Home »
Habari Moto
» #YALIYOJIRI>>>Serikali imeanza kutengeneza sheria ya kutambulisha Dodoma kama Makao Makuu ya nchi.Fahamu zaidi hapa.
Serikali imeanza kutengeneza sheria ya kutambulisha Dodoma kama Makao
Makuu ya nchi na inatarajiwa kupelekwa bungeni ili kuondoa changamoto ya
migogoro baina ya Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) na wananchi.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye
Ulemavu), Jenista Mhagama alisema hayo bungeni hivi karibuni.Alisema
kuanzishwa kwa sheria hiyo kutarahisisha katika kuhamia Dodoma pamoja na
kuondoa migongano ya kisheria kati ya taasisi mbalimbali inayosimamia masuala ya ardhi mkoani Dodoma, ikiwa ni pamoja na kueleza mipaka ya CDA.
“Nataka wananchi wa Dodoma waamini kuwa serikali ina lengo la
kuhakikisha azma hii ya serikali kuhamia Dodoma inatekelezeka, ikiwa ni
pamoja na kuondoa migogoro yote kwa kufuata sheria na taratibu na
kunapokuwa na matatizo kwa ushirikiano wetu na wao inaisha,”
alisema.Alisema.
watahakikisha migogoro yote inaisha, lakini kwa kufuata
sheria ikiwa wananchi wana haki watapata na pale sheria inapowataka wao
waipe haki serikali waoneshe ushirikiano.Waziri huyo alisema mji wa
Dodoma utajengwa kisasa na kuonesha kweli ni makao makuu kama ilivyo
miji mingine duniani kwa kuwa kioo cha nchi ilivyo.Alisema katika
kuonesha nia ya serikali ya kuhamishia makao makuu Dodoma kabla ya
kumalizika kwa mkutano wa Bunge watakutana na wabunge wa mkoa huo na
wizara kujadiliana namna bora ya kuondoa changamoto hiyo.
Related Posts:
#YALIYOJIRI>>>>Magufuli, Museveni wampelekesha Uhuru.Fahamu zaidi hapa.
Kenya yafufua mazungumzo ya ujenzi wa bomba la mafuta na Uganda, lakini njia yake bado yaumiza vichwa
Dar es Salaam. Uamuzi wa
Rais John Magufuli kukubali haraka mradi wa uj… Read More
Polisi Wavamia Nyumba ya Davido Marekani...Mashabiki Wamuokoa Asikamatwe.Fahamu zaidi hapa.
Mkali wa muziki nchini Nigeria, David Adeleke ‘Davido’, amedai kwamba
kutokukamatwa kwake na polisi kumetokana na mashabiki wake.
Wiki iliyopita, Davido alikuwa kwenye nyumba yake nchini Marekani,
lakini polisi walikuwa … Read More
DOGO JANJA AWAPA ZAWADI YA GARI WAZAZI WAKE.FAHAMU ZAIDI HAPA.
Baada ya Dogo Janja kununuliwa gari mpya aina
ya Mercedes Benz na bosi wake Madee na kumfanya kuwa na magari mawili, amedai
gari lake la zamani anawapelekea wazazi wake.
Hii ndio gari yake ya zamani amba… Read More
Dogo Janja amchana Young Dee, Amwambia asilete uteja wake kwenye picha za watu.Fahamu zaidi hapa.
Baada ya diss za mtandaoni hatimaye dogo janja amefunguka wazi
kuchukizwa na kitendo cha rapa Young dee kudiss post ya Babu tale kuhusu
chid benz akimtaka young dee kuacha kuleta #Uteja wake kwenye issue za
watu.
Akizun… Read More
Profesa Jay Afunguka Kuhusu Chid Benz.Fahamu zaidi hapa.
Mbunge wa Mikumi kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema), Joseph Haule ‘Profesa Jay’ (pichani) amesema hali ya Mbongo
Fleva, Rashid Abdallah Makwiro (31) ‘Chid Benz’ ni matokeo ya matumizi
yaliyobebea ya… Read More
0 comments:
Post a Comment