Home »
Michezo
» #MICHEZO>>>Sababu 5 zinazoweza kumpeleka Messi Manchester City.Fahamu zaidi hapa.
Moja ya story ambayo inazungumziwa sana kipindi hiki ni tetesi za
kwamba Messi anaweza kujiunga na kocha wake wa zamani kwenyue club ya
Manchester City msimu ujao.
Hizi hapa ni sababu 5 ambazo zimechambuliwa kuonyesha uwezekano wa Messi kujiunga na Manchester City.
1)Guardiola connection
Pep anaweza kuwa kivutio kikubwa kwa Messi kwa sababu wamepata mafanikio
makubwa wakiwa pamoja ndani ya Barcelona. Muda wote Pep amekua shabiki
mkubwa wa Messi na anamuamini kiasi cha kumuacha afanye kile
anachofikiria uwanjani bila maelekezo yake akiamini hawezi kumuangusha.
Kila mchezaji angependa kuwa na kocha kama huyu.
2)Changamoto mpya
Messi ameshinda karibia kila taji ambalo anatakiwa kushinda akiwa na
Barcelona. Kuanzia binafsi hadi ya ki-team, sasa kwa mtu ambaye
anatafuta mafanikio mengine anaweza kuamua kwenda zake kutafuta
changamoto mpya. Mfano kushinda taji la ligi ya England.
3)Muda muafaka Barca kumuuza Messi
Sasa hivi ana miaka 28 na ana thamani kubwa, baada ya miaka miachache
ijayo lazima thamani yake itapungua na hawataweza kupata pesa nyingi
kama wakimuuza sasa hivi. Wanatakiwa kumuuza na ku-focus kwa vipaji
vyenye umri mdogo kama Neymar.
4)Kufata Pesa
Messi anaweza kuongeza mshahara wake kwa kiasi kikubwa sana kama
akihamia Etihad. Wamiliki wa Man City watamuangalia Messi kama faida
uwanjani na nje ya uwanja, hivyo basi mzigo watakaompa sio wa kitoto
kama kawaida ya warabu kwenye pesa hawana noma.
5)Marafiki
Sergio Aguero na Messi ni marafiki wa karibu sana. Wamecheza pamoja
wakiwa under 20 World Cup mwaka 2005 na pia wakashinda Gold Medal kwenye
Olympic pamoja. Messi ni baba wa ubatizo wa mtoto wa Aguero kuonyesha
kwamba hawa jamaa wapo karibu hadi kifamilia.
Related Posts:
#MICHEZO>>>ULISHANGAA ILE ISHU YA WACHEZAJI LEICESTER KUPEWA MAGARI, BAYERN WAO NI KILA MSIMU, KILA MCHEZAJI GARI.FAHAMU ZAIDI HAPA.
Hivi
karibuni mmiliki wa Leicester City, alitoa magari kwa kila mchezaji wa
kikosi hicho baada ya kufanikiwa kutwaa ubingwa wa England.
Vichai
Srivaddhanaprabha aliwapa wachezaji wake kila mmoj… Read More
#MICHEZO>>>HIKI NDICHO TFF WALICHOMWELEZA JERRY MURO, AFUNGUE TU MDOMO...PAAAA!...FAHAMU ZAIDI HAPA.
KATIBU MKUU WA TFF, MWESIGWA CELESTINE
Wiki
iliyopita Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro,
alitangaza kuendelea kupiga kazi kama kawaida na kwamba hatambui adhabu
yake ya kufungiwa mwaka… Read More
#MICHEZO>>>>Habari Njema Kwa Mashabiki wa Man United Kuhusu Usajili wa Mchezaji Paul Pogba Hii Hapa.Fahamu zaidi hapa.
Headlines za kiungo wa kimataifa wa Ufaransa aliyekuwa anaichezea klabu
ya Juventus ya Italia Paul Pogba kuhusishwa kujiunga na Man United,
zinaelekea kumalizika kwa kiungo huyo kurudi Man United toka aondoke
mwaka 2012.… Read More
#MICHEZO>>>WANAOIGEUZA YANGA ‘KUKODISHWA’ NI DHAMBI NA UDHAUFU WAO WA HOJA.FAHAMU ZAIDI HAPA.
MABINGWA wa England, Leicester City ni timu ya familia moja nchini Thailand.
Familia
hiyo inajulikana kwa jina la Srivaddhanaprabha, imeiongoza Leicester
City hadi kutwaa ubingwa. Leo kuna Watanzania wanataka kuingi… Read More
#MICHEZO>>>>SIMULIZI LA SERENGETI BOYS ILIVYOKOMAA NA WASAUZ LIKO HIVI.FAHAMU ZAIDI HAPA.
Ikicheza
mbele ya Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal
Malinzi na Naibu Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Rosemary
Chambe Jairo, timu ya soka ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17
maa… Read More
0 comments:
Post a Comment