Home »
Habari Moto
» #YALIYOJIRI>>>>Wilaya 43 ziko Hatarini Kukumbwa na Njaa.Fahamu zaidi hapa.
Serikali imesema kuwa nchi ina hifadhi kubwa ya chakula kutokana na
mavuno ya msimu uliopita ingawa kuna wilaya 43 zenye upungufu wa chakula
kutokana na mavuno yao kuwa chini hali iliyosababishwa na mabadiliko ya
tabia nchi.
Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, William Ole Nasha amesema hayo
jana wakati akizindua tovuti ya wakala wa hifadhi ya chakula nchini
(NFRA) mjini Dodoma.
Mhe. Ole Nasha amesema kuwa kwa sasa serikali ipo katika hatua za mwisho
za kuratibu uuzaji wa chakula nje ya nchi bila kuathiri hifadhi ya
chakula na kuwatoa hofu wananchi wenye wasiwasi wa kukumbwa na baa la
njaa.
Naibu waziri huyo ameongeza kuwa kwa tathmini waliyoifanya imebaini kuwa
nchi nyingi za ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika
zinakabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula hivyo serikali itatengeneza
mifumo mizuri ya kupeleka chakula hicho nje ya nchi.
Baada ya kuzindua tovuti hiyo ya wakala wa chakula nchini, uhifadhi wa
nyaraka za serikali kwa njia ya makaratasi umepitwa na wakati lakini pia
akaongeza kuwa hata wizara nyingine zimeanzisha tovuti lakini ni kama
zimekufa kwa sababu haziweki taarifa za mara kwa mara.
Related Posts:
#YALIYOJIRI>>>>Askofu Gwajima amjibu Katibu Mkuu wa zamani wa CCM, Yusuf Makamba aliyemuita muongo.Fahamu zaidi hapa.
Askofu
wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amemjibu katibu mkuu wa
zamani wa CCM, Yusuf Makamba aliyemtuhumu kuwa ni mwongo akisema leseni
yake ni ya kuendesha magari makubwa na siyo vibajaji na maguta. … Read More
#YALIYOJIRI>>> Kauli ya CHADEMA baada ya wanachama wake kutangaza kujiunga CCM.Fahamu zaidi hapa.
Wakati
wa Mkutano Mkuu wa CCM jana mjini Dodoma, Chama cha Demokrasi na
Maendeleo (CHADEMA) kiliwapoteza wanachama wake watatu baada ya
kutangaza rasmi kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM).
Wanachama
hao waliokih… Read More
#YALIYOJIRI>>>>Programu za vyuo vikuu ambazo hazijasajiliwa na TCU na NACTE kufutwa.Fahamu zaidi hapa.
Na:
Lilian Lundo -Maelezo
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Bi.
Maimuna Tarishi ameitaka Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) na Baraza la
Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) … Read More
#YALIYOJIRI>>>Ripoti ya Jeshi la Polisi Dar es Salaam Baada ya Kumalizika kwa zoezi la uhakiki wa silaha......Pia Wamezungumzia Kiasi Walichokusanya Ndani ya Siku 6.Fahamu zaidi hapa.
Jeshi
la Polis kanda Maalumu jijini Dar es salaam limekamata watuhumiwa sugu
1,065 kwa makosa mbalimbali yakiwemo unyang’anyi wa kutumia nguvu, wizi
wa maungoni, wapiga debe, wavuta bangi, kikosi cha mbwa mwitu,
watuhum… Read More
Habari Katika Magazeti ya siku ya Leo Jumatatu ya July 25 yako hapa.
… Read More
0 comments:
Post a Comment