Friday 16 December 2016

KWA AJILI YA MGHANA, KOCHA JOSEPH OMOG ALAZIMIKA KUPANGUA KIKOSI.FAHAMU ZAIDI HAPA.

Benchi la ufundi la Simba chini ya Kocha Mkuu, Joseph Omog, limeridhishwa na kiwango cha kiungo Mghana, James Kotei ambaye amepewa mwaka mmoja. 


Kiungo huyo maarufu kama Mzima Swichi, anamudu kucheza nafasi ya kiungo mkabaji, nafasi anayocheza nahodha, Jonas Mkude, hivyo kuzua sintofahamu ya nani aanze kwenye nafasi hiyo.


Omog amezima maswali hayo kwa kusema kuwa licha ya wote kucheza nafasi moja, bado anaweza kuwatumia kwa pamoja, muhimu ni kucheza na aina ya mfumo kulingana na mechi husika.


Hata hivyo, Mcameroon huyo tangu atue Simba amekuwa akitumia mfumo wa 4-4-2 au 4-5-1 lakini hajawahi kutegemea viungo wawili wakabaji, jambo ambalo litaonekana kwa Mkude na Kotei iwapo atawatumia wote.

“Kweli Kotei naye ni kiungo mkabaji, lakini nafasi ya Mkude kama nahodha ipo palepale, awali sijui nini kilitokea kati yake na uongozi hadi akachelewa kambini lakini bado Mkude ana nafasi yake.


“Pia wanaweza kucheza wote katika mechi moja kulingana na mfumo nitakaoutumia. Siwezi kuutaja maana hiyo ni sawa na kumpa silaha adui, lakini ukweli bado wanaweza kucheza kwa pamoja,” alifunguka kocha huyo wa zamani wa Azam FC kwenye mahojiano maalum.


Wakati huohuo, Kocha Msaidizi wa Simba, Jackson Mayanja ‘Mia Mia’, amesema hawatishiki na rekodi mbovu za watani wao, Yanga kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona wa Ndanda ambako hawajawahi kushinda.


Amesema hayo wakati Simba ikitarajiwa kucheza dhidi ya Ndanda, keshokutwa Jumapili katika Ligi Kuu Bara.


“Sisi hatuchezei rekodi, muhimu ni kuandaa timu kuhakikisha inashinda katika mazingira yoyote, haijalishi ugenini ama nyumbani.”



Download  Application ya Hebron Male Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

 

0 comments:

Post a Comment