Friday, 9 September 2016

MICHEZO>>>Striker wa Simba aelekea uarabuni kufanya majaribio.Fahamu zaidi hapa.

Mshambuliaji wa klabu ya Simba Danny Lyanga amesafiri kuelekea Oman kwa ajili ya kufanya majaribio kwenye timu ya Oman Club.

Haji Manara amethibisha taarifa za kuondoka kwa Lyanga na kusisitiza mchezaji huyo amefuata taratibu zote na kuruhusiwa na klabu yake.

“Danny Lyanga amekwenda Muscat, Oman kwa ajili ya kufanya majaribio kwa muda wa wiki mbili kwenye timu ya Oman Club na kama atafanikiwa sisi Simba hatuna tatizo katika kumwachia mchezaji kwenda kucheza soka la kulipwa”, amethibitisha Haji Manara afisa habari wa klabu ya Simba.

“Oman Club ni timu kubwa, ni kama Simba au Yanga kwa Tanzania, kama atafanikiwa ni faida kwake, kwa klabu na taifa. Ameonfoka kwa kufuata taratibu zote za Simba.”

Lyanga amekuwa hana nafasi ya kudumu kwenye kikosi cha kwanza cha Simba kutokana na uwepo wa wageni Hamisi Kiiza (msimu uliopita), Mavugo, Blagnon na mzawa Ibrahim Ajib (msimu huu).

0 comments:

Post a Comment