Thursday 6 August 2015

#YALIYOJIRI>>Wahamiaji trakibani 300 wamepelekwa Bandari ya Italia.




Wahamiaji trakibani ya watu 300 waliookolewa baada ya boti kupinduka karibu na ufuo wa Libya siku ya jumatano wamewasili nchini Italia.walifikishwa katika bandari ya Palermo kwa meli ya jeshi la wanamaji wa Ireland, Alhamisi jioni likiwa na manusura 367 ndani yake, kati yao wanawake 13 na watoto 12. Shirika la madaktari wasio na mipaka kulikuwa na miili takriban 25 iliyoopolewa
Kwa mujibu wa msemaji wa Shirika la kuhudumia wakimbizi duniani, UNHCR, Barbara Molinario, Watu waliookolewa wanatoka nchini Syria,Bangladesh, Eritrea na wengine kadhaa kutoka nchi za Afrika kusini mwa jangwa la sahara.
Manusura hao wanapatiwa huduma za msingi kama vile chakula,maji,mavazi,na huduma za afya, wengine wengi wanapewa ushauri nasaha na huduma za saikolojia baada ya kufikwa masaibu.
Hivi sasa wamepelekwa katika vituo mbalimbali nchini Italia ambapo watakuwa kwenye vituo hivyo kwa siku kadhaa kabla ya kuanza utaratibu kwa kuomba hifadhi nchini humo.
Inakisiwa kuwa kulikuwa na watu 600 kwenye Boti hiyo, idadi ambayo hata hivyo ni vigumu kuthibitisha, hivyo hakuna anayefahamu idadi ya watu ambao hawajapatikana mpaka sasa.
Wahamiaji takriban 2000 wamepoteza maisha mwaka huu pekee wakati wakijaribu kusafiri kupitia bahari ya maditerrania wakielekea Ulaya.
Chanzo
                BBC.

0 comments:

Post a Comment