Charles
Borniface Mkwasa kocha wa timu ya taifa ya Taifa Stars ameamua kufanya maamuzi
ya ziada baada ya Timu za Azam
na Timu ya Yanga
kutowaruhusu wachezaji wake kujiunga na kambi ya Taifa Stars August 9 na badala yake
kuendelea na maandalizi yao ya mchezo wa Ngao ya Hisani utakaopigwa August 22.
Wachezaji walioongezwa kwenye kikosi cha Taifa Stars ni golikipa Saidi Mohamed, Vicent
Andrew,
kutoka Mtibwa
Sugar, Mohamed Hussein (Tshabalala) na Ibrahim
Ajib,
kutoka Simba, Hamis
Ally na
Juma
Mbwana
kutoka KMKM, Tumba
Swed
kutoka Coast
Union, Samwel Kamuntu kutoka JKT Ruvu na
Ibrahim Hilka
kutoka klabu ya Zima moto ya Visiwani Zanzibar sambamba na golikipa wa Tanzania Prisons Mohamed
Yusuph
ambae bado hajawasili
0 comments:
Post a Comment