Friday 7 October 2016

#MICHEZO>>>>>Baraza la Michezo nchini (BMT) leo limetangaza kutotambua ukodishwaji wa Klabu ya Yanga.Fahamu zaidi hapa.

Sasa kumekucha wapenda michezo wenzangu hii ni kufuatia Baraza la Michezo Tanzania (BMT) leo limetangaza rasmi kutotambua ukodishwaji wa Klabu ya soka ya Yanga
Baraza la BMT lasema ni kinyume na Katiba ya Klabu hiyo.

Baraza la michezo Tanzania (BMT) limetangaza kujitambua ukodishwaji wa klabu ya Yanga kwa kuwa ni kinyume na katiba ya klabu hiyo.

Katibu mkuu wa BMT, Mohammed Kiganja amesema kuwa mkataba huo kati ya Baraza la Wadhamini wa Yanga na kampuni iliyoikodi klabu hiyo, haukufuata taratibu.

"Ili Yanga iweze kubadili jina na kuitwa Yanga Yetu ni lazima ipite kwa msajili. Wao hawajaenda kwa msajili wanaanza kutangaza jina jipya. Huko ni kupinga katiba," alisema Kiganja.

0 comments:

Post a Comment