Leo November 8, 2016 Wamarekani wanafanya uamuzi wa mwisho
kupitia karatasi zenye alama ya tiki kwenye mabox ya kura ili kumpata
mshindi ambaye atakuwa Rais wa 45 wa taifa hilo atakayeongoza kwa miaka
minne.
Pamoja na kura zote zitakazopigwa na Wamarekani leo, bado hazina
maamuzi ya moja kwa moja mpaka pale wajumbe 538 wanaoteuliwa kutoka
katika majimbo yote 50 nchini humo watakapoamua kupitisha jina moja la
mshindi wa Urais.
Kwa mujibu wa sheria za Urais Marekani, ili mgombea athibitishwe kuwa
mshindi wa kiti cha Urais inabidi apate sio chini ya kura 270 kutoka
kwa wajumbe hao 538 ambao huamua mshindi kwa namna watu walivyopiga kura
katika majimbo mbalimbali.
Hillary Clinton na Mumewe Bill wakipiga Kura.
Wakati wa uchaguzi wa mwaka 2012, Barrack Obama alipata ushindi baada
ya kuchaguliwa kwa kura zaidi ya Milioni 65 za raia wa nchi hiyo huku
mpinzani wake Mitt Romney akipata zaidi ya Milioni 60 ambapo baada ya
kura za Wajumbe kupigwa, Obama alipata ushindi wa Wajumbe 332, Romney
206.
Wajumbe walivyopiga kura kwenye uchaguzi wa mwaka 2012
Wakati kura zimeshaanza kupigwa nchini humo inaelezwa kuwa kuna
majimbo ambayo ni ngome ya chama cha Republican sawa na Democratic
lakini kuna majimbo mengine kama Florida, Pennsylvania na Ohio ambayo
hayana mshindi wa jumla, hayo ndio majimbo ambayo yataamua mshindi.
Pamoja na kumchagua Rais siku ya leo Jumanne raia wa Marekani wanapiga
kura kuwachagua wawakilishi 435 watakaofanya kazi kwa muda wa miaka
miwili.
0 comments:
Post a Comment