya Dk Tulia, jambo lililosababisha watolewe bungeni.
Kutokana
na hali hiyo wabunge hao kupitia Mbunge wa Simanjiro, James Ole Millya
akisindikizwa na Mbunge wa Kibamba, John Myika wa Chadema na Mbunge wa
Konde wa CUF, Khatibu Said Haji waliwasilisha hoja hiyo kwa Katibu wa
Bunge, Dk Thomas Kashilillah baada ya Spika, Job Ndugai kutokuwapo
bungeni.
Hoja hiyo iliwasilishwa kwa mujibu wa Kanuni ya 138 (1) ambayo inaeleza utaratibu wa jinsi ya kumwondoa Naibu Spika.
Kanuni
hiyo inasema, “Utaratibu wa kumwondoa Naibu Spika madarakani chini ya
Ibara ya 85(4)(c) ya Katiba utakuwa kama ule wa kumwondoa Spika,
isipokuwa tu taarifa ya kusudio la kumwondoa Naibu Spika madarakani
inayoeleza sababu kamili za kuleta hoja hiyo, itapelekwa kwa Spika
ambaye ataiwasilisha kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge
kwa ajili ya kuijadili.”
Fasili ya pili ya Kanuni hiyo inasema:
“Endapo Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge itaridhika kuwa
zipo tuhuma mahususi dhidi ya Naibu Spika zinazohusu uvunjaji wa Katiba,
Sheria au Kanuni zinazoongoza Shughuli za Bunge, basi Kamati hiyo
itaidhinisha kuwa hoja hiyo ipelekwe bungeni ili iamuliwe.”
Kwa
mujibu wa Ibara ya 85(4)(c), Naibu Spika atakoma kuwa Naibu Spika na
ataacha kiti cha Naibu Spika endapo ataondolewa kwenye madaraka ya Naibu
Spika kwa azimio la Bunge.
Akizungumzia uwasilishwaji wa hoja hiyo, Millya alisema taarifa zaidi watatoa leo kuhusu msimamo wao huo.
Dk
Tulia aliwataka wabunge wenye malalamiko juu ya utaratibu wa uendeshaji
wa shughuli za Bunge kukata rufaa kwa kufuata Kanuni za Bunge.
Alisema
kanuni ndogo ya 5(2) inasema Spika atawajibika kutilia nguvu kanuni
zote za Bunge na 5(3) inasema Spika anaweza kumtaka mbunge yeyote
anayekiuka kanuni hizi kujirekebisha mara moja.
Alisema kwa hiyo mbunge yoyote asiyeridhika, kanuni za Bunge zinamruhusu kukata rufaa na zinamweleza nini cha kufanya.
Wednesday, 1 June 2016
#YALIYOJIRI>>>Serikali Yatoa Ufafanuzi Uboreshaji wa Maslahi ya Polisi na Nafasi za JKT.Fahamu zaidi hapa.
Serikali
imesema kuwa itaendelea kuboresha maslahi ya askari wa Jeshi la Polisi
na kuwajengea nyumba za kisasa za kuishi ili waweze kutekeleza majukumu
yao ipasavyo.
Hayo
yamesemwa na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira
Mhe. Luhaga Mpina wakati akijibu maswali ya wabunge kuhusu mkakati wa
Serikali wa kuboresha maslahi ya Askari wa Jeshi hilo kwa niaba ya Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Bungeni mjini Dodoma leo
Amesema
kuwa Serikali katika mwaka wa fedha 2016/2017 itatekeleza Mpango
kabambe wa ujenzi wa nyumba za Polisi 4136 ambao utakwenda sambamba na
ujenzi wa vituo vya Polisi.
Amesema
Serikali imechukua hatua za haraka kulishughulikia suala la ukosefu wa
nyumba za askari hao katika maeneo mbalimbali nchini ili kuimarisha
ulinzi na usalama katika maeneo yenye ukosefu wa nyumba hizo.
