MODO aliyejaaliwa kuwa na figa matata, Jane Ramoy ‘Sanchi’ amefunguka
kuwa, shepu yake inampa madili ya kumuingizia mamilioni ya pesa hivyo
kuweza kuyaendesha maisha yake bila presha.
Akizungumzia usumbufu anaopata kutoka kwa wanaume wakware kutokana na
bambataa alilonalo, Sanchi alisema, hilo la usumbufu wa wanaume kwake
wala siyo tatizo ila anachoshukuru ni kwamba figa yake inampatia pesa
ndefu.
“Unajua kwa shepu hii niliyonayo, sitarajii wanaume wasini sumbue, kwa
hiyo hilo kwangu wala siyo tatizo, ninachoshukuru ni kwamba napata
madili ya kuwa modo kwenye video mbalimbali, matangazo na michongo
mingine, kwa hiyo namshukuru Mungu kwa kunipa figa hii” alisema Sanchi.
Download Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa
Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
0 comments:
Post a Comment