Katika mkutano wao wa KUMUIDHINISHA rasmi mgombeaji wa upinzani wa ODM
dhidi ya rais Kenyatta. Mh. Raila odinga alitumia video ya kushangaza
sana iliyomwonyesha Rais wetu John Pombe Magufuli kama vile ANASAPOTI
kampeni ya RAILAOdinga.
Mimi binafsi naona ni kama strategists wa NASA wamefanya MAKSUDI ili KUTUGOGANISHAU kati yetu na jirani zetu wazuri Kenya.
Urafiki wao wawili walipokuwa MAWAZIRI hauhusiani HATA KIDOGO na maswala ya USALAMA wa nchi yetu.
Nina maana Magufuli sasa is AN INTERNATIONAL FIGURE/Mtu wa KIMATAIFA.
Hivyo kumweka kwenye VIDEO ya KUOMBA URAIS Kenya HAIMHUSU hata kidogo na
NIKUTUCHONGANISHA!
Kwanza yeye ni Mwenyekiti wa EAC na haitajiki kuwa na upendeleo wowote.
Kampuni za Kenya hapa Tanzania zimeajiri watu 50 elfu na zaidi.
Ni vizuri IKULU ama MSEMAJI wa serikali atoe KAULI rasmi, kuwa Tanzania
haipendelei MGOMBEAJI yeyote yule nchini Kenya na maamuzi ya Wakenya ndo
yatakubalika katika Jumuia ya Africa Mashariki.
Hii itatusaidia Raila Odinga ASIITUIINGIZE katika mizozano isiyo na tija
kati yetu na Kenya maana HATUJUI nani atakuwa RAIS wa KENYA baada ya
UCHAGUZI..
Download Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa
Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa
0 comments:
Post a Comment