Friday 14 August 2015

#YALIYOJIRI>>>>Rais Jakaya Kikwete amesaini hati tatu za maadili jijini Dar es Salaam.




Imeelezwa kuwa sekta binafsi zimetajwa kuwa na mchango mkubwa katika harakati za seriklai za kupambana na tatizo la rushwa amabalo limekuwa likiathiri shughuli za kimaendeleo hapa nchini.
Hayo yameelezwa na rais Jakaya Kikwete muda mfupi baada ya kutia saini hati tatu za maadili ambapo amesema licha ya baadhi ya watendaji katika sekta ya umma kulalamikiwa katika suala la rushwa sekta binafsi zinaweza kuisadia serikali katika kukabiliana natatizo hilo.

Waziri wa nchi ofisi ya rais utawala bora George Mkuchika amewasisitiza watendaji katika sekta ya umma kuhakikisha wanatekeleza ahadi za viapo hivyo vya maadili nakwamba maadili yatakuwa ni moja ya kigezo katika ajira yoyote serikali huku akisisitiza kuanza kufanya kazi muda mfupi baada ya kusainiwa na rais.

Licha ya kuwa na mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi nchini, sekta binafsi inasema ni vema sekali ikajitahidi kushughulikia rushwa kwani kwa kiasi kikubwa imekuwa ikiathiri utendaji wao wa kazi hasa kwa wawekezaji.

Hati hizo tatu zilizosainiwa ni pamoja na hati ya ahadi ya maadili kwa viongozi wa umma, hati ya ahadi ya maadili kwa watumishi wa umma na hati ya ahadi ya maadili kwa sekta binafsi.

Hafla hiyo ya utiaji saini ahadi za maadili imefanyika Ikulu jijini Dar es Salaam na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wandamizi serikalini ambapo kwa mujibu wa tume ya maadili utekelezaji wake tayari umekwisha kuanza.
Chanzo
             ITV HABARI.

0 comments:

Post a Comment