Home »
Habari Moto
» #YALIYOJIRI>>>Serikali imeanza kutengeneza sheria ya kutambulisha Dodoma kama Makao Makuu ya nchi.Fahamu zaidi hapa.
Serikali imeanza kutengeneza sheria ya kutambulisha Dodoma kama Makao
Makuu ya nchi na inatarajiwa kupelekwa bungeni ili kuondoa changamoto ya
migogoro baina ya Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) na wananchi.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye
Ulemavu), Jenista Mhagama alisema hayo bungeni hivi karibuni.Alisema
kuanzishwa kwa sheria hiyo kutarahisisha katika kuhamia Dodoma pamoja na
kuondoa migongano ya kisheria kati ya taasisi mbalimbali inayosimamia masuala ya ardhi mkoani Dodoma, ikiwa ni pamoja na kueleza mipaka ya CDA.
“Nataka wananchi wa Dodoma waamini kuwa serikali ina lengo la
kuhakikisha azma hii ya serikali kuhamia Dodoma inatekelezeka, ikiwa ni
pamoja na kuondoa migogoro yote kwa kufuata sheria na taratibu na
kunapokuwa na matatizo kwa ushirikiano wetu na wao inaisha,”
alisema.Alisema.
watahakikisha migogoro yote inaisha, lakini kwa kufuata
sheria ikiwa wananchi wana haki watapata na pale sheria inapowataka wao
waipe haki serikali waoneshe ushirikiano.Waziri huyo alisema mji wa
Dodoma utajengwa kisasa na kuonesha kweli ni makao makuu kama ilivyo
miji mingine duniani kwa kuwa kioo cha nchi ilivyo.Alisema katika
kuonesha nia ya serikali ya kuhamishia makao makuu Dodoma kabla ya
kumalizika kwa mkutano wa Bunge watakutana na wabunge wa mkoa huo na
wizara kujadiliana namna bora ya kuondoa changamoto hiyo.
Related Posts:
#YALIYOJIRI>>>Mwanamkakati wa Maalim Seif Aswekwa Ndani Na Jeshi La Polisi Zanzibar.Fahamu zaidi hapa.
Mwanamkakati
wa aliyekuwa mgombea urais wa Zanzibar, Mohamed Sultan Mugheiry,
maarufu kwa jina la Eddy Riyami, amewekwa ndani na Jeshi la Polisi mjini
Unguja kwa tuhuma za kumtukana Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Moham… Read More
Habari Katika Magazeti ya Leo siku ya Jumanne Ya Februari 23 yako hapa.
… Read More
#YALIYOJIRI>>>>Waziri Mkuu Majaliwa Awatembelea Waathirika Wa Mafuriko Iringa, Apokea Misaada Ya Maafa Ya Sh. Milioni 86/-.Fahamu zaidi hapa.
WAZIRI
MKUU Kassim Majaliwa amepokea misaada mbalimbali yenye thamani ya sh.
milioni 85.88/- kwa ajili ya wananchi walioathirika na mafuriko kwenye
vijiji vya kata ya Mlenge, tarafa ya Pawaga, wilaya ya Iringa vij… Read More
#YALIYOJIRI>>>Wizara Ya Fedha Yasema Makusanyo Ya Fedha Kwa Mwezi Yamefika Trilioni 1.79,Mchanguo Wote Wa Matumizi wa Pesa Uko Hapa.Fahamu zaidi hapa.
SERIKALI
imeendelea kupaa katika ukusanyaji wa mapato baada ya kukusanya hadi Sh
trilioni 1.79, ambazo imezipeleka katika huduma za jamii, ikiwamo
elimu, maji, miundombinu na miradi ya maendeleo.
Katibu
Mkuu wa Wiz… Read More
#YALIYOJIRI>>>Serikali Yapanga Bei Elekezi Kwa Hospitali Binafsi Ili Kupunguza Mzigo wa Gharama.Fahamu zaidi hapa.
SERIKALI
imesema itatoa bei elekezi katika sekta ya afya hivi karibuni baada ya
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kubariki bei hizo kuanza kutumika kwa lengo
la kuwapunguzia mzigo wa gharama wananchi.
Bei
elekezi kwa v… Read More
0 comments:
Post a Comment