Amelieleza
Bunge kuwa Serikali imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali za kuhakikisha
kuwa maslahi ya Askari Polisi yanaimarishwa ikiwemo malipo ya Posho ya
pango kwa askari wasio na nyumba ambayo ni asilimia 15 ya mishahara yao
ili waweze kulipia gharama hizo.
Ameongeza
kuwa askari wenye utalaam maalum wakiwemo madereva na madaktari
wamekuwa wakilipwa posho ya asilimia 15 ya mishahara yao na kuongeza
kuwa askari wanaoajiriwa katika ajira mpya kama madaktari wamekuwa
wakilipwa mishahara sawa na madaktari wengine bila kujali vyeo vyao.
“Serikali
tumefanya jitihada kubwa sana kuboresha maslahi ya askari wetu, kama
Serikali tumetoa posho za nyumba, posho za utalaam maalum kwa askari
wote ambayo ni asilimia 15 ya mshahara wa kila Polisi hii yote ni
kuwafanya askari wetu waweze kumudu gharama za maisha” Amesisitiza Mhe. Mpina.
Ameeleza
kuwa kwa askari wanaofanya kazi katika mazingira magumu wakiwemo wa
Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) wamekuwa wakipewa posho ya kufanya kazi
katika mazingira magumu (Hardship allowance) kiasi cha shilingi laki
moja (100,000) kila mwezi.
Mhe.
Mpina amebainisha kuwa askari wote wanaohitimu mafunzo yao wamekuwa
wakikatiwa Bima ya Afya kwa asilimia 100 na Serikali pamoja na udhamini
wa mikopo mbalimbali katika taasisi za kifedha ili waweze kupewa mikopo
na taasisi hizo.
Aidha,
amesisitiza kuwa serikali imewapandishia kiwango cha Posho ya katikati
ya mwezi (Ration Allowance) kutoka shilingi 180,000 za awali hadi
300,000 ambazo wanalipwa kwa sasa nchi nzima.
Katika
hatua nyingine Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa imetoa
ufafanuzi kuhusu vijana wa kidato cha nne kutochukuliwa kujiunga na
Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT).
Waziri
wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Hussein Mwinyi amesema kuwa
hatua ya kuwachukua vijana wote wanaomaliza kidato cha nne kwa sasa
haiwezekani kutokana na uwezo mdogo wa kifedha wa Serikali.
Amesema
kuwa uwezo wa JKT kuchukua vijana wa kujitolea kwa sasa ni 5000 hadi
7000 kwa mwaka kulingana na bajeti inayotolewa na kuongeza kuwa mpango
wa Serikali ni kuendelea kutenga fedha na kujenga kambi zaidi za mafunzo
ili kuwawezesha vijana wengi kujiunga na mafunzo hayo kulingana na
upatikanaji wa fedha.
Kwa
upande wa wahitimu wa kidato cha sita wanaotakiwa kujiunga na JKT kwa
mujibu wa Sheria Mhe. Mwinyi amesema Serikali imewachukua vijana 14,000
na inaendelea kujenga uwezo wa ndani wa kuchukua vijana wengi zaidi.
Amesema
Serikali inakusudia kujenga majengo ndani ya makambi ili kuwezesha
vijana wote wanaohitimu kidato cha sita kupitia JKT kabla ya kujiunga na
vyuo mbalimbali hapa nchini.
Aidha,
Amefafanua kuwa kwa wale wanaojiunga na JKT kwa kujitolea ambao idadi
yao inafikia 5000 sio wote wanaopata nafasi ya kuajiriwa katika vyombo
vya Ulinzi na Usalama na kuongeza kuwa ni asilimia 71 ndio hupata ajira
kwenye vyombo hivyo huku waliobaki wakilazimika kurudi nyumbani.
Amebainisha
kuwa Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu inaangalia utaratibu wa
kuwawezesha vijana hao ili wanaporudi uraiani waweze kupatiwa mitaji ya
kuwawezesha kujiajiri wenyewe.
