Wednesday, 21 February 2018

Asasi za Kiraia Zapaza Sauti Zimetaka Tume Huru ya Uchanguzi Kuundwa Kuchunguza Mauaji.

Asasi za Kiraia nchini zimetaka iundwe Tume huru ya uchunguzi wa kifo cha Mwanafunzi wa NIT, Akwilina Akwiline itakayoundwa na Taasisi za Dini, Vyombo vya Habari, Majaji, Mahakimu, Polisi na Baraza la Vyama vya Siasa.

Akizungumza mbele ya waandishi wa habari, Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Equality for Growth, Jane Magigita amesema kuwa Asasi za kiraia zimesikitishwa na vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu.

“Tunapendekeza iundwe Tume huru ya uchunguzi itakayohusisha Azaki, Taasisi za dini, vyombo vya Habari, Baraza la vyama vya siasa, wanahabari, Majaji, Polisi, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala bora kufanya uchunguzi juu ya vifo na vitendo vya utekwaji na utesaji,”-Magigita

“Pia ni kosa kubwa kuwaachia Polisi kujichunguza wenyewe katika matukio yanayowahusu,” -Magigita

Mbali na hilo, pia ameiomba Serikali itazame upya suala la upatikanaji wa Katiba mpya na mchakato wake uanze mwaka huu kwani ndiyo suluhisho la matatizo mbalimbali yanayotokea katika Jamii kwa sasa. 

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

Related Posts:

  • SOMA Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Jumanne. 16 Government Jobs Job Opportunity at CDM Smith, Finance and Accounting Manager Job Opportunity at CVPeople Africa, Secretary/Administrator Jobs at Meru University of Science and Technology (MUST) 2 Job Opportuniti… Read More
  • Mauzo ya Soko la Hisa Yazidi Kushuka. Mauzo ya Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), yameendelea kupungua hadi Sh1.5 bilioni Oktoba 6, kwa wiki ya pili sasa. Takwimu za DSE zinaonyesha wiki iliyoishia Septemba 22, mauzo ya soko hilo yalikuwa Sh53 bilioni ambay… Read More
  • Moto Mkubwa Wasababisha Maafa California, Marekani. Maeneo ya jimbo la California ambayo hukuza mizabibu yameathiriwa na moto mkubwa ambao unaenea kwa kasi sana na kusababisha vifo vya watu 10. Mamia ya watu wamehamishwa makwao na inakadiriwa kwamba zaidi ya nyumba 1,500 zi… Read More
  • IGP Sirro: Tutamshughulikia Mange Kimambi. Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Nyakoro Sirro amefunguka na kusema kuwa jeshi la polisi linatambua makosa ya kimtandao yanayofanywa na mwanadada Mange Kimambi na kusema kuwa jeshi la polisi linashughulikia su… Read More
  • Wanajeshi wawili wa Tanzania wauawa Huko Kongo. Askari wawili wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania, wameuawa kwenye mashambulizi makali yanayoendelea nchini Kongo. Tukio hilo limetokea katika eneo la Beni ambako Askari wa Umoja wa Mataifa wa kulin… Read More

0 comments:

Post a Comment