Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRL) Masanja Kadogosa
amevikana vichwa vya treni ambavyo vipo bandarini na kusema katika
kipindi chote wakati yeye anatumikia nafasi hiyo hajawahi kusaini
mkataba wowote wa kuingiza vichwa hivyo nchini.
"Unapozungumzia tumeagiza
vichwa vya treni ni kwamba lazima kuwe na muuzaji na mnunuaji na kuna
huduma za malipo, TRL haijafanya 'transaction' wala hatujaingia mkataba
wowote na mtu yoyote kutuletea vichwa vya treni nchini, mambo mengine
yatafahamika baada ya kufanyika kwa uchunguzi kwani ndiyo litakuja kuwa
wazi kwamba nini kimetokea, lakini kama tulivyosema TRL pamoja na mimi
kwa mwaka wangu mmoja niliokaa hapa sijasaini mkataba wowote na mtu
yoyote kwa ajili ya kuletewa vichwa hivyo ambavyo vipo
bandari. Tumeshawambia hata bandari kuwa vichwa hivyo hatujaviagiza
sisi, hatujawaambia kutuletea na hatujatuma mtu yoyote kukamilisha
malipo sababu si vyetu" alisema Masanja Kadogosa Mkurugenzi wa TRL
Siku ya Jumapili ya tarehe 2, Juni 2017 Rais Magufuli alikwenda kuweka
jiwe la msingi katika mradi wa upanuzi wa bandari ambapo aligundua kuna
zaidi ya vichwa 10 vya treni ambavyo havijulikani ni mali ya nani, wala
haijulikana vimeagizwa na nani, hivyo aliagiza uchunguzi ufanyike na
ifahamike vichwa hivyo vya treni vimeletwa na nani nchini. Download Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa
Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa
0 comments:
Post a Comment