Thursday 12 May 2016

#MICHEZO>>>>TIMU TATU ZILIZOSHUKA DARAJA MSIMU HUU EPL.Fahamu zaidi hapa.

Hivi umeshaanza kuwaza itakuwaje kwenye michuano ya UEFA pale Leicester City Itakapo pangwa kundi moja na Bayern au Barcelona? Epushia mbali Madrid ambayo inaimalika kila kukicha.

Ligi ya EPL huwa ina sehemu kuu tatu, Ubingwa,Nne bora na mstari wa kushuka daraja hapo ndo watu huchukiana na makocha kugoma kutoa mkono kwa mwenzake.

 

Bingwa amejulikana tayari kwahiyo sehemu ya pili ni kugombania nne bora tayari ishajulikana Leicester,Arsenal na Spurs. Nafasi ya nne sasa ipo chini ya Manchester City au Man U japo mechi Manchester City inanafasi kubwa ya kukata tiketi.

 

Sehemu ya Tatu ya ligi hiyo ni kugombania kubaki ligi kuu, Aston Villa  tayari imeshashuka muda mrefu lakini usiku wa jana timu mbili zimeungana naye ambazo ni Norwich City na Newcastle Uinted. Sundeland imebaki ligi kuu baada ya kuibuka na ushindi dhidi ya Everton. Pole sana Mh. Rais msataafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete kwa kuwa hutakuwa na timu tena kwenye ligi ya EPL baada ya Newcastle kurudi daraja la kwanza.


0 comments:

Post a Comment