Thursday 13 August 2015

#YALIYOJIRI>>>NEC yataja majina ya wagombea wa nafasi za ubunge na uwakilishi katika majimbo yote.



Halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi CCM NEC imemaliza vikao vyake mjini Dodoma na kutangaza majina ya wagombea wa nafasi za ubunge na uwakilishi katika majimbo yote ya uchaguzi bara na visiwani watakao peperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi mkuu ujao huku idadi kubwa ya majina ikiwa ni ya wabunge na wajumbe wanaotetea nafasi zao za awali.
Kikao hicho kilichokutana kwa siku mbili kikitanguliwa na kikao cha makati ya usalama na maadili na kisha kamati kuu pamoja na mambo mengine kimepitia taarifa mbalimbali pamoja na malalamiko ya baadhi ya wagombea sambamba na kupitisha ilani ya uchaguzi ya CCM kwa mwaka 2015 huku majimbo 11 yakishindwa kupata wagombea kutokana na sababu mbalimbali.

Mwaandishi  alizungumza na baadhi ya wajumbe wa halmashauri kuu na wagombea waliopitishwa kupeperusha bendera ya CCM katika nafasi za ubunge kuhusu namna mchakato huo ilivyoendeshwa ambapo wanakiri kulikuwa na changamoto kadha wa kadha huku wakitaka mfumo huo uangalie namna na kupambana na vitendo vya rushwa ambavyo vilikuwa vikitajwa kugubika mchakato mzima.

Nao baadhi ya wakazi wa mji wa Dodoma wanatoa maoni tofauti hukusu zoezi zima la kuwapata wagombea wa nafasi za ubunge na uwakilishi kupitia CCM huku wakiwataka kuwa na dhamira ya kweli ya uongozi na wasigeuze nafasi hizo za kuwawakilisha wananchi kuwa ni ajira zao.
TOA MAONI YAKO HAPA.


0 comments:

Post a Comment