Thursday 20 April 2017

JIBU la Harmorapa Kuhusu Jinsia Yake Laibua Mshangao Mitandaoni.Fahamu zaidi hapa.

Mwanamuziki ambaye amekuja kwa kasi kwenye tasnia ya, Harmorappa au muite Kiboko ya Mabishoo leo amewaacha midomo wazi watu wengi kufuatia jibu lake alilolitoa alipoulizwa kuwa yeye ni mwanaume wa aina gani.

Akiwa katika kipindi cha Kikaangoni kinachorushwa na EATV, Harmorappa aliulizwa swali lililotumwa na shabiki aliyekuwa akifuatilia kipindi hicho ambalo liliuliza, “Wewe ni mwanaume wa aina gani?”  na akijibu swali hilo alisema, “Mimi ni strong woman.” 

Jibu hilo limewashangaza wengi kwa sababu Harmorappa ni mwanaume na hivyo wengi wameshindwa kuelewa kama alielewa swali liliuliza nini au alijibu kama utani.

Alipoulizwa kama anafahamu lugha ya Kiingereza, Harmorappa alisema anaielewa vizuri lakini tatizo ni kwenye kuongea.


“LUGHA YA KIINGEREZA NAIFAHAMU VIZURI LAKINI ILE KUONGEA ONGEA NDIYO SIWEZI” 

Aidha, amesema kuwa kwa sasa hana mpango wa kujiendeleza kimasomo hasa kwenda chuo labda ajifunze zaidi lugha ya Kiingereza. Kuhusu suala la kujiunga WCB, alisema, “Siwezi kujiunga WCB hata kwa shilingi ngapi, Sizuzuki na hela, maana kama ni hela hata mimi mwenyewe ninazo.”


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment