Asasi za Kiraia nchini zimetaka iundwe Tume huru ya uchunguzi wa kifo cha Mwanafunzi wa NIT, Akwilina Akwiline itakayoundwa na Taasisi za Dini, Vyombo vya Habari, Majaji, Mahakimu, Polisi na Baraza la Vyama vya Siasa.
Akizungumza mbele ya waandishi wa habari, Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Equality for Growth, Jane Magigita amesema kuwa Asasi za kiraia zimesikitishwa na vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu.
“Tunapendekeza iundwe Tume huru ya uchunguzi itakayohusisha Azaki, Taasisi za dini, vyombo vya Habari, Baraza la vyama vya siasa, wanahabari, Majaji, Polisi, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala bora kufanya uchunguzi juu ya vifo na vitendo vya utekwaji na utesaji,”-Magigita
“Pia ni kosa kubwa kuwaachia Polisi kujichunguza wenyewe katika matukio yanayowahusu,” -Magigita
Mbali na hilo, pia ameiomba Serikali itazame upya suala la upatikanaji wa Katiba mpya na mchakato wake uanze mwaka huu kwani ndiyo suluhisho la matatizo mbalimbali yanayotokea katika Jamii kwa sasa.
Download Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa
SOMA Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Jumanne.
16 Government Jobs
Job Opportunity at CDM Smith, Finance and Accounting Manager
Job Opportunity at CVPeople Africa, Secretary/Administrator
Jobs at Meru University of Science and Technology (MUST)
2 Job Opportuniti…Read More
Mauzo ya Soko la Hisa Yazidi Kushuka.
Mauzo ya Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), yameendelea kupungua hadi Sh1.5 bilioni Oktoba 6, kwa wiki ya pili sasa.
Takwimu za DSE zinaonyesha wiki iliyoishia Septemba 22, mauzo ya soko
hilo yalikuwa Sh53 bilioni ambay…Read More
Moto Mkubwa Wasababisha Maafa California, Marekani.
Maeneo ya jimbo la California ambayo hukuza mizabibu yameathiriwa na
moto mkubwa ambao unaenea kwa kasi sana na kusababisha vifo vya watu 10.
Mamia ya watu wamehamishwa makwao na inakadiriwa kwamba zaidi ya nyumba 1,500 zi…Read More
IGP Sirro: Tutamshughulikia Mange Kimambi.
Mkuu
wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Nyakoro Sirro amefunguka na kusema
kuwa jeshi la polisi linatambua makosa ya kimtandao yanayofanywa na
mwanadada Mange Kimambi na kusema kuwa jeshi la polisi linashughulikia
su…Read More
Wanajeshi wawili wa Tanzania wauawa Huko Kongo.
Askari
wawili wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania, wameuawa
kwenye mashambulizi makali yanayoendelea nchini Kongo.
Tukio
hilo limetokea katika eneo la Beni ambako Askari wa Umoja wa Mataifa wa
kulin…Read More
0 comments:
Post a Comment