Home »
Michezo
» #MICHEZO>>>>ROONEY AACHWA KIKOSI CHA MAN UNITED KINACHOWAFUATA FEYENOORD.FAHAMU ZAIDI HAPA.
Manchester United wametangaza kikosi chao cha wachezaji 20
kitakachosafiri kwenda kuvaana na Feyenoord kwenye mchezo wa Europa
huku Rooney na Henrikh Mkhitaryan wakitajwa kuachwa kwenye msafara huo.
Jesse Lingard, ambaye alitolewa wakati wa mapumziko kwenye mchezo
waliopoteza dhidi ya mahasimu wao Manchester City pia jina lake halipo,
huku Antonio Valencia pia akikosekana.
Tayari Jose Mourinho amethibitisha kwamba Marcus Rashford ataanza
kwenye mchezo dhidi ya Eredivisie, huku wachezaji kama Timothy
Fosu-Mensah na Memphis Depay wakitazamiwa kuanza.
Mkhitaryan, ambaye ameripotiwa kukosa furaha katika klabu hiyo yenye
maskani yake Old Trafford kutokana na namba anayochezeshwa, hakujumuika
kwenye mazoezi na wenzake mapema kabisa wakati wakijiandaa kuelekea
Rotterdam, wakati Phil Jones akiwa ni mchezaji mwingine ambaye hakufanya
mazoezi.
Kikosi kizima cha United kinachosafiri hiki hapa: De Gea, Romero,
Johnstone; Darmian, Bailly, Blind, Fosu-Mensah, Rojo, Smalling; Carrick,
Fellaini, Herrera, Mata, Memphis, Pogba, Schneiderlin, Young;
Ibrahimovic, Martial, Rashford.
Related Posts:
BAADA YA FIFA KUMFUNGIA MESSI MECHI NNE, BARCELONA YATOA INACHOKIAMINI.FAHAMU ZAIDI HAPA.
Baada
ya Lionel Messi kufungiwa mechi nne na Shirikisho la Soka la Kimataifa
(Fifa) baada ya kumshushia matusi mwamuzi wa pembeni, Klabu ya FC
Barcelona imetoa tamko.
FC Barcelona imesema haiungi mkono waamuzi kuny… Read More
HII NDIYO KAULI YA YANGA KWA WACHEZAJI WANAOTAKA KUONDOKA.FAHAMU ZAIDI HAPA.
Uongozi wa Yanga, umewataka wachezaji wote wanaotaka kuondoka, kusema mapema.
Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa amesema klabu hiyo kongwe ingependa mambo kwenda kwa mpangilio.
“Kama kutakuwa na mcheza… Read More
RONALDO AMPIGA BAO LIONEL MESSI KWA KIPATO HADI SASA, NEYMAR AMUACHA BALE.FAHAMU ZAIDI HAPA.
Mshambuliaji wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo ameongoza kwa kuwa mwanasoka mwenye kipato zaidi kwa msimu wa 2016-17 hadi sasa.
Ronaldo
tayari ameingiza kitita cha pauni milioni 75.62 na amempiga bao
mpinzani wake mkubwa… Read More
OZIL SASA ACHOSHWA NA MASHABIKI ARSENAL WASIOISHA LAWAMA, ATOA POVU.FAHAMU ZAIDI HAPA.
Kiungo nyota wa Arsenal, Mesut Ozil ameonekana kuchoshwa na lawama za mashabiki wa Arsenal ambao ameamua kuwatolea uvivu.
Ozil
raia wa Ujerumani, amesema anaamini amefanya vizuri katika soka kabla
hajatua Arsenal na… Read More
YANGA YAKWAMA KUWAPELEKA WAARABU UWANJA WA KIRUMBA.FAHAMU ZAIDI HAPA.
Kuna kila dalili Yanga itabaki jijini Dar es Salaam na kucheza na kikosi cha MC Alger kutoka Algeria.
Awali Yanga ilitaka kucheza mechi yake hiyo mjini Mwanza kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, mechi ambayo imepangwa kucheza… Read More
0 comments:
Post a Comment