#YALIYOJIRI>>>>NAIBU WAZIRI MASAUNI ATEMBELEA MSITU WA MAPANGOPORI YA AMBONI.Fahamu zaidi hapa.
Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akichungulia
pango lililopo katika msitu wa Mapangopori ya Amboni linalodaiwa kuwa ni
njia kuu ya watu wanaohofiwa majambazi waliofanya mauaji katika
Kitongoji cha Kibatini, Kata ya Mzizima, Tarafa ya Chumbageni, jijini
Tanga.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia) akiwa na vikosi vya ulinzi na usalama vinavyotoa ulinzi katika msitu wa Mapangopori ya Amboni mkoani Tanga. Naibu Waziri alifanya ziara ya kutembelea mapango hayo ambayo yalikuwa makazi ya watu wanaohofiwa majambazi waliofanya mauaji katika Kitongoji cha Kibatini, Kata ya Mzizima, Tarafa ya Chumbageni, jijini Tanga. Kushoto ni Mkuu wa Kikosi Maalum kutoka Kikosi cha Kutuliza Ghasia Makao Makuu Dar es Salaam, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, William Mwampagale.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto meza kuu) akizungumza katika Kikao cha Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama kilichofanyika katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga. Kulia meza kuu ni Mkuu wa Mkoa huo, Martine Shigella. Watatu kushoto ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange na Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali, Ernest Mangu (wapili kushoto). Viongozi hao wamekutana mkoani humo kwa ajili ya kuimarisha ulinzi na usalama mkoani Tanga.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akitoa maelekezo kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Leonard Paulo (kulia), mara baada ya kutoka ndani ya pango lililopo katika msitu wa Mapangopori ya Amboni linalodaiwa kuwa ni njia kuu ya watu wanaohofiwa majambazi waliofanya mauaji katika Kitongoji cha Kibatini, Kata ya Mzizima, Tarafa ya Chumbageni, jijini Tanga. Katikati ni Mkuu wa Kikosi Maalum kutoka Kikosi cha Kutuliza Ghasia Makao Makuu Dar es Salaam, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, William Mwampagale.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia) akiwa na vikosi vya ulinzi na usalama vinavyotoa ulinzi katika msitu wa Mapangopori ya Amboni mkoani Tanga. Naibu Waziri alifanya ziara ya kutembelea mapango hayo ambayo yalikuwa makazi ya watu wanaohofiwa majambazi waliofanya mauaji katika Kitongoji cha Kibatini, Kata ya Mzizima, Tarafa ya Chumbageni, jijini Tanga. Kushoto ni Mkuu wa Kikosi Maalum kutoka Kikosi cha Kutuliza Ghasia Makao Makuu Dar es Salaam, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, William Mwampagale.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto meza kuu) akizungumza katika Kikao cha Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama kilichofanyika katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga. Kulia meza kuu ni Mkuu wa Mkoa huo, Martine Shigella. Watatu kushoto ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange na Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali, Ernest Mangu (wapili kushoto). Viongozi hao wamekutana mkoani humo kwa ajili ya kuimarisha ulinzi na usalama mkoani Tanga.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akitoa maelekezo kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Leonard Paulo (kulia), mara baada ya kutoka ndani ya pango lililopo katika msitu wa Mapangopori ya Amboni linalodaiwa kuwa ni njia kuu ya watu wanaohofiwa majambazi waliofanya mauaji katika Kitongoji cha Kibatini, Kata ya Mzizima, Tarafa ya Chumbageni, jijini Tanga. Katikati ni Mkuu wa Kikosi Maalum kutoka Kikosi cha Kutuliza Ghasia Makao Makuu Dar es Salaam, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, William Mwampagale.
Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto)
akimsalimia Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigella kabla ya kwenda
katika msitu wa Mapangopori ya Amboni mkoani Tanga. Naibu Waziri
alifanya ziara ya kutembelea mapango hayo ambayo yalikuwa makazi ya watu
wanaohofiwa majambazi waliofanya mauaji katika Kitongoji cha Kibatini,
Kata ya Mzizima, Tarafa ya Chumbageni, jijini Tanga. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI.
