Wednesday 26 April 2017

WOLPER Acharukia Wasanii Wenzake..Adai Ni Wanafiki wa Kiwango cha Lami.

Staa mwenye kiwango cha juu Bongo Muvi, Jacqueline Wolper Massawe amefunguka kuwa, wasanii wengi waliopo kwenye tasnia ya filamu ni wanafiki na wanafuata mkumbo, hawako kiuhalisia.
Akizungumza na Showbiz, wakati wa maandamano ya kupinga wizi wa kazi zao na uingizwaji na uuzwaji holela wa sinema za nje, Wolper alisema kuwa, wasanii wangekuwa na umoja wangeungana siku hiyo kwa ajili ya kujua hatima ya kazi zao wanazozifanya na zinazowaweka mjini, lakini kwa kuwa wengi ni wanafiki imeshindikana.
“Nachukizwa na unafiki Bongo Movi, kwa kweli unakera sana, hawako kiualisia ndiyo maana kufika tunapotaka ni ngumu sana,” alisema Wolper.



Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment