Home »
Habari Moto
» #BREAKING NEWS>>>MHANDISI MANISPAA YA ILALA JIJINI DAR ES SALAAM NA WASAIDIZI WAKE WATUMBULIWA.FAHAMU ZAIDI HAPA.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Charles Kuyeko, akizungumza na
wanahabari kuhusu kumvua madaraka Mhandisi wa Manispaa hiyo,Japhery
Bwigane na wasaidizi wake wawili kwa tuhuma za kusimamia ujenzi wa
barabara za manispaa hiyo kwa kujengwa chini ya kiwango.
MANISPAA ya Ilala jijini Dar es Salaam imemvua madaraka Mkuu wa Idara ya
ujenzi, Mhandisi Japhery Bwigane na wasaidizi wake wawili kwa tuhuma za
kusimamia ujenzi wa barabara za manispaa hiyo kwa kujengwa chini ya
kiwango.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam wakati akitoa taarifa
hiyo, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Charles Kuyeko aliwataja
maofisa wengine wa idara hiyo waliosimamishwa kuwa ni Siajari Mahili na
Daniel Kirigiti ambao wamehamishwa idara hiyo ili kupisha uchunguzi
unaoendelea.
Kuyeko alisema kikao cha Baraza la Madiwani kimefikia uamuzi huo baada
ya manispaa kujiridhisha kuwa maofisa hao wamechangia kwa kiasi kikubwa
ujenzi wa barabara mbovu ndani ya manispaa hiyo.
Alisema baada ya kuingia madarakani kwa miezi mitatu walijaribu kutafuta
kero ndani ya manispaa ya Ilala ambapo walibaini idara ya ujenzi ina
malalamiko mengi kutoka kwa madiwani wa kata mbalimbali kwa sababu ya
kusimamia ujenzi wa barabara chini ya kiwango na hakuna hatua stahiki
zilizochukuliwa na maofisa hao.
Alisema madiwani hao walimlalamikia Mhandisi Bwigane kuwa amekuwa
akikaidi wito wao wa kujadili ujenzi wa barabara mbovu pindi
zinapobainika jambo ambalo limesababisha manispaa hiyo kuwa na barabara
nyingi mbovu.
Jitihada za gazeti hili za kumtafuta Mhandisi Bwigane ili kuzungumzia
kusimamishwa kwake kazi hazikuzaa matunda baada ya kupigiwa simu yake na
wakati wote kuwa imefungwa
Related Posts:
#YALIYOJIRI>>>>PICHA 5: Tingatinga Lilivyofukua mamilioni yaliyokuwa Yamefichwa ardhini.Fahamu zaidi hapa.
Kama
wewe unadhani huna fedha, basi kuna wengine ambao wamezichimbia
ardhini, tena kwa mamilioni. Benki ya chini ya ardhi iliyosheheni
mamilioni ya fedha, zilizoswekwa ndani ya mifuko myeusi ya plastiki na
kufukiwa mch… Read More
#YALIYOJIRI>>>>>Profesa Lipumba Apata Pigo, Baraza la Wadhamini CUF Lagoma Kumtambua, Lapanga Kufunga Jengo la Chama.Fahamu zaidi hapa.
TAMKO LA BODI YA WADHAMINI YA THE CIVIC UNITED FRONT (CUF – CHAMA CHA
WANANCHI) KUFUATIA KIKAO CHAKE KILICHOFANYIKA JANA, TAREHE 2 OKTOBA,
2016
Kwa kuzingatia hali iliojitokeza katika chama chetu cha THE CIVIC UNITED
… Read More
#YALIYOJIRI>>>>Tanzania na Congo DRC zimesaini mkataba wa makubaliano kutafuta mafuta Ziwa Tanganyika.Fahamu zaidi hapa.
Serikali
ya Tanzania na nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC),
wametiliana saini makubaliano ya kuimarisha ushirikiano wao katika
nyanja mbalimbali ikiwemo suala la ulinzi na usalama pamoja uchimbaji wa
mafuta … Read More
#YALIYOJIRI>>>>Waandamanaji Ethiopia wakishambulia kiwanda cha Dangote.Fahamu zaidi hapa.
Kiwanda cha kutengeneza simiti
kinachomilikiwa na tajiri wa Afrika, mfanyabiashara wa Nigeria Aliko
Dangote, kimeshambuliwa na waandamanaji katika eneo la Oromia, utawala
wa eneo hilo umesema katika taarifa yake.
Maan… Read More
#YALIYOJIRI>>>>>Waziri atolea maelezo taarifa ya serikali kuhakiki watumishi wanavyotumia mishahara yao.Fahamu zaidi hapa.
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Angellah J. Kairuki
amekanusha taarifa inayosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa
serikali ina mpango ya kuhakiki namna watumishi wake wanavyotumia
mishah… Read More
0 comments:
Post a Comment