#YALIYOJIRI>>>>Wabunge waliosimamishwa watoa ya Moyoni.Fahamu zaidi hapa.
Wakiongea
kwa nyakati tofauti Mjini Dodoma, Mbunge wa Kigoma Mjini Mhe. Zitto
Zuberi Kabwe amesema kuwa ni dhahiri wasiwasi waliokuwa nao toka awali
unajidhihirisha wazi kuwa bunge hilo litakua ni kibogoyo na kukosa
maamuzi.
Nae Mbunge wa Bunda Mhe. Esther Bulaya amesema lengo kuu la adhabu iliyotolewa dhidi yao ni kutaka kupunguza nguvu ya upinzani bungeni pamoja na kutaka kuwatisha wabunge washindwe kuwawakilisha wananchi wao ipasavyo.
Kwa upande wake Mbunge aliesimamisha kwa vikao Kumi mfululizo Mhe. John Heche amesema hata kama atarejea ndani ya bunge hilo ataendelea na misimamo yake ya kutetea wananchi bila woga kwa kujali maslahi ya taifa.
Hati hivyo Baraza la Vijana la Chama cha Demkorasia na Maendeleo CHADEMA wamelalamikia kitendo hicho huku wakimtaka Naibu Spika Mhe. Tulia Ackson ajipime mwenye kama anafaa kuendelea kuliongoza bunge hilo huku Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu(LHRC),Hellen Kijo Bisimba akisema hatua hiyo imewanyima haki wananchi kwa wabunge waliowachagua.
Nae Mbunge wa Bunda Mhe. Esther Bulaya amesema lengo kuu la adhabu iliyotolewa dhidi yao ni kutaka kupunguza nguvu ya upinzani bungeni pamoja na kutaka kuwatisha wabunge washindwe kuwawakilisha wananchi wao ipasavyo.
Kwa upande wake Mbunge aliesimamisha kwa vikao Kumi mfululizo Mhe. John Heche amesema hata kama atarejea ndani ya bunge hilo ataendelea na misimamo yake ya kutetea wananchi bila woga kwa kujali maslahi ya taifa.
Hati hivyo Baraza la Vijana la Chama cha Demkorasia na Maendeleo CHADEMA wamelalamikia kitendo hicho huku wakimtaka Naibu Spika Mhe. Tulia Ackson ajipime mwenye kama anafaa kuendelea kuliongoza bunge hilo huku Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu(LHRC),Hellen Kijo Bisimba akisema hatua hiyo imewanyima haki wananchi kwa wabunge waliowachagua.
Msanii mkongwe Jay Moe asema ukimya wake umemfanya ajue wasanii wenzake huwaga wanakosea wapi.Fahamu zaidi Bofya hii link hapa.
Msanii mkongwe wa muziki wa Hip Hop nchini, Jay Moe amesema ukimya wake
kwenye game la muziki umemfanya ajue wasanii wenzake huwaga wanakosea
wapi.
Rappa huyo ambaye amedai amekaa miaka 4 bila kutoa ngoma yake binafsi, ameiambia Bongo5 kuwa amegundua style mpya ambavyo itamfanya afanye vizuri zaidi.
“Unajua kuna kitu fulani kama malaika anakwambia acha hiki fanya hiki, alafu kweli unakifanya na unaona kabisa leo kinaleta manufaa, nimejifunza vitu vingi sana, sasa hivi wasanii wenzangu wanakuja na nyimbo mpya sometime nakuta nacheka, naona mbona nyimbo hii bado haipo kwenye muziki wa siku hizi. Hii time ambayo nilikuwa nje ya muziki nimejikuta nimesoma vitu mpaka vilivyo mbele yangu,” alisema Jay Moe
Aliongeza, “Pia ukimya wangu nilikuwa napanga mambo mengine nje ya muziki, hatuwezi tukafocus kwenye muziki tu, tumeshakuwa watu wazima wengine, huko tunakoelekea tutafanya muziki labda miaka 4 tu. Hatuna muziki wa Marekani wa kuona akina Dr Dre bado wananufaika kazi zao mpaka leo,” alisema Jay Moe.
