Tuesday 18 August 2015

#YALIYOJIRI>>MAKALLA ATEMBELEA MIRADI YA MWAUWASA JIJINI MWANZA HII LEO.


Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Amos Makalla akikagua mradi wa majisafi katika Kituo cha Majisafi cha Capri Point, akiwa pamoja na Mkurugenzi wa MWAUWASA, Inj. Anthony Sanga.

Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Amos Makalla akiwa kwenye mradi wa majitaka katika Kituo cha Kusukuma Majitaka cha Makongoro
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Amos Makalla akiambatana na Meneja Msaidizi wa Operesheni ya Tiba ya Maji (Sanitation Operation), Inj. Salim Lossindilo katika mradi wa tiba ya maji (sanitation) Butuja, unaopokea majitaka kutoka Makongoro na kuyatibu na kutumika kwa ajili ya matumizi mengine.

Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Amos Makalla akiwa pamoja na Bodi ya MWAUWASA, wafanyakazi wa MWAUWASA na maafisa wa Wizara ya Maji alipotembelea ofisi ya MWAUWASA, Capri Point. Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Amos Makalla leo ameendelea na ziara yake Kanda ya Ziwa kwa kutembelea miradi ya Mamlaka ya Majisafi na Mazingira, jijini Mwanza (MWAUWASA) na kukagua utekelezaji na maendeleo ya miradi ya maji mkoani Mwanza. Aidha, Mhe. Makalla aliweza kujionea ujenzi wa jengo jipya la MWAUWASA, Isamilo na kuzungumza na wafanyakazi wa MWAUWASA katika hafla fupi ya kuwazawadia wafanyakazi waliofanya kazi kwa uaminifu kwa zaidi ya miaka 15 katika ofisi za MWAUWASA zilizopo Capri Point.


0 comments:

Post a Comment