Home »
Michezo
» #MICHEZO>>>GOLI LA VAN PERSIE LAWA GOLI BORA EPL.FAHAMU ZAIDI HAPA.
Unakumbuka magoli ya ajabu ambayo aliyekuwa nyota wa zamani wa
Arsenal alitimka Emirate 2012 na kumfuata Ferguson baadae akachukua
ubingwa wa England kwa mara ya kwanza, huyu ni Robin Van Persie huwa
anafunga magoli ya ajabu ajabu sana haswa pale anapopata nafasi.
Unakumbuka lile goli ambalo alipata pasi kutoka nyuma ya eneo la
katikati ya uwanja kutoka kwa Wayne Rooney ? Ilikuwa kati ya Manchester
United dhidi ya Aston Villa ile pasi ikaja nyuma yake ikampita
akaiunganisha na kuingia nyavuni moja kwa moja, sio mara ya kwanza
kufunga magoli kama yale aliwahi kufunga goli lile 2005 kati ya Arsenal
na Leeds United pasi ikatoka kwa Emanuel Eboue upande wa kulia akapiga
mua kama alioupiga akiwa Manchester United na kuweka kimiani.
Sasa goli lake limechaguliwa kuwa goli bora kule EPL tukio hilo
limefanyika katika jiji la London kutimiza miaka 25 ya Ligi Kuu England,
mchakato ulikuwa mkubwa maana walichaguliwa wachezaji mbalimbali ambao
waliowahi kufunga magoli 100 na zaidi katika ligi hiyo na goli lake
ndilo likachaguliwa goli bora.
Baada ya hafla hiyo Van Persie amechangia watoto wenye mazingira
magumu kiasi cha £20,000 kwa ajili ya watoto hao, katika maelezo yake
Persie amesema amefurahi sana kwa tukio hilo na anajihisi furaha sana
hasa ukizingatia ndio ubingwa wake wa kwanza akicheza nchi hiyo.
0 comments:
Post a Comment