Ndugu
 waandishi wa habari, kwa heshima kubwa ya kutambua nafasi yenu muhimu 
kwenye jamii, nimewaita hapa ili tushirikiane kuujuza umma kwamba tupo 
kwenye wakati mzuri wa haki kuonekana ikitendeka dhidi ya Mkuu wa Mkoa 
wa Dar es Salaam ambae kwa vielelzo vyote anatambulika kama Daudi Albert
 Bashite lakini wengi wanamfahamu kama Paul Makonda.
Ndugu waandishi wa habari, huu ni mwanzo, na kwa hakika ni mwanzo mwema wenye kuashiria kuwa mwisho wa Daudi Bashite umewadia.
Ndugu
 waandishi wa habari, mtakumbuka kuwa 22 Machi 2017 mwaka huu, 
niliwasilisha mashitaka yangu dhidi ya Daudi Bashite kwa Tume ya Maadili
 ya Viongozi wa Umma, kutaka achukuliwe hatua za kinidhamu kwa kukiuka 
maadili ya utumishi wa umma na kukosa sifa yakuwa kiongozi si tu DSM 
bali Tanzania kwa ujumla.
Mashtaka yangu tume yalikuwa ni yafuatayo;
1.
 Kugushi vyeti vya kitaaluma kuliko fannywa na RC makonda huku akijua 
fika kuwa vyeti anavyotumia vya taaluma si vyake wala si muhusika hivyo 
kujiita PAUL CHRISTIAN MAKONDA huku akijua fika kuwa yeye ni DAUDI 
ALBERT BASHITE, amekiuka sheria za nji nakutenda jinai.
2.
 Kula kiapo cha utii na uaminifu mbele ya Mheshimiwa Rais kwa uhusika wa
 kugushi ni kosa kubwa sana kisheria,huku akijua fika kuwa Rais alipaswa
 amuapishe yeye kama DAUDI ALBERT BASHITE na siyo PAUL CHRISTIAN 
MAKONDA.
3.Kujipatia
 Mali kama magari na vinginevyo kinyume na maadili ya viongozi wa umma, 
ambapo zawadi zote unazopokea unapaswa kutangaza hadharani, ikiwemo 
kupata mali hizo kwa wahusika ambao amekuwa akiwatangaza hadharani na 
kuwatuhumu kujihusisha na uuzaji wa madawa ya kulevya.
4.Kukiuka
 Misingi ya utawala bora haki za binadamu na utawala wa sheria kwa 
kutuhumu watu ovyo hadharani kuwa walijihusisha na biashara ya madawa ya
 kulevya kabla ya kukutwa na hatia na kisha wengine kuachiwa huru baada 
ya kubainika hawakutenda makosa hayo; kinyume kabisa na sheria ambapo 
mtu anatakiwa kutangazwa hadharani anapokutwa ametenda makosa.
5.
 Shitaka la mwisho lilikuwa ni la Uvamizi wa kituo cha kirusha matangazo
 ya redio na runinga cha Clouds media, ambapo akijua kuwa maadili ya 
viongozi wa umma, hayaruhusu kiongozi kushurutisha au kulazimisha jambo 
lolote kwakutumia madaraka yake kama kiongozi, ambapo mtuhumiwa alitenda
 kosa la kutaka kutumia nguvu kurusha kipindi cha kumkashifu Kiongozi wa
 dini wa Maknisa ya Ufufuo na Uzima almaarufu kamam Askofu Josephat 
Gwajima.
Ndugu
 waandishi wa habari, jana Aprili 12, nilipokea barua kutoka kwa 
Kamishna wa Tume, Jaji Harold R Nsekela akinijulisha kuwa Tume ya 
maadili ya viongozi wa Umma imekubali Mashtaka yangu dhidi ya mkuu wa 
mkoa wa Dar es salaam, na kunitaarifu kuwa wameanza kuyafanyia kazi 
mashitaka yote.
Ndugu
 waandishi wa habari, taarifa hiyo ya Kamishna wa Tume ya Maadili ya 
Viongozi wa Umma, imetoa mwanga mkubwa kwamba HAKI ambayo wengi wamekuwa
 wakiiomba, sasa Mwanga umeanza kuonekana.
Hivyo
 niwaombe wapenda haki wote popote walipo tushirikiane kwa hili ambalo 
mkuu wa mkoa amekuwa ni kero jijini Dar es salaam, Tupeane ushirikiano 
wa kuniongezea vielelezo vingine zaidi ya vile nilivyowasilisha Tume 
yaani vyeti na nakala zingine za mali kama nimesahau jambo lolote.
Mimi
 mlalamikaji na mashahidi wangu muhimu tupo tayari, mbali na matukio ya 
utekwaji na upoteaji wa watu lakini tumeendelea kutaka kuona mwisho wa 
kero hii jijini Dar es salaam, hivyo wakati wowote shauri litakapo anza 
kusikilizwa kwenye baraza la maadili ya viongozi wa umma, tutakuwa 
mstari wa mbele kutaka haki itendeke.
Wenu
Katika upiganiaji haki
BONIFACE JACOB
MSTAHIKI MEYA
MANISPAA YA UBUNGO
Download Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa
Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
 









 




 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment