Friday 28 April 2017

Kikwete ni Rais Bora au Watu Wanamkomoa Rais JPM?.

Kikwete amekuwa kipenzi cha watu ghafla, kila anapoonekana hushangiliwa na kusifiwa, ilianza pale Msigwa alipotamka bungeni kuwa wamemmiss, ikaja alipoingia bungeni kumsindikiza mkewe, lakini pia hata juzi alipokuwa akiingia uwanjani katika sherehe za Muungano.

Marais wastaafu hatukuwahi kuona wakishangiliwa, si MKAPA, wala MWINYI hata Baba wa taifa sikumbuki kuona akiingia sehemu baada ya kustaafu na watu wakaanza tu kumshangilia bila sababu. Mara nyingi mzee Nyerere alishangiliwa hasa wakati wa speech zake tamu na zenye kugusa.

Swali linaloumiza kichwa, Je huyu Kikwete aliyelaumiwa kila kona wakati wa miaka yake ya URAIS ni kweli kwamba hatukutambua ubora wake wakati huo, au tunamshangilia ili tu kumuudhi na kumkomoa JPM ambaye amejipambanua kuhakikisha anarekebisha yale yaliyofanywa na kikwete?

Nimeshindwa kung'amua kimsingi hasa shangwe za wananchi kwa Kikwete, au wanamuinjoy tu, kama wasemavyo waswahili??


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment