Ukiwa
umetimia mwezi mmoja, baada ya Msaidizi wa Freeman Mbowe ambaye ni
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Benard
Saanane (pichani) kupotea, Jeshi la Polisi limesema linachunguza taarifa
za kupotea kwake ambazo ilizopokea kutoka kwa mtu aliyejitambulisha
kama rafiki wa Saanane Desemba, 5, 2016.
Wakati
akizungumza na waandishi wa habari, Desemba 21, 2016 Kaimu Mkurugenzi
wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, CP Robert Boaz amesema Jeshi la polisi
limefungua jalada la uchunguzi na kwamba taratibu za kiupelelezi za mtu
aliyepotea zilifuatwa na bado upelelezi wa suala hilo unaendelea.
“Tuanashukuru
wananchi wanaotupatia taarifa kuhusu tukio hilo, tunaahidi kwamba
taarifa hizo tutazifanyia kazi. Tunazidi kuwaomba wananchi wenye taarifa
za kupotea Saanane waziwasilishe katika kituo chochote cha polisi,” amesema.
Sambamba
na hilo, Kamishna Boaz amefafanua tukio la uzikwaji wa maiti saba
zilizokufa maji katika mto Ruvu, pasipo kufanyiwa uchunguzi wa kutambua
waliokufa na chanzo cha vifo vyao.
“Mtakumbuka
kati ya tarehe 6 hadi 12, 1016 huko mto Ruvu jeshi la polisi lilipata
taarifa ya kuonekana maiti saba zikiwa zinaelea mtoni kwa nyakati na
maeneo mbalimbali, baada ya taarifa hizo kupatikana askari na daktari
walifika eneo la tukio na kufanya uchunguzi wa kitaalamu,” amesema na kuongeza.
“Kutokana
na ukweli kwamba baadhi ya maiti zilikuwa zimeharibika, maiti 6
ziliamuliwa kuzikwa katika eneo la tukio na moja yenye unafuu ilipelekwa
hospitali ya wilaya ya Bagamoyo kwenye chumba cha maiti hadi pale
ilipozikwa na halmashauri baada ya maiti hiyo kutotambuliwa na mtu
yeyote.”
CP
Boaz amesema hatua zote za kitaalam zilifuatwa na kwamba upelelezi
unaendelea kufanywa ikiwemo wa kuwatambua marehemu hao na kujua chanzo
cha vifo vyao
Download Application ya Hebron Male Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi
Bonyeza Hapa CLICK HERE
0 comments:
Post a Comment