Home »
Michezo
» #MICHEZO>>>>STEWART HALL KUIPA AZAM MKONO WA KWAHERI.Fahamu zaidi hapa.
Siku moja baada ya TFF kuipoka Azam FC pointi tatu kutokana na
kumtumia Erasto Nyoni aliyekuwa anakadi tatu za njano kwenye mchezo wao
dhidi ya Mbeya City, kocha mkuu wa Azam FC Stewart Hall amefikia uamuzi
wa kuachana na kikosi cha matajiri wa Dar baada ya kutokea kwa sekeseke
hilo ambalo limeirudisha nyuma klabu ya Azam kwenye mbio za kuwania
ubingwa wa ligi msimu huu.
“Baada ya jana kukatwa pointi na kupoteza matumaini ya ubingwa,
Stewart Hall amethibitisha kwamba, ataachana na klabu ya Azam baada ya
mchezo wa fainali ya kombe la FA dhidi ya Yanga”, zinasema ripoti kutoka
ndani ya klabu ya Azam FC.
Stewart Hall ameuandikika barua uongozi wa Azam FC akiomba kujiuzulu
nafasi yake mara baada ya kumalizika kwa msimu huu, sababu ambazo
amezitaja Hall za kuamua kuachana na klabu hiyo ni kwamba, wachezaji
hawamuelewi anachowaelekeza na haoni kama kuna maendeleo kadiri siku
zinavyozidi kwenda.
Sababu nyingine iliyotajwa na kocha huyo raia wa England ni pamoja na
aina ya wachezaji waliopo kwenye kikosi chake kutokidhi matakwa yake
huku akidai haoni mustakabali wa baadaye ndani ya Azam FC.
Kwa mujibu wa habari kutoka TFF, katika mechi namba 156
iliyozikutanisha Mbeya City dhidi ya Azam kwenye uanja wa Sokoine,
Mbeya, Azam FC ilimchezesha Erasto Nyoni akiwa na kadi tatu za njano
kinyume na sheria huku wakitambua kufanya hivyo ni kosa kisheria.
Related Posts:
#MICHEZO>>>>SIMULIZI LA SERENGETI BOYS ILIVYOKOMAA NA WASAUZ LIKO HIVI.FAHAMU ZAIDI HAPA.
Ikicheza
mbele ya Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal
Malinzi na Naibu Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Rosemary
Chambe Jairo, timu ya soka ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17
maa… Read More
#MICHEZO>>>>HUYU NDIYE IBRA CADABRA, APIGA BAO LA PILI MAN UNITED IKIITWANGA LEICESTER CITY 2-1 NA KUBEBA NGAO YA JAMII.FAHAMU ZAIDI HAPA.
Manchester United XI: De
Gea, Valencia, Bailly, Blind, Shaw (Rojo 69), Carrick (Herrera 61),
Fellaini, Lingard (Mata 63, Mkhitaryan 90+3), Ibrahimovic, Rooney
(Schneiderlin 88), Martial (Rashford 70)
Subs not u… Read More
#MICHEZO>>>ULISHANGAA ILE ISHU YA WACHEZAJI LEICESTER KUPEWA MAGARI, BAYERN WAO NI KILA MSIMU, KILA MCHEZAJI GARI.FAHAMU ZAIDI HAPA.
Hivi
karibuni mmiliki wa Leicester City, alitoa magari kwa kila mchezaji wa
kikosi hicho baada ya kufanikiwa kutwaa ubingwa wa England.
Vichai
Srivaddhanaprabha aliwapa wachezaji wake kila mmoj… Read More
#MICHEZO>>>>YANGA YASEMA IMETUMA MAJINA TMS, TFF, CAF NA KILA KITU KIKO SAWA LABDA IWE HUJUMA INATENGENEZWA MAKUSUDI.FAHAMU ZAIDI HAPA.
Kumekuwa
na taarifa kuwa Yanga haikutuma majina ya wachezaji wake katika Mtandao
wa Usajili wa Kimataifa (TMS) na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF)
limekaririwa likithibitisha hilo.
Lakini
uongozi wa Yanga, umes… Read More
#MICHEZO>>>AVEVA AWAONGOZA VIONGOZI, WANACHAMA KUKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA UWANJA WA BUNJU.FAHAMU ZAIDI HAPA.
Viongozi
mbalimbali wa klabu ya Simba wakiongozwa na Rais wao, Evans Aveva
wamefika katika eneo la Bunju jijini Dar es Salaam, kufanya ukaguzi wa
maendeleo ya ujenzi wa uwanja wao.
Ujenzi
wa uwanja wa mazoezi … Read More
0 comments:
Post a Comment