Friday 29 January 2016

#MICHEZO>>>Mbwana Samatta akamilisha usajili katika timu mpya.Fahamu zaidi hapa.

 Mbwana Samatta atimae kapata timu mpya baada ya kutoka katika timu ya TP MAZEMBE,akiwa ametoka kwa mafanikio baada ya kuchukua Tuzo ya mwanasoka bora wa Afrika kwa wachezaji wanaocheza soka ndani ya Afrika.

Haya ni maneno ya Mbwana Samatta ambayo aliyoyaandika katika page yake ya facebook baada kufanyika kwa usajili."Leo nimeingia mkataba rasmi na Club yangu mpya ya FC Genk, mkataba wa miaka minne kucheza katika Ligi kuu ya Ubelgiji. Kama mnavyojua Ubelgiji ndio imekuwa chanzo kikubwa cha wachezaji wengi wakubwa na kikosi chao cha timu ya Taifa ni moja kati ya timu bora duniani. Namshukuru Mungu kwa fursa hii na nitaitumia ipasavyo".

0 comments:

Post a Comment