Fainali ya Kombe la FA kati ya Yanga na
Azam FC, imepangwa kupigwa Juni 11,2016 Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania TFF, Jamal Malinzi, amethibitisha
hilo.
“Ratiba
inaonyesha hivyo na hiyo tumefanya hivyo ili kuzipa muda wa kutosha wa
maandalizi timu zote mbili kwasababu tuna fahamu zitakuwa zimetoka
kumaliza mechi za ligi ya Vodacom nap engine nyingine zitakuwa na
majeruhi na mapungufu mengine ya hapa na pale,”amesema Malinzi.
Chonde chonde Azam na Yanga hii ni
fursa nzuri ya kuandika historia ambayo itaishi daima kwenye soka la
bongo. Pia kocha Stewart Hall ni wakati wako sasa kuiaga Azam kwa kombe
ili nawe ujitengenezee heshima kwenye klabu hiyo.
0 comments:
Post a Comment