Monday 19 December 2016

HAMADAI adai alitongozwa na Shilole, aeleza sababu ya kuachana naye.Fahamu zaidi hapa.

Mpenzi wa zamani wa Shilole, Hamadai amefunguka na kueleza jinsi alivyokutana na Shilole na kuanza mahusiano.

Muimbaji huyo mchanga wa bongofleva alifahamika mara baada ya kuwa katika mahusioano na Shilole.

Akiongea katika kipindi cha Enewz cha EATV, muimbaji huyo amesema kuwa kwa sasa ameamua kuachana kabisa na Shilole kwa sababu kuna mambo ambayo alikuwa akiona hayaendi sawa na sasa ameamua kujikita katika muziki wake.

“Shilole ndiye aliyenitongoza mimi na siyo mimi, na sasa nimeona niachane naye kwa sababu kuna vitu ambavyo nilikuwa naona haviendi sawa, pia mimi siwezi mzungumzia vibaya. Kabla yangu alikuwa na watu kadhaa ambao tayari ameachana nao, akawa na mimi na tukaachana na sasa ana mtu mwingine ambaye pia anaweza kuachana naye, hayo ni maisha yake na mimi siwezi kumuingilia” Alisema Hamadai.

Pia aliongezea kuwa yeye sasa hivi amejikita sana katika muziki na kuachana na Shilole hakujampunguzia chochote katika maisha yake.




Download  Application ya Hebron Male Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

                              Follow me instagra 

 

0 comments:

Post a Comment