Tuesday 10 October 2017

Rais wa TFF Atembelea Makao Makuu ya Shirikisho la Soka Barani Afrika CAF.

Rais wa shirikisho la soka nchini Tanzania Wallace Karia pamoja na Kaimu Katibu Mkuu Kidao Wilfred wametembelea makao makuu ya shirikisho la soka barani Afrika CAF na kukutana na Rais Bw. Ahmad Ahmad.

Ziara hiyo ya Rais Karia imefanyika jana ambapo walitua kwenye ofisi za CAF zilizopo Cairo nchini Misri na kupokelewa na Rais Ahmad Ahmad kisha kufanya kikao kilichojadili maendeleo ya soka nchini.

Aidha kikao hicho kilihudhuriwa pia na Rais wa Heshima wa TFF ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya CAF, Bw. Leodegar Tenga.
Rais wa CAF ameahidi kuisaidia TFF katika mipango ya maendeleo ya soka nchini ili kuongeza umoja kwasababu soka siku zote hujenga umoja na mshikamano.

Rais Karia na wenzake waliingia madarakani August 12 mwaka huu ambapo tangu waanze majukumu yao wamekuwa wakijitahidi kuhakikisha soka linapiga hatua kwa kutafuta wadhamini ambao watawezesha maendeleo hayo ya soka.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment