Friday 28 April 2017

Makubwa!!! Ndoa ya Nuh Mziwanda Kufungwa Upya.

Ni siku moja tu imepita tangu staa wa Bongo Fleva Nuh Mziwanda kupitia account ya Instagram kupost picha ya mtoto wake aliyebarikiwa katika ndoa yake, inadaiwa ndoa hiyo kuingia katika mvutano.

Inasemekana kuwa ndugu wa Nuh Mziwanda hawakuridhia ndoa ya ndugu yao iliyofungwa miezi kadhaa iliyopita kwa kuwa Nuh alibadili dini kufuata dini ya mke wake ambapo kupitia U-heard  ya XXL ya Clouds FM April 28 2017 mtangazaji Soudy Brown ameinasa sauti ya mke wa Nuh Mziwanda akimzungumza mama mkwe wake:

“Nilimwambia mama unachelewa, mwambie aniache. Na anajua kuwa mimi sijaolewa na mwanawe, ila anajua nimezaa tu na mwanawe. Kwenye sherehe ya harusi hakuwepo, alikuwa kwenye msiba. Yule mama ni mzee wa Kanisa, alikuwa anataka niende kanisani nibadili dini ndio niolewe.” – Mama ANYA
Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment