Sunday 28 June 2015

FAHAMU RAISI TUNAE MUITAJI NI WANAMNA GANI???.,..




TUREJEE KWENYE KAMUSI KUTAFUTA MAANA YA NENO RAIS NA RAHISI KABLA YA KUTANGAZA NIA
Habari ya wewe ndugu yangu popote ulipo ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea vyema na majukumu yako katika ujenzi wa taifa, leo nimewiwa kuzungumzia mada yenye kichwa habari tajwa hapo juu kwa kuwa nimeona idadi inayovuta hisia za watu wengi kwenye suala la watangaza nia wa chama chetu tawala CCM. Unaweza kujiuliza mpaka inafika idadi kubwa ya watu kwa kiasi kile ni utashi wa kisiasa,kukua kwa kidemokrasia,kuona ikulu ni patamu kama ndizi kisukari au mithili ya asali napata shida kuelewa jambo hili kwani bado najiuliza hawa watangaza nia wote wanazani kupewa ridhaa ya kuwa RAIS ni RAHISI au wanajua wanachokifanya??
Mimi binafsi nimewahi shuhudia demokrasia ya kweli darasani wakati wa kumchagua kiongozi wa darasa wale wenzangu wa st. kayumba tulikuwa tukiwaita monitors/monitress (kiranja) pamoja na kuhisi kuwa hii ni ngazi ya chini kabisa kujifunza uongozi au kuonesha kuwa wewe ni kiongozi wa badae sijawahi kuona wagombea hata ukiranja wakifika kumi katika darasa labda walikuwa wakiofia ni nani atapiga kula kama wote tutaamua kuwa wagombea.
Agenda zangu binafsi au maswali ninayojiuliza kutokana na watangaza nia kuwa utitiri (wengi kupita kiasi)
1.   Ina maana wote hawa hakuna mwenye imani na mwenzake kuwa ni kiongozi anayestahili, sikiliza hotuba zao utanielewa tu, kila mtu anasema nitafanya hiki nitafanya kile sio kama huyu wala sio kama yule kwani yule na yule pale ni mafisadi au sababu wanazozijua wao binafsi.
2.   Au ndio maandalizi ya goli la mkono kama alivyosema kiongozi wetu katibu wa itikadi na uenezi ili mradi tu refa asione? Naanza kujiuliza haya kwakuwa hawachelewi kutuletea hesabu za sayari ya tano(jupiter) watangaza nia 40 wakitimiza masharti ya kuwa na wadhamini nchi nzima kwa kila mkoa na kila mmoja kufikisha idadi tajwa ya wadhamini ukizisha mara 40 mara mikoa yote unaweza pata mtaji mzuri wa kula ambazo wazee wa goli la mkono wanaweza kutuambia ni mtaji wao wa kuanzia kama kura wenye uhakika nazo kwani leo hii mtu awezi kuidhamini yanga tena akiwa mwanachama hai wa yanga alafu akashangilia simba sijui kama tunaelewana wandugu.
3.   Hivi walimu walio kuwa wakitufundisha methali,nahau,vitendawili,misemo na maneno mengi ya busara kama FIKIRI KABLA YA KUTENDA walikuwa hawajawahi kuwafundisha hawa wenzetu au mimi nitakuwa nimepanic?? Kama mtu unaweza fikiri kabla ya kutenda ni bora ukajipima,ukapima na upande wa pili na kukubali matokeo kwani nafikiri wapo wengi tu katika kundi la watu 40 ambao wanajua fika kabisa kuwa kutaka ridhaa ya URAIS si RAHISI na wanajua kabisa kuwa sifa,vigezo na hata mvuto wa kisiasa hawana ila wamekazana na kuchukua fomu.
Tutaendelea tena kesho Mungu akipenda, nchi yangu bado changa wacha nijikongoje kwenda kuijenga nchi mie, wengine watakuja kupaka rangi wakishamaliza kutuletea maigizo na kutufanya kama watoto. Uwazari tu ulikuwa changamoto sasa ili la URAIS sijui wanalichukuliaje???




0 comments:

Post a Comment