Monday 7 August 2017

MANARA AMTAMBULISHA MGHANA MPYA WA SIMBA MAKAO MAKUU MSIMBAZI.

Mshambuliaji Nicolas Agyei leo ametambulishwa rasmi katika klabu yake mpya ya Simba.


Agyei ametambulishwa makao makuu ya klabu ya Simba baada ya kuwasili nchini leo usiku.

Raia huyo wa Ghana amekuwa ndiye mchezaji wa mwisho kujiunga wakati wa usajili.

Msemaji wa Simba, Haji Manara ndiye aliyemtambulisha Agyei mbele ya baadhi ya waandishi wa habari na baadhi ya wanachama wa Simba waliokuwa klabuni hapo.
Pamoja na Mghana huyo, wengine waliotambulishwa klabu hapo ni Haruna Niyonzima, Emmanuel Okwi na wenyeji wawili, Method Mwanjale na Mohamed Hussein Zimbwe.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment