Sunday 9 October 2016

#YALIYOJIRI>>>>AJALI NYINGINE INAYOHUSISHA BASI LA MWENDO KASI.FAHAMU ZAIDI HAPA.

Ajali nyingi zimekuwa zikitokea Tangu kuanza kwa Magari yaendayo kasi, huku kubwa zaidi ikidaiwa kuwa suala la elimu kuhusu matumizi ya njia za magari yaendayo kuwa kikwazo kwa baadhi ya madereva wa magari na bodaboda.

Katika pitapita za Mtembezi imekutana na ajali inayolihusisha basi la mwendo kasi na gari lenye namba za usajili T 154 DEP katika barabara ya Morogoro, jirani na msikiti mkubwa wa dhehebu la Shia jijini Dar es Salaam.

Basi hili la Mwendokasi lilikuwa linaelekea Kimara, huku gari hiyo ikiwa inatokea maeneo ya Msikiti huo mkubwa wa dhehebu la Shia, hakuna kifo wala majeruhi walioripotiwa licha ya gari lenye namba za usajili T 154 DEP kuchubuliwa na kubonyea kwa ndani.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi

Bonyeza Hapa CLICK HERE

 
<<<<DOWNLOAD APPLICTION KWENYE SIMU YAKO HAPA>>>

0 comments:

Post a Comment