Jay Moe amesema anajipanga kuachia wimbo wake mpya uitwao ‘Pesa ya Madafu’.
Rappa huyo ambaye amedai amekaa miaka 4 bila kutoa ngoma yake binafsi, ameiambia Bongo5 kuwa amegundua style mpya ambavyo itamfanya afanye vizuri zaidi.
“Unajua kuna kitu fulani kama malaika anakwambia acha hiki fanya hiki, alafu kweli unakifanya na unaona kabisa leo kinaleta manufaa, nimejifunza vitu vingi sana, sasa hivi wasanii wenzangu wanakuja na nyimbo mpya sometime nakuta nacheka, naona mbona nyimbo hii bado haipo kwenye muziki wa siku hizi. Hii time ambayo nilikuwa nje ya muziki nimejikuta nimesoma vitu mpaka vilivyo mbele yangu,” alisema Jay Moe
Aliongeza, “Pia ukimya wangu nilikuwa napanga mambo mengine nje ya muziki, hatuwezi tukafocus kwenye muziki tu, tumeshakuwa watu wazima wengine, huko tunakoelekea tutafanya muziki labda miaka 4 tu. Hatuna muziki wa Marekani wa kuona akina Dr Dre bado wananufaika kazi zao mpaka leo,” alisema Jay Moe.
Jay Moe amesema anajipanga kuachia wimbo wake mpya uitwao ‘Pesa ya Madafu’.
#YALIYOJIRI>>>Utafiti: Mbwa kuwa tiba ya Malaria.Fahamu zaidi hapa.
Watashirikisha usaidizi kutoka watoto 400 wa Gambia,ikiwemo baadhi ambao wanajulikana kuwa na ugonjwa wa Malaria ambao watahitajika kuvaa soksi za nailoni kwa saa 24.
Mbwa hao watafunzwa kubaini kati ya violezo vya malaria na vile ambavyo sivyo.
Mmoja ya watafiti James Logan aliambia BBC Newsday kwamba hatua hiyo itasaidia kuzuia kusambaa kwa Malaria.
Chanzo
BBC SWAHILI.
#YALIYOJIRI>>>ZITTOKABWE:Kukubali kufanywa vikaragosi vya viongozi ni dalili ya woga.Fahamu zaidi hapa.
Hiki ndo alicho kisema Zittokabwe kwenye ukulasa wake wa Instagram"Kukubali kufanywa vikaragosi vya viongozi ni dalili ya woga,
si dalili ya heshima; na woga na heshima ni vitu viwili mbali mbali.
Maadili mema hayatudai tuwaogope viongozi wetu. Na viongozi makini
hupenda kupata heshima ya wananchi wenzao, lakini hawapendi kuogopwa.
Kuogopwa ni sifa na ada ya madikteta, viongozi halisi hawapendi
kuishiriki. Kujenga mazoea ya kutii viongozi hata katika mambo haramu ni
dalili ya woga, ni kukaribisha udikteta"
UONGOZI WETU NA HATMA YA TANZANIA...MWL J.K.NYERERE.
Rose Ndauka:Ahadi yangu ipo pale pale.Fahamu zaidi hapa.
Msanii wa Filamu bongo Rose Ndauka
Akizungumza
na eNewz Rose alisema kuwa yeye hajashindwa kufanya hivyo kwa kuwa
tayari anawasanii ambao wameshawasajili wakiwa na nyimbo zao tayari na
kudai kuwa yeye peke yake hawezi kwakuwa hafahamu kitu kuhusu muziki
lakini kwa kusaidiana na wataalamu ambao yupo nao watakamilisha tu hivi
karibuni
Aidha, Rose aliweza kutoa maoni yake kuhusiana na kauli iliyokuwa imetolewa na nguli wa filamu nchini Bibi Hindu dhidi ya wasanii wa kike wa Bongo movie kuhusu uvaaji wao wa nusu uchi mpaka kufikia filamu kushindwa kuangaliwa na watoto wakiwa na wazazi wao,
"Hakuna shida mtu kuvaa kimini kama mtu ana mguu unamruhusu kuvaa hivyo inategemea na uhusika tu wako tu na pia filamu zinaandikwa kabisa kuwa hii inaangaliwa na wote na hii hairuhusiwi kuangaliwa na mtoto wa chini ya miaka kumi nane kwanini sasa watoto waangalie,” alihoji Rose Ndauka.
