Saturday 8 October 2016

#MICHEZO>>>>IVO MAPUNDA HATAKI MCHEZO; AMEAMUA KUFUATA NYAYO ZA RAIS MUGABE.FAHAMU ZAIDI HAPA.

  IVO na RAIS MUGABE
Kipa mkongwe nchini aliyewahi kukipiga katika timu za Moro United, Yanga na Simba, Ivo Mapunda, amesema atastaafu kucheza soka siku akisikia Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe ametoka madarakani.

Ivo ambaye anasubiri kwenda kucheza soka Kenya, amesema kwa sasa hana kabisa mawazo ya kustaafu soka kama ilivyo kwa Rais Mugabe ambaye tangu aingie madarakani Desemba 22, 1987, mpaka leo bado ni rais wa nchi hiyo.
IVO
 
Mlinda mlango huyo, pia amewahi kucheza Gor Mahia ya Kenya na Saint George ya Ethiopia.


Ivo alisema bado nguvu anazo, hivyo akistaafu soka kwa sasa atakuwa hajakitendea haki kipaji chake, sasa anasubiri simu kutoka Kenya aende akacheze soka.“Labda watu wanaotaka kujua nitastaafu lini, niwaambie tu wasubiri siku wakimuona Mugabe anaachia madaraka ndiyo na mimi hapo hapo nitaacha kucheza soka,” alisema Ivo.

Mugabe ndiye rais anaongoza kukaa kwa muda mwingi zaidi madarakani huku akiendeleza ubabe bila ya woga hata kwa nchi za Magharibi.

SOURCE: CHAMPIONI

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi

Bonyeza Hapa CLICK HERE
 

0 comments:

Post a Comment