Friday, 11 November 2016

#YALIYOJIRI>>>>Mke Wa Rais Mama Janeth Magufuli Aruhusiwa Kutoka Hospitali ......Awashukuru Madaktari.Fahamu zaidi hapa.

Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli aliyekuwa amelazwa katika wodi ya Sewahaji ya Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam ameruhusiwa na kurejea nyumbani leo tarehe 11 Novemba, 2016 baada ya afya yake kuimarika.

Kabla ya kuondoka katika wodi ya Sewahaji alikokuwa amelazwa Mama Janeth Magufuli amewashukuru Madaktari na Wauguzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu mazuri aliyoyapata na pia amewashukuru Watanzania wote kwa kumuombea afya njema.

"Namshukuru sana Mungu kwamba afya yangu imeimarika, pia napenda kuwashukuru Madaktari na Wauguzi, nimepata huduma nzuri sana maana siku nilipoletwa hapa nilikuwa sina fahamu na hali yangu ilikuwa mbaya lakini mmenipigania na leo narudi nyumbani nikiwa na afya imara.

"Naomba pia niwashukuru Watanzania wote kwa kuniombea, nawahakikishie kuwa sasa nipo vizuri na madaktari wameniruhusu nirudi nyumbani ambako nitamalizia matibabu yangu" amesema Mama Janeth Magufuli.

Mama Janeth Magufuli alilazwa hospitalini hapo tangu Juzi tarehe 09 Novemba, 2016 baada ya kuugua ghafla na kupoteza fahamu.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
11 Novemba, 2016

Related Posts:

  • Polisi Wakamata Machungwa Yaliyoibiwa. Polisi wa huko jijini Seville nchini Hispania wakamata watu watano jana baada ya kufukuzana nao kwa kasi na ndipo hapo polisi waligundua tani hizo za machungwa zilizoibiwa ambazo watuhumiwa walikuwa wameyajaza ndani ya m… Read More
  • Kampuni ya TTCL Yafutwa. Akizungumza na waandishi wa habari, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Makame Mbarawa, amesema kuwa anamshukuru sana Rais Magufuli kwa kuona umuhimu wa kuona wa kuwa na shirika la mawasiliano madhubuti kwa ajili … Read More
  • TANZIA: Mzee Kingunge Ngombale Mwiru Afariki Dunia. Mzee Kingunge Ngombale–Mwiru amefariki dunia alfajiri ya leo.Tupo hapa na masikitiko makubwa.Poleni sana sana wafiwa na kijana wake Kinje (Mama yake alifariki 4/1/2018 na Baba yake leo)May his soul Rest in Eternal Peace. D… Read More
  • Mzee Kingunge Kuzikwa Leo Hii Hapa Ratiba ya Mazishi. RATIBA  ya mazishi ya aliyekuwa mwanasiasa mkongwe, Kingunge Ngombale Mwiru, iliyotolewa na familia yake jana inaonyesha atazikwa leo Jumatatu katika shughuli itakayoanza saa 9:30 hadi 11:30 katika makaburi ya Kinon… Read More
  • TCRA Yafafanua Matuzi ya Alama za Vidole Kwenye Usajili wa Laini. “Ndugu mteja katika kuboresha usajili wa laini za simu alama za vidole zitatumika kuanzia Februari 5, 2018. Kwa mawasiliano zaidi tembelea maduka yetu,” ni ujumbe ambao watumiaji mbalimbali wa mitandao ya simu nchi wamet… Read More

0 comments:

Post a Comment