Aidha, Rose aliweza kutoa maoni yake kuhusiana na kauli iliyokuwa imetolewa na nguli wa filamu nchini Bibi Hindu dhidi ya wasanii wa kike wa Bongo movie kuhusu uvaaji wao wa nusu uchi mpaka kufikia filamu kushindwa kuangaliwa na watoto wakiwa na wazazi wao,
"Hakuna shida mtu kuvaa kimini kama mtu ana mguu unamruhusu kuvaa hivyo inategemea na uhusika tu wako tu na pia filamu zinaandikwa kabisa kuwa hii inaangaliwa na wote na hii hairuhusiwi kuangaliwa na mtoto wa chini ya miaka kumi nane kwanini sasa watoto waangalie,” alihoji Rose Ndauka.
#YALIYOJIRI>>>>Rais Magufuli amteua Dr. Kyaruzi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi TANESCO.Fahamu zaidi hapa.
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzanoa Dr. John Pombe Joseph Magufuli
leo tarehe 31.05.2016 amemteuwa Dr Alex L. Kyaruzi kuwa mwenyekiti wa
bodi ya wakurugenzi wa shirika la umeme Tanzania (TANESCO).
Kufuatia uteuzi huo, Waziri wa Nishati Prof Sospeter Muhongo amewateua wafuatao kuwa Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa shirika la umeme Tanzania ( TANESCO) kuanzia tarehe 31.05.2016 hadi tarehe 30.05.2019
1.Dkt. Samwel Nyantahe
2.Dkt. Lugano Wilson
3.David Elias Alal
4.Mhandisi Stephen Peter Mabada
5.Mhandisi Leonard R. Masanja
Aidha, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amekamilisha uteuzi wa Wajumbe wa Bodi ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO). Kuanzia tarehe 31.05.2016 hadi tarehe 29.05.2019
**Abdalah H. Musa
**Dkt. Coretha Komba
**Felix M. Maagi
**Dkt. Lightness Mnzava
**John B. Seka
Aidha imeelezwa kuwa uzinduzi wa bodi hizi utafanyika makao makuu ya mashirika haya tarehe 02.06.2016 siku ya Alhamis saa 4:00 asubui kwa STAMICO na Saa 8:00 Mchana kwa Tanesco.
Kufuatia uteuzi huo, Waziri wa Nishati Prof Sospeter Muhongo amewateua wafuatao kuwa Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa shirika la umeme Tanzania ( TANESCO) kuanzia tarehe 31.05.2016 hadi tarehe 30.05.2019
1.Dkt. Samwel Nyantahe
2.Dkt. Lugano Wilson
3.David Elias Alal
4.Mhandisi Stephen Peter Mabada
5.Mhandisi Leonard R. Masanja
Aidha, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amekamilisha uteuzi wa Wajumbe wa Bodi ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO). Kuanzia tarehe 31.05.2016 hadi tarehe 29.05.2019
**Abdalah H. Musa
**Dkt. Coretha Komba
**Felix M. Maagi
**Dkt. Lightness Mnzava
**John B. Seka
Aidha imeelezwa kuwa uzinduzi wa bodi hizi utafanyika makao makuu ya mashirika haya tarehe 02.06.2016 siku ya Alhamis saa 4:00 asubui kwa STAMICO na Saa 8:00 Mchana kwa Tanesco.
#YALIYOJIRI>>>>Magufuli: Serikali Itakomesha Watumishi na Wanafunzi Hewa.Fahamu zaidi hapa.
