Kamishna wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi, Nsato Marijani
ameongea na waandishi wa habari mchana huu na kutolea ufafanuzi tukio la
mauaji ya Askari Polisi 8 lililotokea jana jioni huko Kibiti, Pwani.
CP Marijani ameeleza kuwa tukio hilo sio la kigaidi kama ambavyo imekuwa
ikivumishwa, bali ni tukio la kawaida la ujambazi ambalo halililazimu
Jeshi la Polisi kuunda Kanda Maalumu ya Kipolisi kwa Mkoa wa Pwani.
Aidha, amesisitiza kuwa, hilo ni tukio la kawaida na wala sio tukio la
kutisha na kuzua hofu bali imetokea tu bahati mbaya mapolisi kuuawa na
wao kama Jeshi Imara watazidisha mapambano na kudumisha ulinzi.
Mpaka sasa, wameshajibu mashambulizi yaliyowalaza chini majambazi 4 na
idadi yao itaongeza kwa kuwa imeundwa operesheni maalumu ambayo
haitokuwa na mzaha wala msamaha.
Nikimnukuu CP Nsato Marijani
"Ninasema wazi kwamba hiki ni kitendo ambacho hakikubaliki, mpaka sasa
nimekwishapoteza askari zaidi ya kumi. Ninaamini wanatosha.
Kuanzia sasa jeshi linakwenda kwenye operesheni maalumu, hatutokuwa na
mzaha wala msamaha, tutafanya kile ambacho Jeshi linapaswa kufanya.
Tutawafuata popote walipo, tutawashughulikia kikamilifu na hakuna ambaye
atakayebaki. Na mapambano haya hayana mwisho, yaani huu ni mwanzo
hayana mwisho. Askari 10 ni wengi sana.
Wananchi mtuwie radhi, mtuunge mkono. Katika hili mtaona sura halisi ya Jeshi la Polisi
Dawa ya moto ni moto, tuna uhakika tutawakamata, sasa hivi ni nane kwa nne lakini magoli yetu yatakuwa mengi kuliko wao.
Wale wote ambao walikuwa wanafikiria kufanya ujambazi wa aina hii wa kutumia silaha wajue kwamba dawa ya moto ni moto."
Download Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa
Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
0 comments:
Post a Comment