Home »
Burudani
» #YALIYOJIRI>>>>GADNER SIJUTIA KUMTUSI KOMANDO JIDE,MAMBO MAZITO YAIBUKA.Fahamu zaidi hapa.
SIKU chache baada ya kipande cha video kuonekana katika mitandao
ya kijamii, ikimuonesha mtangazaji maarufu, Gardner G Habash akitoa
maneno ya matusi kwa mkewe wa zamani, Judith Wambura ‘Jide’, ameonekana
kujutia kitendo chake hicho. Katika eneo ambalo linalotajwa kuwa ni
katika Ukumbi wa TCC Chang’ombe, Ijumaa ya wiki iliyopita, Gardner,
aliyejitambulisha kuwa ni Mtangazaji wa Clouds FM, alitoa maneno ya
kidhalilishaji kwa msanii huyo wa Muziki wa Kizazi Kipya, baada ya
kuulizwa na mashabiki kama alikuwa na matatizo na mtalaka wake. “Mimi
sina neno na yule mtoto wa kike, nime… (tusi) kwa miaka 15,” alisema
mtangazaji huyo, ambaye aliishi katika maisha ya ndoa na Jide kwa zaidi
ya miaka kumi, kabla ya kutengana miaka miwili iliyopita Akizungumza na
Risasi Mchanganyiko lililotaka kufahamu kisa na mkasa wa kutoa maneno
hayo, Gardner alishindwa kuongea akidai alikuwa katika kikao, lakini
alituma ujumbe mfupi wa maneno akisema;
Gardner, aliyejitambulisha kuwa ni Mtangazaji wa Clouds FM.
“Kaka pole kwa usumbufu, sitakuwa na cha kusema kwa sasa ili kuepusha
tafsiri isiyo sahihi, naomba nielewe mkuu. Asante.” Gazeti hili pia
lilimtafuta kupitia simu yake ya mkononi mwimbaji huyo wa kibao cha Ndi
Ndi Ndi, Jide lakini hakupokea.
Hata Meneja wake, Severin Mosha maarufu kama Seven, alipoulizwa kama
wana taarifa na kipande hicho cha video na mpango wao kuhusiana na
jambo hili, alisema wameiona lakini hawana la kusema kwa sasa. Katika
hali nyingine, Naibu Waziri wa Afya, Jinsia na Watoto, Dk. Khamis
Kigwangalla amekitaka Kituo cha Redio cha Clouds na Gardner kumuomba
radhi Jide.
Chanzo: Risasi Jumatano/GPL
Related Posts:
#BURUDANI>>>>>>Mwanamuziki Trey Songz Ambeep Juma Jux Kwa Kumuita Vanessa Mdee 'Baby'.Fahamu zaidi hapa.
Akisifika kama bingwa wa nyimbo za kutafutia watoto chumbani na pia
akiwa na mashabiki wengi zaidi wa kike, Trey Songz akimuita mpenzi wako
‘baby’ ni lazima moyo ukudunde!
Muimbaji huyo wa ‘Nana’ yupo Nairobi, Kenya alik… Read More
#BURUDANI>>>>TETESI za Bifu Kati ya Raymond na Harmonize Kutoka WCB, Meneja Wao Asema Haya.Fahamu zaidi hapa.
Meneja anayewasimamia wasanii wa WCB wakiwemo Harmonize na Raymond,
Ricardo Momo, amekanusha tetesi kuwa mafahari hao wamekuwa wakivimbiana
na kwamba kila mmoja anajiona bora.
Akiongea na mtangazaji wa kipindi cha Supa M… Read More
#BURUDANI>>>>MASKINI MSANII ROMA ANAELEKEA WAPI NA MUZIKI WAKE..ASHUSHWA KWA NGUVU FIESTA MORO KISA KUIMBA MATUSI.FAHAMU ZAIDI HAPA.
Jumapili ya septemba 18 ilikuwa ndio siku rasmi ya kihistoria kwa
mvua ya burudani kuwanyeshea wakazi wa Morogoro katika msimu huu wa
Fiesta.
Ni wasanii wengi na wakali ambao walikuwa wamepangwa kufanya show usiku
huo b… Read More
#BURUDANI>>>>Davido Achekelea Nyimbo yake Kutumika Katika Movie Huko Marekani.Fahamu zaidi hapa.
Msanii David Adeleke Adedeji ameonesha furaha ya hali ya juu baada ya
kuisikia nyimbo yake ya Skelewu ikichezwa katika movie kubwa huko
Hollywood Marekani iitwayo Qween of Katwe
Katika movie hii pia yupo mkenya aliyewe… Read More
#BURUDANI>>>>>Orodha ya Wasanii Watakaowania Tuzo za MTV MAMA 2016, Navykenzo, Diamond na Alikiba Ndani.Fahamu zaidi hapa.
Orodha
ya wasanii watakaowania tuzo za MTV MAMA 2016, Jumamosi ya Oktoba 22
kwenye ukumbi wa Ticketpro Dome, Afrika Kusini imetoka – kuna vipengele
tisa. Tanzania inawakilishwa na Alikiba, Diamond na Navy Kenzo.
Hii ni … Read More
0 comments:
Post a Comment