RAIS
John Magufuli (pichani) amesema Serikali ya Awamu ya Tano imejipanga
kumaliza makosa yote yaliyojitokeza huko nyuma ikiwemo tatizo la
watumishi na wanafunzi hewa lililoibuka hivi karibuni.
Amewataka
Watanzania kuacha kuingiza siasa kwenye makosa yanapojitokeza, hasa
yale yanayogusa sehemu nyeti kama elimu, kwani yakiachwa kuna uwezekano
wa kutengeneza taifa la watu wa ajabu.
Alisema
tangu aingie madarakani amekumbana na changamoto mbalimbali, ikiwemo
matatizo ya rushwa, ukwepaji kodi, watumishi hewa na sasa amekumbana na
tatizo la wanafunzi hewa.
“Nchi
yetu ina changamoto na mambo mengi sana hata mimi nimekumbana na
changamoto naziona mwenyewe, nikigeuka hivi watumishi hewa ambao hadi
sasa wamefikia 10,500, nikigeuka hivi kuna wanafunzi hewa,” alisisitiza.
Alisema
ni Tanzania pekee ambayo mtu anaweza kupata daraja la nne kidato cha
nne katika elimu ya sekondari, halafu akapata fursa ya kujiunga na chuo
kikuu na kupatiwa mkopo wa serikali, wakati mhitimu aliyefaulu kidato
cha sita akikosa fursa hiyo.
Alisema
endapo kulifanyika makosa lazima yarekebishwe, kwani inafahamika fika
mtu akimaliza kidato cha nne akifeli ataanzia ngazi ya Astashahada,
Stashahada ndio apate nafasi ya kujiunga chuo kikuu.
“Sasa hapa kwetu ni tofauti ukifeli kidato cha nne unajiunga chuo kikuu,” alihoji
na kuwataka watu waache siasa kwenye makosa kwani mambo kama hayo
yakiachwa kuna hatari ya nchi kutengeneza taifa la ajabu.
Hivi
karibuni, Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo Ufundi,
Profesa Joyce Ndalichako aliivunja Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) na
kuwasimamisha kazi viongozi wanne waandamizi kwa tuhuma za kudahili
wanafunzi wasio na sifa.
Aidha,
Mwenyekiti wa Bodi ya TCU, Awadh Mawenya naye alisimamishwa kazi kwa
kosa la kushindwa kuwachukulia hatua watumishi waliodahili wanafunzi hao
wasio na sifa.
Profesa
Ndalichako alichukua hatua hizo baada ya TCU kudahili wanafunzi 489
waliopata daraja la 4.32 katika mitihani yao ya kidato cha nne lakini
walijiunga na chuo kikuu na kupatiwa mikopo yenye thamani ya Sh milioni
784.
Picha: Harmonize Amtambulisha Wolper Ukweni.Fahamu zaidi hapa.
Wikiiliyopita staa anaechipukia kwenye bongo fleva Harmonize alimpeleka
mpenzi wake Jacqueline Wolper kwao Mtwara alikoenda kutumbuiza kwa mara
ya kwanza tangu aukwae ustaa kupitia label ya WCB.
“Time Ya Kumsaidia mama Harmo Kuanda Chakula Cha Usiku Mtwara Life
@wolperstylish,” aliandika Harmonize kwenye picha inayomuonesha Wolper
akichuma matembele shambani.
Naye Wolper alipost picha akiwa na mama mkwe na kuandika: I am having
the best time of my life.. Nikiwa na Mama angu… Kabla hamjatoka lazima
mpige story, akuchekeshe… Mjipikilishe.. Akushauri
Hapa nimepata rafiki kwa kweli…I love my mama Mkwe.. Mama Raj wangu.”
Bongo5
Wolper akiongea na mama yake Harmonize
Hapa nimepata rafiki kwa kweli…I love my mama Mkwe.. Mama Raj wangu.”
Bongo5






















