Sunday, 8 May 2016

#MICHEZO>>>VIDEO: MAGOLI YA YANGA WALIVYOIUA SAGRADA ESPARANCA.

Magoli ya Simon Msuva na Matheo Anthony yameiweka yanga kwenye mazingira mazuri ya kufuzu kucheza hatua ya makundi ya michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika.

Yanga wamepata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Sagrada Esparanca ya Angola, magoli yote yakifungwa kipindi cha pili cha pambano hilo.

Simon Msuva alianza kuifungia Yanga bao dakika ya 71 kipindi cha pili kwa kuunganisha kwa kichwa krosi ya Geofrey Mwashiuya kabla ya kabla ya Matheo kuipa Yanga bao la pili dakika za nyongeza kwa shuti kali akiwa nje ya takribani mita 25 kutoka golini.

0 comments:

Post a Comment