Mwili
 wa aliyekuwa spika wa bunge,  Samuel Sitta unatarajia kuwasili nchini 
siku ya Alhamis ukitokea nchini Ujerumani ambapo alipokuwa akipatiwa 
matibabu.
Taarifa hiyo imetolewa na Gerald Mongela ambaye ni msemaji wa familia.  
Amesema
 mara baada ya mwili huo kuwasili nchini utapelekwa nyumbani kwa 
marehemu Masaki jijini Dar es Salaam na siku ya Ijumaa shughuli za kuaga
 zitafanyika katika viwanja vya Karimjee kisha kupelekwa bungeni mjini 
Dodoma.
“Mwili
 wa mpendwa wetu mheshimiwa Samuel Sitta utawasili na ndege ya Emirates 
siku ya Alhamis saa tisa na nusu alasiri na baada ya hapo mwili 
tutauleta hapa nyumbani kwaajili ya kukaa nao na kupumzika kusubiri 
ratiba ya Ijumaa,”alisema Mongela.
Mazishi ya Marehemu Samwel John Sitta yatafanyika siku ya Jumamosi Urambo mkoani Tabora. 













0 comments:
Post a Comment