Thursday 18 February 2016

#YALIYOJIRI>>>CUF Yatangaza Maandamano Makubwa Dar es Salaam.Fahamu zaidi hapa.

Wanawake wa chama cha wananchi CUF maarufu kama JUKECUF wametangaza kufanya maandamano ya Amani siku ya tarehe 22,mwezi huu wa pili Jijini Dar es salaam yenye adhma ya kupinga hali ya kisiasa inayoendelea visiwani Zanzibar.

Akizungumza na wanahabari mapema leo mwenyekiti wa jumuiya hiyo  Mh severena mwijage amewaambia wanahabari kuwa maandamano hayo yataanzia ofisi kuu za CUF buguruni kuelekea ofisi ya makamu wa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh Samia Suluhu

Amesema kuwa jumuiya hiyo inatambua kwamba hali ya Amani iliyopo Zanzibar ikivurugika kwa kiasi kikubwa watakaoathirika ni kina mama na watoto hivyo wameona  ni bora kufikisha kilo chao hicho kwa makamu wa Rais ambaye ni Mwanamke mwenzao awasaidie.

Maandamano hayo yatapita barabara ya uhuru,ofisi ya mkuu wa mkoa Dar es salaam,karume,kariakoo,mnazi mmoja,Central polisi,barabara ya sokoine ,Bandarini,mahakama kuu,mahakama ya ardhi,Hadi ofisi ya makamu wa Rais.

Maandamano hayo bado hayajaruhusiwa na polisi licha ya polisi kupata barua kutoka CUF.

0 comments:

Post a Comment