Tuesday 10 October 2017

Wanajeshi wawili wa Tanzania wauawa Huko Kongo.

Askari wawili wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania, wameuawa kwenye mashambulizi makali yanayoendelea nchini Kongo.

Tukio hilo limetokea katika eneo la Beni ambako Askari wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani wanapigana na kikundi cha waasi cha Uganda (ADF), kilichoanza vurugu na ukiukaji wa haki za binadamu kwa kuua raia.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amethibitisha kuuawa kwa wanajeshi hao kutoka Tanzania, huku akitoa tarifa kuwa askari wengine 18 kutoka nchi tofauti wamejeruhiwa.

Pamoja na hayo Katibu Mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa amehimiza mamlaka za Kongo kuchunguza haraka tukio hilo na kuwachukulia hatua wahusika.

Hivi karibuni nchini Kongo kumekuwa na machafuko baada ya vikundi vya uasi kuanza tena vurugu na mauaji baada ya miaka kadhaa kupita kukiwa shwari, huku serikali ya nchi hiyo na Umoja wa Mataifa wakiishtaki ADF kwa ukiukaji wa hai za binadamu na mauaji ya watu zaidi ya 700 katika eneo la Beni, tangu Oktoba 2014.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment