Wednesday 26 April 2017

SIMBA WAJIANDAE, BOCCO SASA YUKO VIZURI NA TAYARI KWA KAZI YA JUMAMOSI.

Kati ya mechi zinazosubiriwa kwa hamu ni Simba dhidi ya Azam FC na itakuwa mechi ya Kombe la Shirikisho.

Mechi hiyo itapigwa Jumamosi na wanachojivunia Azam FC kwa sasa ni kurejea kwa nahodha wao, John Bocco.


Bocco amerejea mazoezi siku chache zilizopita baada ya kuungana na wenzake.


Kabla alianza mazoezi ya taratibu akifanya peke yake chini ya uangalizi wa daktari.

Lakini sasa Bocco yuko fiti ameungana na wenzake ambao amekuwa akifanya nao mazoezi pamoja.


Bocco ni tishio kwa Simba na Yanga kutokana na uwezo wake mkubwa wa kupachika mabao kila anapokutana na timu hizo.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment