Katika
hali isiyotarajiwa, jana Alhamisi mashabiki wa Yanga walioungana na wa
Simba, kwa pamoja kuipokea timu ya Simba ilipowasili mkoani Lindi
ilipokuwa inaelekea Mtwara kucheza dhidi ya Ndanda.
Simba
ambayo keshokutwa Jumapili itapambana na Ndanda kwenye Uwanja wa
Nangwanda Sijaona, ilifika Lindi na kupata fursa ya kufungua Tawi la
Simba Kwanza Kitomanga lililopo mkoani hapo.
Aliongeza
kuwa, wakati gari la Simba likitaka kuondoka eneo hilo, mashabiki wa
Simba na Yanga, waliomba lisiwashwe na badala yake wakaanza kulisukuma
kwa umbali wa zaidi ya kilomita tano.
Mwenyekiti
wa tawi hilo, Remy Mohammed Mpamba, amesema kuwa: “Kikosi cha Simba
kilifika hapa saa 9:15 alasiri na kilikaa kwa saa moja kabla ya
kuendelea na safari ambapo tulipata fursa ya kupiga nao picha huku Kocha
Joseph Omog akikata utepe wa kufungua tawi letu.
“Kitu
kizuri ambacho kila mmoja amekipenda hapa ni kwamba, watani zetu wa
jadi, Yanga, tulishirikiana nao kwa kila kitu na wote tulikuwa wenye
furaha huku tukiweka pembeni tofauti zetu.
Download Application ya Hebron Male Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi
Bonyeza Hapa CLICK HERE
0 comments:
Post a Comment