Kiungo wa klabu ya Simba SC, Muzamiru Yassin amekuwa almasi kwa baadhi ya timu za Afrika Kusini.
Muzamiru yuko Afrika Kusini akiitumikia timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) katika michuano ya Cosafa ambayo imetinga nusu fainali kwa kuwatoa wenyeji Afrika Kusini hatua ya robo fainali.
Taarifa zinaeleza, mawakala kadhaa wameanza kumfuatilia kwa karibu baada ya kuwa mmoja wa wachezaji waliofanya vizuri zaidi katika michuano.
Baadhi ya magazeti ya Afrika Kusini yameeleza kuwa nyota huyo wa Simba na timu ya taifa amekuwa lulu kutokana na uwezo aliyo uonyesha katika mechi zote ambazo Stars imecheza.
Imeelezwa miongoni mwa timu zilizovutiwa ni Bidvest na Mpumalanga Black Ace lakini wataalamu wanaofuatilia wachezaji(mawakala) wanaweza kuwapeleka wachezaji hata katika timu za nje ya Afrika Kusini.
Katika michuano hiyo Muzamiru amekuwa injini kuu ya kuendesha kiungo cha Stars na kusababisha mvuto mkubwa kwa watazamaji.
Download Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa
Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa
0 comments:
Post a Comment