Home »
Michezo
» #MICHEZO>>ENGLAND KUAMUA VITA YA HISPANIA UEFA.Fahamu zaidi hapa.
May 28 mwezi huu ndio fainali ya UEFA,
mashindano yenye msisimko wa hali ya juu duniani kwa ngazi ya vilab
ambayo itafanyika Italia katika mji wa Milan. Wakati hayo yakiendelea
UEFA imemtangaza mwamuzi Mark Cluttenburg kuamua mechi hiyo kati ya
majirani wasiopendana Real Madrid dhidi ya Atletico Madrid.
KITUKO
Moja ya matukio yaliyompa
umaarufu Clattenburg ni mechi ya kombe la ligi kati ya Liverpool na
Reading ambapo alibaini hana kadi ya njano baada ya kutaka kumzawadia
mchezaji wa Reading alipopapasa mfukoni hakuiona ndipo mwamuzi wa akiba
akamletea nyingine na kutoa adhabu hiyo.
Mwaka huu inawezekana ikawa neema
kwakwe kwani atachezesha fainali ya FA kati ya Manchester United dhidi
ya Crystal Palace. Kisha atachezesha fainali ya UEFA Champions League.
Hii inakumbusha Mwingireza Howard Webb alichezesha fainali ya UEFA
kisha fainali ya kombe la dunia.
Je naye atafika huko? kama unakumbuka
mchezo kati ya Manchester United na Chelsea 2012 alipompa Torres kadi
nyekundu kwa uzembe wake mwenyewe ambapo Torres alisukumwa lakini kadi
akapewa yeye. Leo hii amekuwa mtamu kama mcharo kweli ukitulia utaweza
kubadilika.
0 comments:
Post a Comment